WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Thursday, June 30, 2016

TUMEPEWA UHURU WA MAAMUZI(FREE WILL)- TUNAUTUMIAJE?


June 30       

Tafakari yetu leo tunaangalia matumizi ya uhuru ambao mwenyezi Mungu ametujalia sisi wana wa Adamu; (free will) tukijikita zaidi katika uhuru wa wakovu katika maamuzi yetu na utumishi wetu mbele ya Mungu; kwa maneno mengine ni uwezo wetu huru wa kufanya maamuzi ya vipawa mbele ambavyo sisi tunataka view; na uchaguzi wetu sisi binadamu misingi yake iko kwenye, furaha, mapenzi, upendo na matamanio yetu kulingana na vionyo vyetu. Tunachagua kila ambacho tunaona sisi kinatupendeza zaidi na kutupa raha zaidi kwa wakati huo husika. Kuna wale wanaojiuliza kama Mungu anajua mawazo na nini tunataka kufanya kwa nini sasa ametupa sisi huo uhuru wa kufanya tutakavyo; Anajua nini kitatokea mbele yetu katika dakika au sekunde inayokuja; sasa kwa nini ametupa huu uhuru wa kuamua?


Tafakari yetu inatukumbusha kuwa tukisoma Bibilia Mungu haoni furaha kumwona mwenye dhambi akifa katika dhambi na kuishia kupata adhabu ya milele; Tukisoma Ezekieli 33:11 Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli? Kinyume chake tunakiona tukisoma kitabu cha ufunuo 4:11 Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa. Kwa nini sasa Mungu ametupa sisi uhuru wa kuamua ili tuweze kufurahia uumbaji wake, tuwe na furaha kamili, furaha ambayo nasi ni sehemu ya kuiamua na kuiishi. Upendo ambao hauna uhuru sio upendo wa kweli; Upendo wa kweli ukupa wewe nafasi ya kufanya maamuzi. Tatizo letu ni busara ya maamuzi yetu.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa hata tukiangalia kazi ya uumbaji ambao Mungu aliufanya katika siku sita kabal ya kupumzika siku ya saba alivitazama vyote alivyofanya pamoja na uhuru aliompa binadamu wa kufanya maamuzi kuwa vyote vilikuwa ni vitu vyema. Sisi wenyewe tunatakiwa tuutumia vizuri uhuru huu kwa kuishi maisha yale yanayompendeza Mungu na kuachana na dhambi zetu. Kuishi katika dhambi sio lengo la Mungu kwetu, bali anataka sisi wenyewe tupime na kufanya maamuzi sahihi ambayo yatampendeza Mungu na sisi wenyewe. Dhambi ni zao uhuru wa maamuzi wa binadamu, zawadi ya Mungu kwetu ya kuishi maisha bila dhambi daima tumekuwa tukiidharau, matokeo yake kwetu  dhambi ndio imekuwa zao letu tulipendalo na zao ndani ya Mioyo yetu, ndio maana hata maamuzi yetu yametawaliwa na dhambi. Matokeo ya uchaguzi wetu ni kilio na kusaga meno kwani Mungu hauvumilia matumizi mabaya ya maamuzi yetu. 


Tafakari yetu leo tukumbuke kuwa Mungu anajua kila kitu kwani ni yeye ndiye aliumba vitu vyote. Na tazama vyote vilikuwa vikipendeza kama waraka wa waefeso 1:11 unavyosema na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake. Hivyo anajua mawazo yetu na nini tunatka kufanya kwani ni yeye ambaye alitupa sisi uhuru wa kuamua nini tufanye; anaona jinsi ambavyo tunafanya maamuzi yetu tukiangukia kwenye dhambi na kwa upendo wake alituletea Mkombozi wetu yesu Kristo aje kuishi nasi na kutufundisha jinsi ya kufanya maamuzi sahihi ambayo yanampendeza Mungu. Na isitoshe alikubali kupita katika njia ya Mateso na kufa msalabani ili tu tusamehewe dhambi zetu ambazo zilitokana na maamuzi mabaya. Ni wajibu wetu sasa kubadilika na kuanza sasa kufanya maamuzi ambayo yanampendeza Mungu kwa kuacha kufanya maamuzi katika njia ya dhambi.

Hii ndio tafakari yetu ya leo –Amina_


Emmanuel Turuka

Wednesday, June 29, 2016

UNAZIJUA SILAHA ANAZOTUMIA SHETANI KUTUANGAMIZA?


June 29

2 Wakoritho 2:11


Tafakari ya leo tuangalia jinsi shetani anavyotumia silaha ambazo tunazo kutuangusha sisi wenyewe; shetani anapinu nyingi sana za kutuangamiza kabisa kama hatuko makini; tukisoma 2 Wakoritho 2:11 Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake. Huu ni wajibu wetu kuzuia mbinu zote za shetani kwani tunamjua vizuri, na mikakati yake yote; silaha moja nzito sana ya shetani ni kuwa na majivuno silaha hiyo ni hatari sana katika maisha yetu kama wafuasi wa kristo; mara nyingi sisi kama binadamu hatuoni tofauti yeyote pale mambo yanapokwenda vizuri tukifurahia utajiri na amani mfano mzuri tukimwangalia Lucifer mkuu wa malaika ambaye alikuwa akiishi vizuri chini ya utawala Mungu; hatimaye tama na majidai yalimjia kupingana na Mungu. Timoteo 3:6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. 

