WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Wednesday, March 23, 2016

MSAADA WANGU UTATOKA WAPI?



March 23

Zaburi 121

Tafakari yetu ya leo tusome na kusali pamoja Zaburi hii ya 121 ambayo ni mwongozo mzuri sana katika ulinzi, na mafanikio ya maisha yetu. Kwa zaburi hii Mungu anatenda kazi ya upendo wake kwetu kupitia ulinzi wake katika maisha yetu ya Kila siku. Mungu atabaki kuwa Mungu wakati wote. Tuna kila sababu ya kufurahi na kuringa kama wakristo.

1  Nitayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi?

2  Msaada wangu u katika Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.

3  Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye;

4  Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5  Bwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.

6  Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.

7  Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.

8  Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

Hii ndio Tafakari yetu ya leo tunavyoendela kumshukuru Mungu katika Juma hili takatifu tukisubiri sherehe ya Bwana- PASAKA   - Amina.

 Emmanuel Turuka





No comments:

Post a Comment