WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Wednesday, May 11, 2016

HATUJECHELEWA MUNGU KUSAFISHA UCHAFU WETU




May 11

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa pamoja na uchafu wote ambao tunao katika maisha yetu, ni wazi kabisa hakuna sabuni yeyote ambayo inaweza kutusafisha na  uchafu huo. Sabuni pekee ni  damu  ya  Yesu.  Mkumbuke Daudi  alivyomlilia Mungu baada ya  kufanya dhambi ya kuua, ili kufanikisha adhama yake ya kuhahalisha uchafu wa zinaa.

Sisi leo tunafanya uchafu wa kila aina na  kujisifu kuwa nguvu yetu ya kibinadamu ina nguvu kuliko nguvu ya Mungu. Kwa kweli tunajidanganya sana. Uchafu ambao umezunguka mwili wetu, unatoka na na  kiburi chetu, na kujiona kuwa sisi tuna  akili ziadi ya Mumgu, afya njema ambayo tunayo ni haki yetu na haina uhusiano wowote na upendo wa Mungu; Lakini tunatakiwa kukumbuka kuwa hata   nguvu ni sehemu ya upendo wake kwetu ili tuweze kutimiza mahitaji yetu kulingana na mwongozo wake.

Leo hii sisi tumekuwa wale wanaoendesha Gari huku tukitazama nyuma,  hivyo hatuko tayari kwa ufalme wa Mungu. Tunatakiwa kufuata maelekezo na mafundisho ya bibilia ili tuweze kutembea katika njia ya bwana inavyotakiwa tutembee;


Siku ya  leo  tujitafakari kuwa hatujechelewa kusafisha uchafu wetu,  kwa sharti moja, la kumkabidhi Mungu maisha yetu kwa dhati na kuishi kulingana na sheria zake. tukitimiza ili amri kuu ya upendo na kuishi kwa vitendo - Amina

No comments:

Post a Comment