Tukisoma Ezekieli 28: 14-17 Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto.  Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto.  Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa hatuna sababu ya kuwa na majivuno kama 1 Wakoritho: 13:8 inavyosema Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; tunatakiwa kujiepusha na huluka ya majivuno yatokanayo na kufanya mambo mazuri kama Yesu alivyokuwa akiwafundisha wafuasi wake katika Luka 18:9-14 Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote. Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang'anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.  Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa. Hatutakiwa kujihesabia haki wenyewe hata kama tunafanya mema Mungu peke yake ndiye ajuae matendo yetu na anakipimo sahihi cha kutupima na kutupa thawabu tunayostahili.

Tafakari yetu inatusisitiza kuwa lazima tuendelee kuchukua taadhari  dhidi ya adui wa roho zetu. Tukisoma 1 Petro 5:8 Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Ni ukweli ambao haupingiki kuwa unapopigana vita na unataarifa za kutosha juu ya adui yako, hukusaidia na kupunguza ugumu wa vita yako na uwezekano mkubwa sana wa ushindi; tukumbuke kuwa Mungu alikuwako tangu kuumbwa kwa dunia lakini shetani shetani hakuwako toka mwanzo wa dunia; Mungu kamwe haumbi kitu chochote kibaya; Mungu huumba vitu vyote katikaukamilifu mkuu; Adamu na Hawa waliumbwa katika ukamilifu na ubora uleule kama yeye alivyo; hata shetani alipoumbwa alikuwa katika ubora wa ukamilifu na alikuwa haitwi shetani; na alikuwa akijulikana kama Nyota ya asubuhi tukisoma

Tafakari yetu inatukumbusha anguko la Lusuferi ( Nyota ya Asubuhi) tukisoma kitabu cha Isaya 14:11-12 Fahari yako imeshushwa hata kuzimu, Na sauti ya vinanda vyako; Funza wametandazwa chini yako, Na vidudu vinakufunika.  Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa. Kabla ya kuwa Shetani alikuwa mkuu wa malaika wote, alikuwa akiwaongoza malaika katika masifu mbele ya Mungu; alijaliwa nguvu nyingi na uwezo mkubwa kutoka kwa Mungu; Lakini alianguka katika dhambi alipotaka kufanana na Mungu na kugeuka kuwa shetani. Hivyo huyu adui bado ni mbaya katika maisha yetu ya kiroho kwa sababu ananguvu nyingi bado na Mungu hakuziondoa nguvu hizo. Kwa nini lakini Mungu hakuzichukua hizo nguvu za shetani ambazo zinatutesa leo; kwa sababu Mungu hachukui zawadi ambazo anakupa wewe hata pale unaposhindwa kutimiza yale ambayo yeye anataka wewe utimize mbele yako. Je wewe ukimpa mtu zawadi pale mnapotofautiana unaichukua ile zawadi tena; kwa ujumla jibu ni hapana;

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa tujiepushe na majivuno, mwonekano wetu, nafasi ambazo tunazo kimaisha,akili zetu, uwezo wetu kifedha kwani hivyo ni baadhi tu vitu ambavyo shetani anavitumia katika vita vya kutuangusha ili tusiweze kumtumikia Mungu vile itupasavyo sisi kuishi; tunatakiwa tutumie uwezo wa kiakili tuliojaliwa katika kumtumikia Mungu na sio shetani; tunatakiwa kuwa makini na kuendelea kuzitambua silaha ambazo shetani anazitumia juu yetu katika kutuangamiza; Amka leo na uwe mshindi wa maisha ya kiroho na maisha ya baadae.

Hii ndio tafakari yetu ya leo – Amina-


Emmanuel Turuka

Tuesday, June 28, 2016

JE MAOMBI YETU TUNAYAOMBA KATIKA NJIA SAHIHI?



June 28

Yohana 16:24


Tafakri ya leo tujukumbushe umuhimu wa kufanya maombi ipasavyo ili tuweze kupata kile ambacho kweli tunakihitaji kwa wakati muafaka;  Tunatakiwa kukubali kuwa  Mungu anajibu maombi yetu lakini pengine jibu lake linakuwa hapana wakati sisi tulikuwa tumetegemea ndio; Tukumbuke kuwa hata jibu likiwa hapana ni kwa ajili ya faida yetu sisi kama binadamu ambao hatuna upeo wa kuweza kuona yale ambayo yako mbele yetu; Jukumu letu la msingi wakati tukiwa tunafanya maombi tunatakiwa tuwe  watu tuliojaa uaminivu na ukweli na tujue kuwa ambaye anatawala maombi yetu ni mmoja tu ndiye yeye ambaye ni Alpha na Omega; yeye ndio anayetufanya tuyaelewe maisha yetu; tuyakubali na mwisho ndiye anayeleta uzima. Je tunapoomba maombi yetu tunaomba katika njia sahihi na lengo sahihi; Yakobo 4:3 anatukumbusha Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu. Tukumbuke kuwa lengo kubwa sala kwanza ni kumshukuru na kumwabudu Mungu kwa wema na utukufu wake. Je tunapomwomba Mungu tunakuwa tayari tumekiri makosa yetu na kuomba msamaha?

