WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, September 30, 2016

UWEZO WA KUPIMA MAPUNGUFU YETU UNATOKA WAPI?

Tafakari ya Leo tujiulize je uwezo na hekima ya kupima mapungufu yetu tunaupata wapi? Je maisha yetu yamekamilika na  hatuna mapungufu?

Thursday, September 29, 2016

KWA NINI TUNAKAWAIDA YA KUFANYA MAAMUZI KATIKA JAMBO MOJA?

Tarafakari yetu Leo tunaangalia upungufu wetu ambao tunao, kamwe hatuangalii ukuu wa Mungu juu ya maisha yetu. Bali sisi maamuzi ya kushukuru au kulaani huangalia jambo moja ambalo tunalitilia mkazo.

Wednesday, September 28, 2016

KULA NA KUNYWA KWETU KUNATOKA WAPI?

Tafakari yetu Leo tuangalia je yote ambayo Mwenyezi Mungu ametufanyia ameyafanya kwa upendo mkuu. Tukisoma Mhubiri 3: 11,13 Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho. 13 Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.

Tuesday, September 27, 2016

UNATAKA NIKUFANYIE NINI?

Tafakari yetu ya Leo Yesu anakuuliza wewe unataka ukufanyie nini? Yule kipofu aliomba aponywe ili aweze kuona. Jemedali aliomba mtumishi wake aponywe. Je wewe unataka Yesu akufanyie nini?

Sunday, September 25, 2016

JE WEWE NI MPOLE?

Tafakari ya Leo tujipime kwa kiwango gani wewe na mimi ni wapole.  Je tunaelewa nini maana ya upole na kuwa mfuasi wa kristo? Wafilipi 2:3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.

Friday, September 23, 2016

NI WAJIBU WETU KUSUBIRI

Tafakari ya leo inatukumbusha umuhimu wa kusubiri: Zaburi ya  106:13 inatukumbusha adhaa ya kushindwa kusubiri Wakayasahau matendo yake kwa haraka,Hawakulingojea shauri lake. Mara nyingi tunakosa subira katika kusubiri maombi na haja zetu kupata kibali cha Mungu. Tukumbuke kuwa Mwenyezi Mungu hutujibu kwa wakati wake na sio kwa wakati wetu. Wakati wa Mungu ndio wakati sahihi kupita wakati wetu. Hivyo ni wajibu wetu kusubiri.

Thursday, September 22, 2016

JE WEWE NI TAA?

Tafakari ya Leo tuangalie umuhimu wa taa katika maisha yetu ya imani: Je wewe unaogopa giza, na tunafanya nini kuondoa giza?

Wednesday, September 21, 2016

JE MAISHA YAKO YANA THAMANI:

Tafakari ya Leo tuangalie  nini thamani ya maisha yetu. Je maisha yako yanathamani? Kwa kiasi gani?

JE WEWE UNA AMINI UMEBARIKIWA?

Leo jiulize je wewe umebarikiwa na unaitumiaje baraka hii ya kubarikiwa. Ni tafakari yetu ya leo ambayo inatakiwa kuamsha unyenyekevu ndani ya maisha yetu.

Monday, September 19, 2016

ASANTE MUNGU

September 19


Ni wajibu wetu kushukuru kwa neema ya ufahamu wa maisha yetu kwani daima tumekuwa tukikosa hii busara ya utambuzi; Ni jukumu letu kusema asante;

Sunday, September 18, 2016

AMANI YA KWELI INATOKA WAPI

September  18


Mungu wetu ndio asili ya amani yetu; amani ya kweli huletwa na Mungu na amani hiyo tayari Mungu ametujalia sisi tuweze kuiishi; laniki kwa tamaa zetu tumekuwa chanzo cha kuharibu amani yetu.

Saturday, September 3, 2016

WEWE NI MUNGU

September 3



Tafakari yetu leo ni kweli kuwa Mungu anabaki kuwa Mungu; ni wajibu wetu kumwabudu;

Friday, September 2, 2016

YESU NI BWANA

September 2


Tafakari yetu leo inatuonyesha kuwa ukuu wa Yesu hauna mipaka yuko pande zote za dunia kwa wakati mmoja; Hivyo Yesu ni kimbilio letu;