WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Tuesday, March 29, 2016

ASIYE FANYA KAZI NA ASILE


2 Thess. 3:10

March 28

Tafakari ya leo tunaangalia maagizo ya Mtume Paulo alipokuwa akiwafundisha watu wa Tesolonike kuhuhusu umuhimu wa kufanya kazi kwa neema ya Mungu na kwa afya zao kama binadamu ambao bado wana mahitaji yao binafsi. Tunafahamu katika baadhi ya nchi mafundisho haya bibilia hayafuatwi sana kwani kuna watu ambao kwa makusudi kabisa hawataki kufanya kazi; na watu hao wanaafya njema, wana akili za kutosha na wanasababu zote za msingi za kufanya kazi bali hawataki kufanya kazi nab ado serikali zao zinawahudumia katika kuwasaidia kuwalisha. Lakini Mtume Paulo alitaadharisha hili mapema sana ili kuondosha tabia ya uvivu miongoni mwa wanajamii ambayo inaweza kupelekea au jumuia kuwa mtumwa katika jamii husika. Maonyo hayo yalitokana na uzushi wa dini za uongo,  waliokuwa wakitaka kuishi wakitegemea ndugu zao kaka na dada bila kufanya lolote

Tafakari ya leo inatusisitiza kuwa kama una afya njema huna sababu ya kutegemea msaada kutoka kwa watu wengine; Mwenye afya njema anatakiwa asiwe mzigo kwa watu wengine; asiwe tegemezi. Asiwe chanzo cha mtu mwingine kupata dhambi ya masononeko au hasira katika kumsukuma mtu huyo kufanya kazi; tunafahamu kuwa familia bora itakuwa vyema kama inaweza kujitegemea vizuri; Kwa msingi kuwa kazi ni muhimu katika kutunza familia na katika kuwakuza watoto. Inapendeza kuona kuwa tunaishi kwenye jamii zetu bila  kutegemea wengine, na tunatakiwa kuzingatia mafundisho ya Bibilia kuwa familia ndio msingi mkubwa wa kazi ; Mafano mzuri tunaupata kutoka familia takatifu  ya Nazaret inaonesha jinsi familia ya Yesu ilikuwa ya wafanyakazi, maana Yesu mwenyewe aliitwa mtoto wa seremala na hata kuitwa yeye  mselemala.

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa  kufanya kazi kunaleta tija na heshima ya utu na  kutambua  kuwa umeumbwa kwa mfano wa Mungu, Hivyo tukumbuke kuwa utafutaji wa ajira ni jukumu kubwa la binadamu ili kujikuza mwenyewe familia yake na jamii nzima na katika kutimiza wajibu wetu kama ilivyoelezwa katika bibilia. Tatizo ambalo binadamu wengi linatukabili ni tumezoea mno kutafutiwa kulalamika kuhusu ugumu wa maisha; hilo ni tatizo ambalo pia tunalipeleka kwa watoto wetu tunawakuza kwenye huo mfumo wa kulalamika kila siku! Hivyo hatuwezi kufikia ndoto  ya malengo ya mafanikio kwa  kushindwa kufanya kazi

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa mafanikio yoyote yanahitaji bidii kama maandiko yanavyosema kuwa asiye fanya kazi na asile, 2 wathesalonike 3:10. Maandiko msingi wake uko kwenye mafanikio ambayo yanatokana na kazi; sote tunatakiwa kufanya kazi kwa bidii ili tufikie malengo tuliyojiwekea ndipo mafanikio yataweza kutokea; Tunatakiwa tumtangulize Mungu mbele ili malengo yetu ya kufanya kazi kwa bidii yaendelee kupata kibali toka kwa Mungu ili Mungu awe anatembea na nasi kwa kila jambo na malengo yetu yaweze kutimia; inatupasa kutenda vile alivyoagiza  naye atakusaidia katika kutupa nguvu ya kutimiza malengo yetu kwani tunajua kuwa  Mungu hamtupi mja wake.

Tafakari yetu inaendelea kutukumbusha kuwa tuwapo kazini sio tu nguvu itumike bali pia akili na kauli zetu ziwe zimejaa hekima itokayo kwa Mungu . Tukiwa  kazini ni rahisi watu kutamani kuwa na wewe muda wote kwani kinywa chako huneno yaliyo mema wakati wote. Ukisoma 1Petro 3:10 utaona jinsi Mungu anavyotuagiza kutumia mdomo au kauli zetu katika kutangaza yaliyo mema kwa kulitangaza neno lake “Kwa maana,atakaye kupenda maisha na kuona siku njema,azuie ulimi wake usinene mabaya na midomo yake isiseme hila”. Epuka kula na kunywa kupita kiasi, katika mchakato wa kutafuta maendeleo kula na kunywa kupita kiasi kunasababisha kurudisha nyuma maendeleo yako kwani unakuwa unatumia pesa bila sababu za msingi. Mithali 23:21 “ Kwa maana mlevi na mlafi huingia umasikini na utepetevu humvika mtu nguo mbovu,” neno la mungu pia linatuasa kula na kunywa kwa kiasi kwani mlevi na mlafi huishia kwenye umasikini daima mpaka kukosa hata vazi zuri la kuvaa. Chagua marafiki wenye hekima, kwani marafiki nao wana nafasi kubwa katika kutafuta maendeleo yako. Marafiki mwenye hekima watakupa njia mbalimbali za kupata maendeleo. Tukisoma kiatabu cha Matendo 20:35. . “Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu jinsi alivyosema mwenyewe, ni heri kutoa kuliko kupokea,”

Tafakari yetu bado inasisitiza kuwa mafanikio ya kitu chochote yakupasa kutenda yampendezayo Mungu ili kuwe na mwisho mzuri tofauti na kutaka mafanikio ya haraka na kuwa na mwisho mbaya. Hivyo Mungu hapendi watu wavivu. Watu ambao hawajishughulishi; lakini anatak watu ambao wanajishughulisha kwa kazi ambazo ni halali na zinazompendeza yeye; Hivyo ni wajibu wetu kufanya kazi kwa bidii huku tukiomba mwongozo na hekima zetu kwa ajili ya ustawi wetu wenyewe na wa wote wanaotuzunguka.
Hii ndio tafakari yetu ya leo; Amina

Emmanuel Turuka



No comments:

Post a Comment