Tafakari yetu inaendelea kutufundisha kuwa mkono wa Mungu sio mfupi katika kutuokoa au sikio lake ni bofu kusikia, tatizo ni dhambi zetu ambazo zinakuwa zinatutenganisha sisi nayeye hata asisikie shida na maombi yetu kwa wakati kwani anatusubiri sisi kwanza tujitambue kuwa tuna dhambi nasi tuweze kukiri dhambi zetu na kasha kuomba msamaha kabala ya kuomba ili tupate msadda wa shida zetu. Isaya 59: 1-2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.  Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong'ona ubaya. Ezekiel 14:3 Mwanadamu, watu hawa wametwaa vinyago vyao na kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni laiki yangu niulizwe na wao katika neno lo lote? 

Katika Tafakari yetu leo tukumbuke kuwa ni jambo la muhimu sana kudumisha uhusiano wetu mzuri wakati wote; kwa kufanya hivyo tutaweza kushinda majaribu ya Shetani ambaye anasababisha maombi yetu yasipokelewe; Laki kama tutadumisha  na kujielekeza kwa Mungu tutaweza kushinda kama Injili ya Yohana 15:7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa. Tatizo maisha yetu bado tunayaishi katika ulimwengu wa dhambi na kiburi huku tukitegemea Mungu asikilize shida zetu na kutubariki. Je Mungu anaweza kumbariki Mwenye dhambi ambaye hajitambui na hayuko tayari kujuta dhambi zake? 1 Yohana 3:21-22 Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu;  na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake.  Tukumbke kuwa hatuwezi kumzihaki Mungu Wagalatia 6:7 Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.

Zaburi ya 66:17-20  inatukumbusha kuwa Nalimwita kwa kinywa changu, Na sifa kuu zilikuwa chini ya ulimi wangu. Kama ningaliwaza maovu moyoni mwangu, Bwana asingesikia.  Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu.  Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake. Mara nyingi sana Maombi yetu hayapati kibali mbele ya macho ya Mungu kwa sababu tunadhambi ambazo zinatakiwa tuziungame na tuache kuishi katika dhambi ili sala na maombi yetu yapate kibali cha Mungu. Tukitimiza hayo Mungu anaweza jibu maombi yetu kwa kadiri na namna ambayo sisi tumemwomba; lakini jibu lake llinaweza lisije kaulingana na kalenda ya mwombaji, anaweza hata tumia njia ya kuchelewesha kidogo ili kutufundisha sisi subira,unyenyekevu na upole. Kusubiri ni fadhila moja kubwa sana katika maombi yetu.

Tafakari yetu vile vile inatukumbusha kuwa tunaye mpatanishi ambaye anatuombea kwa Baba na hivyo ni wajibu wetu kuomba kupitia yeye Mathayo 7:7-8 inavyotukimbusha Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. Ili tufanikiwe katika hili tusijenge tabia ya kumaliza ombi letu kwa kutaja tu jina Yesu mwisho wa maombi yetu; bali tunatakiwa kuishi maisha ya utakatifu ili sala zetu zipate kibali; lazima tuishi katika mapenzi ya Mungu. Jambo nyingine lakuzingatia ili maombi yetu yapate kibali cha Mungu ni kuhakikisha kuwa kwa wale wote wako kwenye ndoa wajue kuwa mahusuiano yao mazuri na utii miongoni mwao ni kibali kikubwa katika usikivu wa maombi yetu; 1 Petro 3:7 Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.

Tumalizie tafakari yetu kwa kukumbuka tujijengee tabia ya ushindi kwa kuzingatia matendo yetu mema, maisha bora yanyompendeza Mungu; Kutimiza wajibu wetu ipasavyo katika jamii tukiendelea kuamini kuwa Mungu ndiye mwenye mamlaka na ndiye mwenye mamlaka na pekee ndiye jibu la shida zetu kama Mtume Paulo 2 Wakorinto 12:8-10 aliposema Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.  Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu. Mungu anatupenda sana na daima anajibu kwa wakati wake ambao ndio wakati muafaka ambao unapita uelewa wa akili zetu.

Hii ndio tafakari yetu ya leo. Amina


Emmanuel Turuka

Monday, June 27, 2016

MNAFIKI KATIKA IMANI


June 27

Mathayo 6: 5-7

Tafakari ya leo inatukumbusha kuhusu utekelezaji wa majukumu yahusuyo imani ambayo yanampendeza Mungu. Je Mungu anapenda sadaka tunayoitolea kwake iwe ya aina gani? Je sisi tunapomwomba au kumtolea sadaka tunakuwa katika msingi wa namna gani ni ule unaopendeza Mungu au tunakuwa wanafiki mbele ya macho ya mataifa? Tukisoma bibilia tunaona kuwa Mungu anataka Moyo wa kweli, moyo thabiti ambao unajitoa kweli kwa Mungu. Mungu hataki mtu mwenye sura mbili ambazo zinatofautiana na ukweli wa Moyo wake; Mungu hajali kuhusu mwonekano wetu wa nje bali anataka mwonekano wetu wa ndani ambao unatakiwa kuwa umejaa ukweli na imani: Mungu anatazama unyenyekevu wa mioyo yetu; Mungu anatak kuona utakatifu wa mioyo yetu; na sio unafiki wa mioyo yetu. Mungu aliuona unafiki huu toka kuumbwa kwa dunia; tukifungua bibilia tunaona tatizo la unafiki liko toka katika kitabu cha Mwanzo mpaka Ufunuo wa Yohana. Kwa msingi hii Hata Mwokozi wetu Yesu alionyesha kwa vitendo unafiki ambao ulukuwako katika Nyumba za ibada; Unafiki ambao ulikuwako miongoni mwa wanasheria; hata kati ya mitume wale 12 kulikuwako na unafiki pia.

