WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, March 25, 2016

BABA YAMETIMIA; MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU.



John 19:28-30

Leo ni Ijumaa kuu ni siku muhimu sana katika ukombozi wetu; ni siku muhimu sana katika safari ya usindi wa ukombozi wa maisha yetu kama wakristo ambao tegemeo la ukombozi wetu liko mikononi mwa Bwana wetu yesu kristo; ni siku ambayo Yesu alisulubiwa msalabani kwa dhambi zetu. Ni siku ambayo maadui wake walijua kuwa tayari wameshinda vita ya kumwangamiza baada ya kumtesa na kumdhihaki katika kipindi chote cha mateso na kumsulubisha pale msalabani;

Tafakari yetu leo inatuhamasisha kuwa maadui wa Yesu mafarisayo na wakuu wa sheria walijua wameshinda na wamemwangamiza Yesu kwa kifo cha Msalabani; wakati huo huo wanafunzi wa yesu walikuwa na machungu wasijue nini cha kufanya na walikuwa wamejificha na hawataki kuonekana hadharani; Lakini Yesu baada ya kusulubiwa msalabani na maandiko kutimia aliinua macho mbinguni na kusema yametimia; Ni neno muhimu kwa sababu kunaashiria mwisho mafanikio ya hatua muhimu katika ukombozi wetu. Ni neno hili Yametimia hutumika wakati wa ukamilifu ulio sahihi wa jambo fulani muhimu. Yesu alilitumia neno hili kwa kumaliza kazi ngumu ambayo bwana wake waliompa kufanya , alikuwa akisema kwa bwana - tetelestai - "Mimi kuondokana na matatizo yote ; Nimefanya kazi kwa kadri ya uwezo wangu na nimelaiza salama kwa mafanikio makubwa ya ukombozi wa binadamu. Naamini kuwa hakuna neno nyingine  bora linaloweza kutuonyesha ukuu wa Yesu. 

Tetelestai maana ya kumaliza, yametimia. Ni mara zote neno hili tunalitumia kama furaha na ushindi; Hapa tunasherekea ushindi wa kuishinda dhambi iliyoingia ulimwenguni kupitia Adamu na Hawa na hitimisho lake ni siku hii ya Leo ya Ijumaa kuu.

Tafakari ya leo inaonyesha kuwa Mungu ni mwenye haki; Yeye pia ni huruma ; Mungu ametoa njia ambayo tumekombolewa kwa damu mbadala ya mwokozi wetu Bwana wetu Yesu Kristo. Mwenyezi Mungu ametupenda ametuamini sisi wana wake kwa kumtoa Yesu kuwa ndio daraja letu la ukombozi: warumi 3: 24-26 wamehesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake ili aonyeshe haki yake, kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa Mungu dhambi zote zilizotangulia kufanywa; apate kuonyesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye Yesu.

Tafakari yetu leo inatuonyesha jinsi  Mungu alivyotimiza ahadi ya kufanya malipo halisi ; Kwa kumtoa Yesu mbele kama malipo ya dhambi zetu.Yesu amekuwa Kipatanisho chetu na Mungu  kupitia damu yake Takatifu; damu pekee ambayo inaweza kweli kulipia dhambi zetu. Hii ilikuwa ni kuonyesha haki ya Mungu , kwani kwa uvumilivu wake wa Uungu amesafisha dhambi zote  zilizofanywa Kwa kipindi cha muda kirefu toka kuumbwa kwa dunia , kwa sababu Mungu si mwepesi wa hasira na mikopo yake iliyojaa huruma iko juu yetu siku zote; hivyo aliamua kutoa Yesu ambaye alizaliwa kama binadamu awe malipo ya kweli kwa ajili ya dhambi zetu , hii ilikuwa kuonyeshaupendo wake kwetu.

Tafakari yetu tunamshukuru Yesu kwa Kilio chake cha ushindi Yametimia; Kwetu Yesu kufa msalabani ni tendo la ushindi mkubwa sana, kwani alishatueleza kuwa Mwana wa Adamu atapata mateso makali na kufa msalabani kisha aatafufuka kutoka kaburini na hiyo inadhihirisha  uishinda dhambi na mauti. Na tukumbuke kuwa sisi ambao tunaamini kuwa Kwa kusulubiwa kwake Krsito tumepata ushindi mkubwa sana ambao wanaamini, Kristo aliyesulubiwa ni neno la wokovu, ni neno la ushindi. Na maneno ambayo Yeye anaongea hapa ni kelele za ushindi. Kwa macho haya si ushindi kelele. Lakini kwa macho ya imani na tukiendela kushukuru kwani kristo anaishi ndani yetu; hivyo mpango wa Mungu na madhumuni ya maisha yangu sasa yametimia. Njia ya uvumilivu, unyenyekevu kusamehe na kuto shindwa hata katika magumu ndio njia ambayo Mungu anataka sisi kuishi nasi mwisho wa safari hii tuweze kusema kama Yesu alivyosema Msalabani YAMETIMIA;

Leo ni siku Muhimu sana katka maisha yetu kama Mkristo, askari shupavu wa Yesu; hivyo Mungu anataka wewe kukamilisha na kuishi maisha yetu kama kristo alivyoishi duniani; kupigana vita vizuri, na tuweze kumemaliza mbio za kumtafuta Mungu kwa ushindi na kuvikwa taji katika makao ya milele; Kwa ushindi wa Yesu tumeondolewa dhambi zote na tumelipwa kwa ukamilifu;

Hii ndi tafakari yetu ya leo katika Ijumaa hii Kuu ambayo ni muhimu sana katika ukombozi wetu kama Wakristo – Amen


Emmanuel Turuka

No comments:

Post a Comment