WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Thursday, March 10, 2016

NI WAJIBU WETU KUWAHESHIMU NA KUWAPENDA WAZAZI WETU


Kutoka:20:12

March 10

Tafakari ya leo tunaangalia wajibu wetu kama watoto kuwapenda kuwajali wazazi wetu; hili sio ombi ni sheria ambayo Mungu ameiweka katika kitabu chake ambacho ndio mwongozo wetu katika maisha yetu ya kila siku ya ukristo wetu. Kama tunavyo soma katika kitabu cha kutoka 20:12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.

Hata katika 2 Timotheo 1-2 inatukumbusha kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu wakuwa wenye kujipenda wenyewe, na kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukanana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio wasafi;

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa tunatakiwa kuwaheshimu wazazi wetu, na sio kuwaheshimu, viongozi wa serikali, au walimu au marafiki, wafanyakazi wenzetu bali wazazi wetu; siri kubwa hapa ni kuwa tukiweza kuwaheshimu wazazi wetu, tukifanya hivyo  mahusiano mengine yote yatakuwa rahisi katika kuyatekeleza. Heshima inaanza nyumbani; kama huwezi kuwaheshimu watu wa nyumba yako utawezaje kuwaheshimu watu wengine wa mbali? Ndio maana shetani anafanya jitihada kubwa ya kuharibu uhusiano mzuri kati ya Wazazi na watoto ili wasitimize adhima yao kutekeleza amei hii ya Mungu bali tuangamie;

Tafakari yetu leo hii inatukumbusha kuwa jinsi tunavyoweza kuwaheshimu na kuwapenda wazazi wetu ndivyo itakavyo kuwa rahisi kwetu kumpenda na kumheshimu Mungu. Huu ni muhimili mkubwa sana katika maisha yetu; wazazi ni kiungo muhimu sana kati yetu na Mungu na wao wanamwakilisha Mungu hapa duniani. Hapa ndipo wazazi wetu wanatakiwa kuwa makini kwa sababu Sisi watoto tunafahamu kwa wao ndio wawakilishi wetu wa kwanza hapa duniani na jinsi taswira ya matendo yao kwetu inakuwa aina ya Mungu ambaye sisi tunamwona kupitia kwao.

Kama wazazi wetu hawawezi kuonyesha mfano mzuri wa maisha yao kwa watoto; sisi tunamjua Mungu wetu na Hulka zake; je sasa mungu tunayemwona kupitia kwao ni Mungu wa upendo, neema, wa msahama, mafanikio? Au Mungu tunayemwona kupitia kwao anageuka kuwa Mungu wa Tamaa za mwili, Uzinzi, hasira, wizi, mkatili, mnyanyasaji na kadhalika?

Tafakari ya leo inatukumbusha  kuwa Baba na Mama wamepewa nafasi kubwa sana katika maisha yetu; na tunatakiwa kuwaheshimu wote katika uzito sawa. Ni wajibu wetu kuwatii na kuwaheshimu kwani Mzazi mwema hatakuwa sababu ya wewe ufanye dhambi yeyote ile. Waefeso 6: 1-3  Enyi watoto watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki:  Waheshimuni baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, upate heri, ukae siku nyingi katika dunia

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa tunatakiwa kuonyesha adabu kwa wazazi wetu tunapoongea nao hasa kwenye hadhara ya watu na hasa mbele ya watoto wetu; hata kama hatukubaliani nao yale wanayosema bali tunaowajibu wa kuonyesha adabu na uvumilivu. Tukumbuke kuwa jinsi ambavyo tutakuwa tunawawatendea wazazi wetu ndivyo hata watoto  wetu watakavyo tutendea.

Tafakari ye leo inatukumbusha kuwa Mungu ndio asili ya uhai wetu lakini wazazi wetu ni kiungo muhimu ambacho Mwenyezi Mungu alikichagua katika kutuleta sisi duniani. Tunafahamu kuwa kuna baadhi ya wazazi kwa kweli wao ndio wanakuwa waaribifu wa maisha ya watoto  wao. Lakini bado kama watoto tunatakiwa tuwaombee na wapate msamaha wa Mungu lakini bado tunawajibu wa kuwaheshimu.

Mungu anajua machungu yote ya nyuma lakini anangalia leo yetu na kesho yenye faraja katika maisha yako. Ndio maana anatuambie leteni mizigo yenu kwangu name nitibeba kwa ajili yenu. Tukumbuke kuwa pamoja nay ale yote yaliyotokea katika maisha yetu bado sisi ndio pekee tutayoyajenga maisha yetu. Hivyo itakuwa vyema kama tutaweza kuishi maisha yenye uadilifu, mafanikio na furaha ya kweli na wazazi wetu watutupenda kwa hilo.

Tunafahamu kuwa wakati mwingine inakuwa vigumu kutekeleza amri ya msamaha dhidi ya wazazi wetu kwa makosa yao ya makusudi na kusababisha kukosekana kwa upendo kati ya watoto na wazazi kama tatizo, la utoaji mimba, ubakaji na kadhalika; matendo kama haya hupoteza kabisa upendo wa mzazi kwa motto; hivyo mtoto anakua katika maisha hatarishi na mtoto anajenga hasiri ya kulipiza kisasi cha kutaka kuua na kuwa huru kutoka katika minyororo ya wazazi wa namna hii. Mara nyingi tunawaona wazazi wetu kama vikwazo katika maisha yetu na sio kisima cha busara cha kutusaidia sisi kusonga mbele.

Ndio maana mwenyezi Mungu anatukumbushga leo katika mazingira ya namna yeyote yale bado tunawajibu wa kuwaheshimu wazazi wetu na kuwaombea kwa Mungu. Huku tukiwasamehe dhambi zao. Mungu alipoweka hii amri ya kuwaheshimu wazazi wetu alijua kabisa wazazi ni chanzo cha familia na nyumba ndio msingi mkubwa wa jamii na jumuia zetu; na hakuna jumuia zetu zinataweza kuwa na msingi imara kama hatutakuwa na familia bora ambazo zinajenga jumuia hizo; kinachofanyika nyumbani ndicho kinachofanyika katika jumuia zetu;

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa tukiyaangalia maisha yetu huko nyuma tunaona kuwa tumekuwa watoto ambao kwa namna moja au nyingine hatukuwapa heshima inayotakiwa kwa wazazi wetu, tume waonyesha kiburi, dharau na hata kuto fuata ushauri wao. Lakini bado ninakila sababu leo kusema asante sana Mungu kwa kunijalia wazazi ambao wamenilea na kunifikisha hapa nilipo leo. Ni ukweli kuwa katika namna moja au nyingine pengine hatukubaliana nao katika baadhi ya mambo; na pengine walitutendea vibaya lakini yoye ya yote tunatakiwa kuwasamehe ili tuweze kutembea katika amri hii ya Mungu tunatakiwa kuwaheshimu wazazi wetu na kuwapenda. Hii ni amri na wala sio ombi na hatuna njia ya kukwepa amri hii. Wazazi wetu wanastahili heshima kwa upendo wote ambao tunastahihi kuwapa.

Hii ndio tafakari yetu ya leo. Ameni

Emmanuel Turuka



No comments:

Post a Comment