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa  tukimsoma nabiia Amos katika sura ya 5: 21-23 Mimi nazichukia sikukuu zenu, nazidharau, nami sitapendezwa na makutano yenu ya dini.  Naam, ijapokuwa mnanitolea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za unga, sitazikubali; wala sitaziangalia sadaka zenu za amani, na za wanyama walionona. Niondoleeni kelele za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu.  Lakini hukumu na itelemke kama maji, na haki kama maji makuu. Katika maneno mengine Mungu anatufundisha kuwa katika vitu vyote ambavyo nimewapa; katika vitu vyote anbavyo vimevumbuliwa; katika vitu vyote ambavyo nimeamsrisha sisi tumeshindwa kuvitekeleza ipasavyo na badala yake tumevigeuza na kuvudharau na kufanya mambo tujuavyo sisi; hata kuomba tuonavyo sisi inafaa; hivyo hata tunavyoomba tunaishia zaidi kujipamba kwa nje na sio kwa ndani; huu ndio unafiki ambao Yesu aliukataa.

Tunavyoendela na tafakari yetu hebu tuangalie Ole ambazo Mathayo alizitoa katika sura ya 23:13-24 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.  [Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnakula nyumba za wajane, na kwa unafiki mnasali sala ndefu; kwa hiyo mtapata hukumu iliyo kubwa zaidi.]  Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnazunguka katika bahari na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja kuwa mwongofu; na akiisha kufanyika, mnamfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.  Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga.  Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.  Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang'anyi na kutokuwa na kiasi. Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi.  Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote. Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi.  Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki, Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? 

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa  mnafiki hujifanya kuwa ni mwenye haki kwa mwonekano wa nje; lakini kwa mwonekano wa ndani sinyo alivyo; maisha yake yamejaa uwongo na mara nyingi ikiwa mwongo mwonekano wako wan je unakuwa na tofauti na mwonekano wa ndani; hivyo mtu wa namna hiyo anakuwa sio mwaminifu; sio mkweli; mpenda kujisifu hata kwa vitu ambavyo hawezi kutimiza; anataka kupata kibali kutoka kwa watu wanaomzunguka na kupendwa. Je wewe unatabia hiyo? Bwana wetu yesu Kristo alitutaanzarisha kuwa tukisoma Mathayo 6: 1-4 Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni. Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu. Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;  sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi. Hii ni taathari ambayo Bwana wetu Yesu aliitoa kwetu ili kuwa wakamilifu wa kweli;

Tafakri ya leo inatukumbusha kuwa lazima tujitambue kuwa sisi ni wenye dhambi na tumemkosea Mungu Ukisoma warumi 3:23 Ukisoma Mithali 20:9. Tunatakiwa kuelewa kuwa Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu Warumi 5:8 na lazima tuwe tayari kupokea matokeo ya dhambi zetu Warumi 6:23 na Yatupasa kuomba msamaha wa dhambi zetu Matendo ya Mitume 20:21/ 3:19. Tusipokuwa wanafiki ni rahisi kujenga imani yetu ya kweli juu ya Mungu. Huu ni wajibu wetu wa msingi na tunapaswa kuutekeleza bila shuruti;

Hii ndio tafakari yetu ya leo – Amina

Emmanuel Turuka


Saturday, June 25, 2016

ASANTE MUNGU

June 25

Tafakari yetu inatuhimiza kuwa moja ya wajibu wetu ni kusema asante kwa wema wako ambao unatupa sisi mwelekeo wa maisha yeu na baraka ya kila jambo ambalo liko mbele yetu; basi ni wajibu wetu kusema asante kwa kila jambo.

Wednesday, June 22, 2016

UNAFIKIRI UMEJIFICHA?


June 22

Mwanzo 3:8


Yeramiha 23:24

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa  mara nyingi kuwa tunafikiri tunaweza kujificha mbele ya uso wa bwana lakini ukweli ni kuwa  mwanadamu hawezi kujificha mbele ya uso wa Mungu  bali tunaweza kufichwa ndani ya Utukufu wa Mungu. Bahati mbaya mawazo yetu yanatudanganya na kujiona kuwa tunaweza kujificha na kufanya chochote tutakacho bila kuonekana mbele ya Macho ya Mungu. Pengine hilo linawezekana kujificha mbele ya macho ya binadamu. Tumekuwa na tabia za kuacha njia zipasazo kufuatwa na  kwenda kinyume na utaratibu tuliokubali kuufuata tukiamini kuwa hakuna anayeweza kuona au kugundua. Lakini tukumbuke kuwa hakuna  kwa namna yeyote ile tunaweza kujificha mbele ya uso wake; tuwe kwenye ngiza; ndani ya chumba; tumejificha kwenye kichaka kwa ujumla hakuna jambo litakalo tendeka ambalo Mwenyezi Mungu asiweze ona. Chochote unachoangalia; kusoma; uanchoamua kuangalia; unachofikiria; mahali popote mabapo unakwenda Mungu anajua kwa nini uko mahali hapo na kwa sababu gani kamwe huwezi jificha mbele ya uso wake;

