WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Saturday, January 2, 2016

YESU ANASEMA NJONI KWANGU NIPO KWA AJILI YENU.



JANUARY 2

Tukisoma kutoka katika kitabu cha 2 cha Wakorito 4:7; matatizo na majaribu ambayo tunakumbana nayo katika maisha yetu ya kila siku bililia inatueleza ni ya muda tu kama tunaamini ukuu wa Mungu. Jukumu letu ni kuamini katika ukuu wa kazi ya Mungu. Tunatakiwa kuendelea kuamini kuwa tukiweza kufungua mioyo yetu na kuukaribisha utakatifu wake ndani yetu tutafanikiwa; lakini bila nguvu ya Mungu sisi sio kitu na hatuwezi kitu chochote. Uwezo wa kufikiri, uwezo wa ubunifu, uwezo wa kuongea vizuri na hata mafanikio yote ambayo leo tunajivunia ni zawadi kutoka kwake. Nani aijuaye kesho? Kesho iko mikononi mwa Mungu peke yake;

Kumbusho kubwa hapa ni hili hakuna kitu chochote kinachoshindikana mbele ya Mwenyezi Mungu; hata kama tunakuwa na shida au maumivu tunakumbushwa kuwa maumivu ni sehemu ya maisha na ukuaji wa maisha ya ukristo ndani yetu. Tunatakiwa kutumia maumivu tunayoyapata katika maisha yetu ni sehemu ya kukua kwetu kiimani.Tunaaswa kuwa ushindani mkubwa amabo daima tunapambana nao ni mapigano ambayo yapo ndani ya miili yetu yetu kati ya nguvu ya mwili na nguvu Roho; Nguvu ya mwili ina jumuisha: matamanio ambayo ndio yanatawala maisha yetu kwa kiasi kikubwa kama, choyo, ubinafsi, kutukuwa na subira; kushindwa kujishusha hii inahitimiswa na dhana ya kuwa sisi ni wafalme wa maisha yetu na hatuhitaji msaada wa Mwenyezi Mungu katika mafanikio yetu hapa duniani.

Nguvu ya roho ni ile khali ya kumtegemea Mungu kuwa yeye ni kila kitu kila jambo nzuri au bay ambalo lio mbele yetu ni kazi ya mikono yake na inatupasa kushukuru; Unyenyekevu ni silaha inayotumika kwa wale wote ambao hutegemea nguvu ya Kiroho; Hapo ndipo yesu anajidhihirisha kwa usemi huu wa Njoni kwangu nami nitawasaidia katika shida zenu;Mungu pekee ambaye yeye hutuongoza katika mapito yake ambayo ni sahihi lakini tunatakiwa tuweze kusikia sauti yake ili uweze kukanyaga kwenye mapito yaliyo sahihi;

Mara nyingi tunaendelea kulalamika kuwa Mungu hasikilizi shida zetu na kwa nini shida zetu zinaendelea kudumu kwa muda Mrefu? Tatizo ni dogo tunashindwa kuwa wanyenyekevu wakusikiliza sauti yake bali sisi tunaendeleza kiburi chetu na tunajifanya hatusikia sauti ya bwana na huo ndio unakuwa mwanzo wa upotevu.

Tunatakiwa kusikiliza neno la mungu ambalo ndilo ngao kwani neno la mungu ni ngao salama kwa ajili ya ukombozi wetu na baraka katika maisha yetu. Ni kweli kabisa unaweza pita katikati ya bonde ka mateso kumbe likawa linakutayarishia na kukujengea daraja la baraka.Tumesahau kuwa kama tunaishi katika imani ya kweli tukumbuke kuwa daima mungu hugeuza kilio kuwa furaha kubwa sana sana.

Jukumu letu la msingi ni kuwa tayari kubadilika na kumwamini Kristo kama ni njia pekee ya utatuzi wa maumivu katika maisha yetu; tukumbuke kuwa maumivu tunayoyakabili kila siku yanaweza tu kukoma kama tutakuwa tayari kumkaribisha Kristo ndani ya maisha yetu. Kwani alitueleza kuwa njoni kwangu wote wenye kuelemewa na mizigo nami nitawapa faraja tukikumbuka kuwa yeye anapobeba mizigo yetu huondoa kabisa maumivu sisi wenyewe hatuwezi kuyaondoa.

siku ya leo inatupasa kutafakari kuhusu umuhimu wa kujijengea IMANI ya kweli ili tuweze kufanikiwa katika kufanikiwa katika maishayetu. Endeleaa kutembea nami katika tafakari hii muhimu ya maisha yetu na kuutafuta soluhisho la kweli kuhusu mizigo yetu.


No comments:

Post a Comment