WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Tuesday, May 3, 2016

TAZAMA ILIVYO NJEMA NDUGU WAKIKAA KATIKA UPENDO


May 2

1Peter 3:8

Tafakari ya leo inatukumbusha kuhusu umuhimu wa wa kuishi pamoja kwa upendo na maelewano; kama waraka wa 1 Petro 3:8 unavosema Neno la mwisho ni hili; mwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu;  kama Waraka wa Waefeso 4: 2-8 unavyoyukumbusha kuwa sote lazima tuishi kwa upendo na kuwa wamoja tukizingatia kuishi katika unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.  Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.  Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.  Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo. Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa. 

Tafakari yetu vile vile inasisitiza kuwa  bibilia inatukumbusha kuwa tunatakiwa kuishi kwa kupendana pamoja kama waraka wa Warumi 12: 15- 18 Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao. Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.  Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.  Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote. Tukumbuke kuwa pale penye amani na upendo furaha ya bwana utawala na watu wanakua katika neema ya Mungu na maarafa ya mungu; umoja wa kweli huzaliwa miongoni mwetu. Lakini pale ambapo pana chuki amani hutoweka neema ya Mungu na maarifa yake hutoweka pia; woga hutawala, uwazi hupotea shetani natawala na kuleta maangamizo ambayo mwisho wake humwangamiza mwanadamu na kumfanya kujenga kiburi na majivuno.

Tafakari ya leo neno la msingi katika kuishi kwa upendo na wezetu linatawalia na neno heshima; tukiweza kuwaheshimu wezetu na kuwapa haki wanayostahili upendo utatawala maisha yetu, na hakuna kiburi wala chuki kitapata nafasi katika maisha yetu; mwenyezi Mungu anatamani sana sisi tuwe tofauti katika dhana nzima ya kuishi pamoja kwa kupendana; Mungu anataka sisi tuwe chanzo cha Baraka kwa wenzetu; tuwe watu ambao hatutamani wenzetu wapate shida au tabu; na pale wanapofanikiwa tusiwe watu wa kwanza kuwaonea wivu na kuwachukia. Bali tushangilie pamoja katika mafanikio yao na tulie pamoja na kuwapa nguvu katika shida zao.

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa ili tuweze kufanikiwa lazima tukubali na kujikataa wenyewe; tusiwe watu ambao tunajijali wenyewe na kuona vitu bora vyote ni vyako na wengine hawastahili; bali tunahitaji kuwa wenyenyekevu na kuweka matakwa ya wengine mbele zaidi katika kuleta maisha ya upendo wa kweli miongoni mwenu na kufanikisha amri ya upendo wa kuishi pamoja. Ni jambo gumu ambalo linasumbua katika utekelezaji wake. Maisha yetu yamejaa choyo, umimi, wivu na unafiki; ni neema tu itakayo tusaidia kutekeleza dhana ya kuishi kwa pamoja kama ndugu kama tutaweza kusoma na kuelewa nyakati za Mungu na maarifa yake, katika kutekeleza upendo wa kweli .

Hii ndio tafakari yetu ya leo; Amina

Emmanuel Turuka



No comments:

Post a Comment