Tafakari yetu inatukumbusha jinsi Yeramiha 23:24 Je, mtu ye yote aweza kujificha mahali pa siri, nisimwone? Asema Bwana. Je! Mbingu na nchi hazikujawa nami? Asema Bwana. Yeramiha 49:10 Lakini nimemwacha Esau hana kitu, nimepafunua mahali pake pa siri, wala hataweza kujificha; kizazi chake kimeangamizwa, na ndugu zake, na jirani zake, naye mwenyewe hayuko. Ezekieli 28:3 Tazama, una hekima kuliko Danieli; hapana neno la siri watu wawezalo kukuficha; ufunuo 6:15-17 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya ilima,  wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.  Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?

Tafakari yetu leo hebu tujikumbushe nini kiliwatokea Adamu na Hawa tukisoma Mwanzo 3:8-10 Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu asiwaone.  Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi? Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha. Adamu na Hawa baada ya kutenda dhambi waliamua kujificha wakitambua kuwa Mungu hataweza waona na hivyo kuwa mbali kabisa na uso wa bwana; kumbe haikuwa hivyo ndivyo yalivyo maisha yetu; akili zetu zinajaa ukungu na kufikiri kuwa tunaweza kufanya dhambi yoyote na Haitaonekana mbele ya Mungu; Sababu kubwa ya kujificha ni kwa sababu tunakuwa tumefanya dhambi mbele ya Mungu;

Tafakari yetu bado inatukumbusha kuwa dhambi na tendo la kujificha hatuwezi kuvitenganisha na hilo ndilo anguko la mwanadamu; lakini pamoja nahii tabia ambayo inasababisha anguko la mwanadamu Mungu daima bado anataka kuturudisha katika njia iliyo bora kabisa; njia ya ukamilifu mkubwa tukisoma Luka 19: 1-5 anasema hivi, Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake. Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri. Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo. Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile. Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.  Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watozaushuru, naye ni tajiri.  Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.  Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.  Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako. Mungu yuko tayari kutushirikisha sisi katika ufalme wake, kama tutaacha tabia ya kujificha pamoja na dhambi zetu, tukiwa kama Zakayo tutapata wokovu wa kweli;

Tafakari yetu inatuonyesha kuwa Zakayo alijitambua kwa alikuwa Ni Mtu mwenye dhambi na ambaye alikuwa akichukiwa na watu kutokana na kazi yake. Hivyo baada ya kujificha yeye aliamua kumtafuta Yesu amwone ni  mtu wa aina gani. Alijua kuwa kwa habari juu ya Yesu alijua kuwa atakuwa amekutana na mtu mbaye ataweza msamehe dhambi zake na yeye kuanza kuishi maisha mapya ya wokovu. Hatutakiwi kujificha tunapokosea bali tumkimbilie mwokozi wetu Yesu kristo ili aweze kutusamehe na kutuondolea aibu ambayo inatupelekea sisi kujificha.

Tukumbuke kuwa hakuna yeyote ambaye anaweza kujificha kukimbia uwembo wa Mungu na uwepo wa Bwana wetu Yesu Kristo juu ya Matendo yetu; Tunatakiwa kubadilika kwa tuweze sasa kuwa wakamilifu kwa kuacha dhambi na kuishi maisha mema yanayompendeza mungu.

Hii ndio tafakari yetu ya leo – Amina


Emmanuel Turuka

Tuesday, June 21, 2016

JE YATUPASA KUISHI KWA MASHAKA?



