WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Wednesday, May 4, 2016

WAACHENI WATOTO WADOGO WAJE KWANGU



May 4

Mathayo 18: 3-4

Tafkari yetu leo tunaangalia jinsi Yesu alivyotuagiza kuwa tukiwa kama motto mdogo ni rahisi sana kuingia katika ufalme wa Mungu; Je Kwa nini yesu anataka sisi tuwe na fikra na akili za motto mdogo katika kuridhi ufalme wa mbinguni? Watoto wadogo mara zote ni wategemezi wa wazazi wao kwa kila kitu; ni wasikivu, na pale wanapokosea wataumia watalia lakini mwishoni hujinyenyekeza na kuomba msamaha, hawana kiburi, hawafikirii madaraka , wala mali na kila kitu mbele yao wanachokipata wanashukuru na kufurahia; hupenda kujifunza na hata wakikosolewa hucheka na kujaribu tena;
Tafakari yetu leo wazo kubwa ni ugumu wa sisi kama watu wazima ambao tayari tumeshakuwa na akili zetu zimeshakuwa na tunakuwa na ugumu wa kujinyenyekeza mbele ya mungu tukitambua kuwa sisi tunaweza kujitegemea sisi wenyewe na hatuhitaji msada wa Mungu; Yesu hapa anatukumbusha kuwa ili ukuu war oho unahitaji unyenyekevu ambao watoto wanao na sisi watu wazima tunapingana nao; tukumbuke kuwa unyenyekevu ni hatua ya kiroho ya kukua na sio hatua ya kujidumaza;  Yesu anatufundisha kuwa lazima tubadilike kama tunataka kuingia katika ufalme wa mbinguni; Lazima tutubu makosa yetu kwa moyo na kuweka kusudio la kuacha kutenda dhambi au kuendelea kutenda dhambi. Lazima tabia zetu kuhusu dhambi ziwe za kupinga dhambi.

Tafakari yetu  tukisoma 1 Wakoritho 14: 20 inatukumbusha kuwa Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima. Akili ya watotohawafikirii mabaya; ma hawafikirii kutendewa mabaya humpenda kila mtu, humwamini kila mtu, humfurahia kila mtu wamwonaye; hivyo sisi kama wakristo tunatakiwa kubadilika kuwa wema, kuishi katika maadili mema, kutenda mema, na tukifanya hivyo thawabu yetu itakuwa kubwa mbele ya Mungu; ndio hata tukisoma kutoka Injili ya Yohana 3:3-5 Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.  Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?  Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. Kwa kuzaliwa kwa mara nyingine ni kuwa tayari kubadilika na kuuvaa unyenyekevu ambao ni msaada mkubwa katika matendo yetu katika kukamilisha safari yetu ya Mbinguni;

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa Mtoto hana hadhi yeyote ndani ya familia au jamii; kwa vile huonekana kuwa ni tegemezi basin a hana nafasi ya kufanya maamuzi yeyote; Hili ni tatizo kubwa kwetu kwani tunapenda kuheshimiwa, kunyenyekewa, hata wakati mwingine kuabudiwa; tunatakiwa tuwe watu ambao sio kitu katika ulimwengu huu bali tukijua kuwa Mungu ndio tegemeo letu na ngao na kinga yetu; Kama vile watoto wanavyowategemea wazazi wao kwa kila kitu nasi ni wakati wetu wa kumtegemea Mungu kwa kila kitu. 

Hii ndio tafakari yetu ya leo Amina

Emmanuel Turuka









No comments:

Post a Comment