WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Saturday, May 14, 2016

WEMA NA FADHILI ZA BWANA

May 14

Tafakari ya leo tujikumbushe wema na fadhili za Mungu ambazo zimeendelea kutuzunguka kila siku katika maisha yetu. Sisi tumepata bahati ya kubwa ya ufadhili na upendeleo wa  Mungu katika kila hatua ya maisha yetu.

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa pale ambapo tumekuwa tukikosea bado kwa upendo na  neema yake tumekuwa tukipata msamaha wa makosa yetu.

Tafakari yetu vile vile inatufundisha jinsi ambavyo kwa upendo wake alimtoa kwetu bwana wetu Yesu Kristu awe kimbilio letu na ondoleo la dhambi zetu. Damu yake iliyomwagika msalabani alipokufa katika kifo cha msalaba imetupa sisi ushindi wa ajabu sana.

Tunakila sababu ya kutembea kifua mbele kwani wema wake unaendelea kutuzunguka daima. Wema wake  hauna mipaka,  wema wake ufunguo wa maisha yetu  katika safari yetu ya mbinguni.

Tuna kila sababu ya kushukuru na kusema Aleluya. Ni wajibu wetu sasa kumpa Mungu shangwe zetu bila kukoma. Amina

Emmanuel Turuka

No comments:

Post a Comment