June 21

Matthew 11:2-3

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa kama nina amini na kwa nina wasiwasi? Tukiangalia katika mazingira tofauti tofauti simulizi katika vitabu vya  Ayubu, Mhubiri, maombolezo, zaburi na Habakuki vyote katia mazingira tofatuti vimegusia dhana ya mashaka kwa hisia kuwa Mungu alikuwa amewaacha katika shida zao; Katika mazingira ya maisha ya kuwa Mfuasi wa Kristo ni wazi kuwa dhana ya kuwa na mashaka ni jambo la kawaida; tukumbuke kuwa hata imani ili iweze kuimarika yatupasa kuwa mashaka ili kukomaza imani hiyo; kama wataalamu wengi walivyopata ongea kuwa kama utakuwa na wasiwasi basi utakuwa umefika katika mahali ambapo pa mwisho kabisa katika imani na mahali hapo ni mbinguni.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa mashaka /wasiwasi tunaweza vielezea katika makundi makuu matatu; kuna wasiwasi ambayo inaletwa na wasomi ambao wao mashaka yao wanayaelekeza nje ya imani yetu, wakiuliza Mungu kweli yuko? Je bibilia ni neno la Mungu? Kweli yesu ni mwana wa Mungu? Ni kweli kuwa Yesu alifufuka? Kundi la pili la wenye mashaka ni wale ambao ni washiriki katika makanisa yetu; ambao wanajiuliza kama kweli wao ni wakristo kweli? Je kweli wananamini? Kwa nini bado najisikia mdhambi? Kwa nini inachukua muda mrefu kwangu kufanikiwa kupona, au shida yangu kutatuliwa. Na kundi la tatu wale ambao mashaka yao yanalengwa na swali kwa nini? Kwa nini mototo wangu alikufa? Kwa nini ndoa yangu imevunyika? Kwa nini sipati Mume? Kwa nini marafiki zangu wananisaliti; Mungu alikuwa wapi wakati Mjomba wangu aliponibaka? Haya ni maswali machache kati ya mengi; tunachokiona hapa ni mwingiliana wa imani na maumivu ambayo yanapatikana katika maisha na kuleta mashaka na tatizo ni pale sasa majibu hayapatikani hata wale wahusika ambao wako ndani ya kanisa ambao walitakiwa kusaidia kuondoa mashaka haya nao wanamua kudharau na kuto kutoa msada wa ufafanuzi mzuri ambao unamjenga mtu kiimani zaidi na kuweza kuondoa mashaka ya namna hii. Kwa kushindwa kuyapatia ufumbuzi maswali kama haya ndio mashaka ya kiimani au mashaka ya kiroho huanza kujitokeza na watu wananza kukimbia kanisa.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa watu wengi wanafikiri kuwa kuwa na mashaka ni kukosa imani; lakini kwa ujumla wake sio kweli isipokuwa kama wewe huamini hivyo huna imani; kwa asiye amini ni tendo la makusudi na lililo kusudiwa; lakini kuwa na mashaka ni  kuwa na mashaka ya ndani ya nafsi yako; mshaka yanasemehewa na mungu hatuazibu sisi tunapo jiuliza maswali mengi kuhusu yeye; tuwakumbuke Ayubu na Daudi mara kadhaa walikuwa wanajiuliza maswali mengi kuhusu Mungu lakini hata hawakuwalaani; Uwezo wa mungu ni wa ajabu kutatua mashaka yetu na maswali yote yenye mashaka juu yake; watu wengi wanafikiri jinsi tunavyo jiuliza maswali mengi kuhusu Mungu kwamba hatuna imani la hasha tukumbuke kuwa bila kuwa na mashaka imani yetu haitakuwa inavyotakiwa.

Tafakari yetu inaendelea kufafanua kuhusu mashaka kwa kuangalia mfano kutoka Mathayo 11:2-3 Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza,  Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine? Hili ni swali lenye nguvu sana; cha kujiuliza hapa masha ya Yohana Mbatizaji yanatokea wapi; kumbuku kuwa yeye wenyewe huko nyuma alishakiri kumjua Kristo kama masiha; ukisoma Yohana 1: Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi. Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake.  Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!  Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.  Wala mimi sikumjua; lakini kusudi adhihirishwe kwa Israeli ndiyo maana mimi nalikuja nikibatiza kwa maji....  Nami nimeona, tena nimeshuhudia ya kuwa huyu ni Mwana wa Mungu.

Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!  Kwa maelezo haya toka injili ya Yohana: Yohana Mbatizaji alikuwa anamjua Yesu kuwa ni nani; lakini swali la kujiuliza ni hili kwa nini mtu ambaye alimfahamu sana Yesu aliishika kuwa na Mashaka na mafundisho yake? Lakini tukumbuke kuwa watu wenye mashaka ndio wanaokuwa watu wenye imani kubwa sana.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa Mungu yuko tayari  kutatua mashaka yote; kuondoa woga; na kukujibu maswali yote ambayo unafikiria kuwa hayana majibu; anatawala mbingu na dunia bila msaada; tujue kuwa mashaka yetu kamwe hayamletei hasiara yeyote; yeye ni Mungu wetu sote katika khali yeyote ile; tunachopaswa kufanya ni kuishi na kutekeleza majukumu yetu kwa Imani tumkumbuke Noha alipokuwa akijenga safina alitenda kwa Imani; Abrahamu alipo acha ur na kwenda Chaldees alifanya kwa imani bila mashaka; Abrahamu alipotakiwa kumtolea sadaka Isaki alifanya kwa Imani bila mashaka; tunakumbuka Kisa cha Musa na  alipotembea na wana wa Israeli katika ya Bahari ya shamu kwa imani na sio mashaka; mwangalie samweli alipotupwa katikati ya samba alikuwa na imani zaidi na sio mashaka. Hivyo pamoja na mashaka yetu bali tunatakiwa kutanguliza imani zaidi na kutenda kwa imani na sio mashaka;

Hii ndio tafakari yetu ya leo – Amina-


Emmanuel Turuka

Monday, June 20, 2016

MUWE WAMOJA KAMA SISI TULIVYO:


