WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, March 4, 2016

NAJINYENYEKEZA CHINI YA MKONO WA MUNGU



March 4

1 PETRO 5: 6

Tafakari ya leo tunaangalia mkono wa Mungu na kazi yake kwetu; Mkono wa Mungu unaleta unyenyekevu kwetu; Mungu anatumia namna mbali mbali za kutuletea na kutuonyesha sisi unyenyekevu wake; kuna wakati anawatumia watu wengine katika kutuletea unyenyekevu ambao Mungu anataka sisi tuwe nao. Wakati mwingine anatuletea maafa katika maisha yetu na mali zetu hata pale tunapopoteza wapendwa wetu lakini lengo lake ni kutufundisha jinsi gani tunaweza kuwa wanyenyekevu mbele yake na mbele ya watu wengine. Kama tunavyosoma kutoka kwa Waroma 8: 28 Nasi twajua kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi  pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani wale walioitwa kwa kusudi lake.

Tafakari ya leo inatumbusha kuwa kuishi kwa enyenyekevu sio jambo rahisi, ni kuwa tayari kukubali kuwa Mungu ndiye mwenye mamlaka na maisha yako, yeye ndiye ayaendeshae maisha yako. Jambo ambalo mara nyingi hatutaki kukubali au kulifuata. Sisi tunataka tuishi maisha ya kujitawala wenyewe na kufanya mambo yetu vile ambavyo tunataka iwe. Unyenyekevu unatukumbusha kuwa tunakuwa tayari kukubali kuwa kila kinachotokea katika maisha yetu kimepata kibali cha Mungu. Na hivyo tunatakiwa kushukuru na kukubaliana na matokeo hayo bila kulalamika hata kama matokeo yake yanaumiza na ni vigumu  kuyakubali na wala Mungu hatupi sisi maelezo yeyote yale.

Ugumu wa kuishi kwa unyenyekevu ni kushindwa kwetu kujishusha, asili yetu binadamu tunataka kujikweza, tunataka kuonekana;  tunapenda kujulikana;   kuheshimiwa na kuogopwa. Ndio maana ni neema ya hali ya juu kwa wale wote ambao ni wanyenyekevu na wanaisha maisha ya unyenyekevu.

Tafakari yetu ya leo inatuonyesha kuwa  sifa nyingine ya mtu Mnyenyekevu ni kuwa mtegemea neema ya Mungu , Baraka na nguvu za Mungu kwa mahitaji na shida zake zote. Mtu ambaye sio mnyenyekevu huwa na kiburi, majivuno hayuko tayari kusubiri Baraka za Mungu katika maisha yake, kwani kwake Mungu sio chochote; yeye anaweza kufanya ka kujitosheleza katika haja zake. Lakini Zaburi ya 55.22 umtwike bwana mzigo wako naye atakutegemeza, hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele. Tunatakiwa kumpa bwana mizigo yote ambayo tunayo na yeye ataibeba kwa ajili yetu, hata amuru wewe utabike.

Unyenyekevu ni kielezo cha sisi kuona tuna mapungufu yetu, hivyo kutengeneza utegemezi wetu na kuomba au kutegemea nguvu za Mungu katika kupata mafanikio ambayo tunayo yahitaji. Hivyo madhaifu yetu ni sehemu ya mpango wa Mungu ili kutonyesha sisi yeye pekee ndio kimbilio letu lakini twatakiwa kuwa wanyenyekevu mbele ya Mungu ili uwepo wa Mungu ufanye kazi ndani yetu. Kwa hiyo palipo na Mungu na unyenyekevu upo pia, na unyenyekevu unatemebea  katika uwepo wa Mungu.

1 Peter 5 hivyo hivyo ninyi vijana watiini wazee. Naam ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema. Tunatakiwa kuwa wanyenyekevu ili tupate neema ya Mungu.
Bali tusipokuwa hivyo na tukaleta kiburi chetu Mungu atakuwa kinyume chetu, lakini tukiwa wanyeynyekevu Tutapewa neema kwa wakati muafaka na Mungu atatimiza haja za mahitaji yetu na hatupaswi kuwa na mashaka.
Hosea 13: 4-6 Lakini mimi ni Bwana Mungu wako tangu Misri; wala hutamjua Mungu mwingine ila mimi; wala zaidi ya mimi hakuna Mwokozi. Mimi nilikuja katika jangwa katika nchi yenye kiu nyingi. Kwa kadiri ya malisho yao, kwa kadiri  iyo hiyo walishiba; walishiba na moyo wao ukatukuka: ndiyo sababu wamenisahau mimi.
Tafakari yetu inatuonyesha Jinsi Musa alivyowaonya watu wa Mungu tukisoma kutoka  8: 11-17  kuhusu nini kitatokea watakapo kuwa wametulia katika nchi ya ahadi: jihadharini, usije ukamsahau Bwana, Mungu wako kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake ninazokuamuru leo. Angalia utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake.
Na makundi yako ya ngombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;  basi hapo moyo wako usiinuke ukamsahau Bwana, Mungu wako aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa; aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyokutolea maji katika mwamba mgumu. Aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako. Hapo usiseme moyoni mwako, nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo.
Yeramia  13: 9-10  jinsi hii nitakiharibu kiburi cha yuda na kiburi kikuu cha yerusalem. Watu hawa waovu wanaokataa kusikilizamaneno yangu, wanaokwenda kwa ushupavu wa mioyoyao, na kufuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu, watakuwa hali moja na mshipi huu, usiofaa kwa lolote.
Tafakari yetu inatufundisha kuwa watu wanyenyekevu hawataki makuu; hawapendi kujikweza kwani wanajua Mungu atawekweza tu. Bali wasio wanyenyekevu wao hupenda kuonekana kama Mathew 23:6 inavyotufundisha; hupenda viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi.
Tafakari ya leo inatuonyesha kuwa Mungu anapenda sisi wenyewe tumpe shida zetu, japo yeye anazijua lakini anataka sisi tuonyeshe unyenyekevu wetu kwake. Tukumbuke kuwa unenyekevu ni neema kutoka kwa Mungu; na kila kitu ambacho tunacho ni zawadi pia toka kwa Mungu, uwezo ,mafanikio vipawa vyote tumepewa kama zawadi. Hivyo vyote ambavyo tumepata angeweza pewa mtu mwingine. Je unaitumiaje zawadi yako kwa manufaa ya Mungu.
1 Peter 5: 8-9 Tunatakiwa kumpelekea shida zetu mungu lakini wakati huo huo kuwa makini na hila za shetani. Huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. Nanyi mpigenihuyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.
Tukumbuke kuwa kila mmoja wetu ana mapungufu yake, inaweza kuwa sehemu ya tabia  mbaya, vishawishi hivyo shetani naye anatumia mapungufu yetu katika kuondoa unyenyekevu wetu kwa mungu kwani atatujengea kiburi na tutajiona kuwa hatuhitaji nguvu ya Mungu katika maisha yetu yatupasa kuwa makini. Hii ni tafakari yetu ya leo –Amina
Emmanuel Turuka


No comments:

Post a Comment