June 20

Yohana 17: 1-5

Tafakari yetu ya leo inatukumbusha ombi ambalo Yesu, aliwaombea mitume wake wawe na umoja kama wao walivyo katika ufalme wa mbinguni. Yesu aliwakumbusha mitume wake bila kujali khali zao, wametoka wapi; wana nini wanapaswa kuwa wamoja. Tafakari yetu inatukumbusha kuwa watu wa mungu  wametoka kutoka makabila yote; lugha zote;mataifa yote;katika khali tofauti za uchumi. Ndio maana Yesu aliwaombea wafuasi wake wawe na Umoja kama wao walivyo. Tunatoka katika mazingira tofauti lakini wote ni zao lake yeye; tunajitenga na kuchukiana kwa sababu za tofauti zetu na mazingira ambayo tunajijengea miongoni mwetu; mungu anataka sisi kushirikiana pamoja kwa upendo wote;

Tafakri yetu leo inatumumbusha kuwa tunatakiwa kufikiria katika akili zetu kuwa  mimi ndio natakiwa kuwa sababu ya umoja wetu; natakiwa nititoe kwako, niwe nawe na nishiriki nawe katika yale yote ambayo yameelezwa katika  amri ile kuu ya upendo; kuwa Mkristo wa kweli na sio wa kuhudhuria katika makanisa ni kuishi amri hii ya upendo kwa vitendo; na tukiishi kwa vitendo ndipo tutatekeleza maana ya kuwa Mfuasi wa kristo; tukumbuke kuwa zawadi zote ambazo Mungu ametupa sisi, zawadi za Muda, zawadi ya Nguvu, afya njema Mungu ametujalia sisi lakini anataka zawadi hizi tuzitumie kwa manufaa ya wengine pia; heshima ambayo sisi tunatamani kuwa nayo ndio iwe hsehima hiyo hiyo ambayo tunapaswa tuionyeshe na kwa wengine; tunapaswa kushauriana; inatupasa kutiana moyo; yatupasa kushirikiana kwa Yesu alivyotenda kwetu; Yesu daima anataka sisi tuwe chumvi ambayo inaleta radha nzuri katika chakula. Wafilipi 2:2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, nia moja. 

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa Jamii yetu leo kuwa ukweli sio kitu ambacho kinapewa thamani ya kweli; Mungu katika mafundisho yake ukweli mmeweka kuwa msingi wa kila kitu; tukiangalia zaburi ya 51:6 Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni; Nawe utanijulisha hekima kwa siri, au Zaburi ya 86:11 Ee Bwana, unifundishe njia yako; Nitakwenda katika kweli yako; Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako; Wafilipi Ufunuo 21: 27 Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.

Yesu alituombea tuwe na umoja akijua kuwa palipo na umoja ukweli hutawala na amani itadumu, na palipo na ukweli na umoja unyenyekevu utatawala uwazi wa mambo ya msingi yahusuyo amani yatafanyika, na mashauriano mema yatafanyika kwa upendo mkubwa; ndio maana yesu alitaka tuwe wamoja tukiwa wamoja tutashirikiana kwa ukaribu zaidi. Tutapendana na hata pale ambapo hatutakubaliana tutamaliza tofauti zetu kwa upendo na hekima ya kweli. Yesu anatufundisha kuwa Maisha ya Mkristo ni mchanganyiko wa vitu viwili yaani machungu na furaha; katika machungu maisha yanakuwa yamegubikwa na mambo mengi ambayo yamejaa masikitiko, taabu na mateso kwa baadhi ya yetu na wengine wakifurahi maisha yalijaa furaha na starehe. Tukisoma Warumi 8:28 inatukumbusha kuwa Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Hivyo sisi sote pamoja na taabu zetu na furaha zetu Mungu ametuita tuwe pamoja naye, Ndio maana yesu alituombea tuwe wa moja katika umoja wetu tutaweza kusaidiana katika kyakabili maisha katika khali yeyote ile;

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa katika umoja wetu hakuna magumu. Bali neema ya Mungu ndio silaha ya kweli katika kupambana na majaribu yeyote yale. 2 Wakorinto 12:9-10  inatukumbusha kuwa Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu. Pasipo na umoja ni karibisho la udhaifu; bali tukiishia katiaka umoja tunajenga nguvu ya ushindi. Ombi la Yesu aliloomba juu wa wafuasi wake lilikuwa la maana na msingi mkubwa akitambua kuwa mitume wake walikuwa ni watu wenye uwakilishi tofauti, utu tofuti na walikuwa wamekulia katika mazingira Tofauti, walikuwa wengine ni wapole, waaminifu, wengine ambao walikuwa tayari kwa shari; hivyo ombi lake juu yetu likuwa ni msingi mkubwa;

Yohana 17; 20-26 inavyotukumbusha Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli.  Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakao niamini kwa sababu ya neno lao.  Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.  Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.  Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.  Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.  Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma.  Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao. Umoja ni silaha muhimu sana katika imani yetu.

Hii ndio tafakari yetu ya leo Amina

Emmanuel Turuka


Sunday, June 19, 2016

ASANTE BABA KWA UPENDO WAKO MKUU


June 19


Ezekieli: 22:30

Tafakari yetu ya leo inalenga katika kushukuru kwa baraka ya Baba kama Mzazi kiongozi; Mtazamo sahihi mbele ya Mungu:  Zaburi ya 111:10 kumcha Bwana ndio mwanzo wa hekima, wote wafanyao hayo wana akili njema, sifa zake zakaa milele. Tukisoma Marko 12:30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwan nguvu zako zote. Yohana 14:15 mkinipenda, mtazanishika amri zangu. Yakobo 4:7 Basi mtiini Mungu. Mpigeni Shetani, naye atawakimbia. Mtazamo wetu lazima heshima, utii, upendo, uaminifu, unyenyekevu, utii, worshipful, na sala.

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa kuiangalia upya tena wajibu wa Baba katika familia hasa katika malezi na makuzi ya Taifa ambalo tugemeo letu ni vijana ambao lazima watokane na malezi Bora ya familia ambayo ndio msingi wa familia bora. Tukisoma kitabu cha Ezekieli 22:30 kinatukumbusha kuwa Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu. Mungu anaonyesha Kiongozi bora wa familia na jamii anayemtaka ambaye atasimama kati yake na nchi; je wewe leo kama baba wa familia uko tayari kuchukua haya majukumu?
Tafakari yetu inatuonyesha kuwa  baba hodari; Baba mwema; baba anayekubalika mbele ya Mungu, lazima awe tayari kuyabeba majukumu kama baba; anatekeleza wajibu wake kama baba; anafikiri kama baba; anatenda kama baba; aliyejaa upendo na msamaha;  akitekeleza haya yote anapata sifa ambazo Mungu ameziweka kwa Kiongozi wa familia; lakini bibilia inatukumbusha kuwa Baba hodari lazima awe ni mtu mzuri, na mtu mzuri ni Yule ambaye anafuata mafundisho na maandiko ya bibilia na kuweza kuwalea watoto katika misingi mizuri ya kiimani. Kama Mithali 3:5 inavyotukumbusha  kuwa jukumu kubwa la Baba liwe; Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Katika njia zake zote tunawajibu kama Baba kukiri na kuomba mwongozo katika malezi ya watoto wetu, tukumbuke kuwa hakuna kisichowezekana mbele ya Mungu wajibu wetu ni kusimamia imani yetu.

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa sisi kama baba wa familia tujue kuwa kwa imani tumekombolewa, na imani ili iweze kuwa dhabiti utiifu ni lazima; Kama baba tunatakiwa kuonyesha mfano mzuri ndani ya familia na kwa kufanya hivyo hata malezi ya vijana wetu yatakuwa rahisi sana Waefeso 2:8-9. Sisi kama wanaume (Baba) tuna tabia ambayo tunataka daima kuwa juu na kutoa maamuzi na wengine wote wayafuate hata bila kukaribisha  ushiriki wa mawazo mengine toka ndani ya familia. Tunatakiwa tujifunze kutoka kwa Mama zetu ambao kwa maumbile yao na busara zao ni rahisi sana kujikabidhi kwa kila wananchokifanya katika mikono ya Mungu. Yesu kwa kutambua ubabe wa sisi wanaume ndipo aliposema Mathayo 18:3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. Watoto na wanawake wana tabia ya kuamini na kutegemeana.
Tafakari yetu leo inaendelea kutukumbusha kuwa kwa wanaume kama watatekeleza majukumu yao kwa utaratibu ambao unatakiwa Mungu atakeleza haya kwetu: tukisoma Isaya 40:30-31 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;  bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia. Hiyo ni ahadi ya Mungu kwetu kama tunasima kwenye mstari sahihi; wakati waraka wa Paulo kwa Wafilipi 4:19 unatukumbusha kuwa ya Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu. Wagalatia 5:16-18 inatukumbusha kuwa Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.  Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria. 


 Tafakari yetu inatukumbusha kuwa jukumu la baba ni kuleta matumaini ndani ya familia; Kuleta upendo; amani ; umoja; heshima; uwajibikaji wa kila mtu ndani ya familia; bibilia inatukumbusha kupitia Wakolosai 3:21 kuwa Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tama. Huu ni ujumbe mzuri sana ambao tunatakiwa kuuzingatia ili kuleta matumaini ndani ya familia yetu na umoja wa familia.  Ujumbe huu kutoka Wakolosai 3: 15-20 ni muhimu sana katika siku hii ya leo Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani. Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu. Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.  Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.  Ninyi waume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao. Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana. Ni ujumbe ambao umetoa mwongozo mzuri sana katika kusherekea siku hii ya leo ya Kumbukumbu ya Akina baba



Hii ndio tafakari yetu ya leo Amina


Emmanuel Turuka

Saturday, June 18, 2016

NAWATUMA - MKIKARIBISHWA INGIENI

June 18


Tafakari ya leo tujikumbushe jinsi Yesu alipowatuma wale sabini na wawili na kuwaagiza kuwa Mathayo 10:8-23  Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.  

Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.  Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.  

Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;  wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake.  Na mji wo wote au kijiji cho chote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; mkae kwake hata mtakapotoka.  

Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni.  Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.  Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung'uteni mavumbi ya miguuni mwenu.  

Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule.  Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.  

Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;  nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.  Lakini hapo watakapowapeleka, 

msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.  Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.  Na ndugu atamsaliti nduguye ili auawe, na baba atamsaliti mwana, na wana watawainukia wazazi wao, na kuwafisha. 

 Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.  Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia, Hamtaimaliza miji ya Israeli, hata ajapo Mwana wa Adamu.