WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Tuesday, May 3, 2016

JE WEWE NI MKE WA LUTU?



May 3

Mwanzo 19:26

Tafakari ya leo tunatafakari maisha yetu hapa dunia kwa kuangalia zaidi lengo letu kubwa na hatima ya maisha yetu tunaielekeza wapi? Yesu kupitia injili ya  Luka 17: 28-29 Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;  lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote. Bwana wetu Yesu Kristo alituonya kuwa Mke wa Lutu alikuwa Baridi, hajali, hana utii sio tu kwa mumeo hata kwa Mungu ndio sababu hukumu ya mungu alishuka juu yake; Kama uilivyokuwa kwa Adam na Hawa ndivyo ilivyokuwa na Mke wa Lutu; Aliambiwa asigeuke nyuma na akageuka nguzo ya Chumvi kwa kupenda kuishi katika ulimwengu wa dunia na sio ulimwengu wa Kimungu.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa tulio wengi leo hii ni kama Mke wa Lutu, hatusikii sauti ya Mungu na maelekezo yake, na kama tunaisikia basi hatuko tayari kufuata haya maelekezo yake na tunaishia kuwa Nguzo ya chumvi ambazo zinatemebea na hazina huhai wa kimungu. Mathayo 24:12 inatukumbusha kuwa  na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa; Kama ilivyokuwa kwa mke wa Lutu kuwa pamoja na kuishi na mume ambaye alikuwa akimwogopa na kufanya kazi na Mungu kwa imani kubwa na Mungu Kuwapa zawadi ya Kuishi zaidi pale alipoamua kuwasha moto wa kibiriti na kuiingamiza Sodoma, Mke wake alishindwa kutembea katika Mwendo huu wa imani na kumwogopa Mungu.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa wakati huu Sodoma ilikuwa imejaa uchafu wa kila aina; hivyo mke wa Lutu sio tu alihamia Sodoma bali Sodoma ilihamia ndani ya Nafsi yake; alikuwa mwanamke ambaye alipenda na kuabudu anasa ambazo zilikuwa zikifanyika Sodoma; Ndio maana hakuweza kusikia sauti ya Mungu ambayo ilikuwa ikimwokoa katika maangamizi alijawa na kiburi cha anasa na hivyo alishindwa kutekeleza agizo la Mungu. Hivyo tatizo kubwa ni nini hapa? Mke wa Lutu aliupenda zaidi ulimwengu kuliko kumpenda zaidi Mungu;

Kama ilivyo kwa mke wa Lutu hata sisi leo tumesongwa sana na anasa za dunia hata ile damu ya yesu ambayo imetukomboa hatuipi thamani kwani matendo yetu hayafanani na thamani ya Damu hiyo. Hata hatufanyi majukumu yetu vile inavyotakiwa; hatuna nafasi ya kuwalea watoto wetu katika maadili ya kimungu; muda wetu mwingi tunapotezea katika maisha ya anasa za dunia hii; sauti ya Mungu daima inatuambia kuwa “Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea”. Lakini hatusikii sauti hiyo na tunaendelea na maisha yetu ya anasa za duniii hii. 

Tafakari yetu leo inaendelea kutukumbusha kuwa tuache dhambi ya kiburi ambayo ndio msingi wa dhambi nyingine zote; Tuwe wanyenyekevu tusikie sauti ya bwana na kutekeleza maagizo yake; tukumbuke kuwa utii ni sadaka ya juu sana, Yesu alituagiza kama tunampenda tutazishika amri zake; kutotii ni dhambi mbaya sana; Mungu anafurahishwa na utii wetu kwake na amri, mafundisho yake kwetu sisi kupitia Mwokozi wetu yesu kristo. Tunakumbushwa kuwa tusiwe kama Mke wa Lutu aliyeangalia nyuma kwa kufikiri kuwa dunia hii ndio zaidi kwetu kuliko Mungu. Tunatakiwa kuacha dhambi ya kiburi na kutekeleza utii kwa Mungu katika kuishi maisha yetu kama yeye anavyotaka sisi tuishi;

Tafakari yetu inatutadharisha na matendo yetu ya kuangalia Nyuma; Tumeagizwa tuangalie mbele ili tuweze kufuzu kuingia katika nyumba ya Mungu; lakini kwa kuangalia nyuma kama mke wa Lutu tunakuwa tumejiondoa wenyewe katika kushiriki utukufu wa Mungu; tukisoma Luka 9: 61-62 Mtu mwingine pia akamwambia, Bwana, nitakufuata; lakini, nipe ruhusa kwanza nikawaage watu wa nyumbani mwangu. Yesu akamwambia, Mtu aliyetia mkono wake kulima, kisha akaangalia nyuma, hafai kwa ufalme wa Mungu. Hatutakiwi kabisa kuangalia nyuma tunapoutafuta ufalme wa Mungu; Kuangalia nyuma hapa maana yake ni nini? Tunayaangalia maisha yale ya zamani, ya ulevi, uzinzi, uwongo, wizi, chuki, na kadhalika; tukumbuke kuwa hakuna maisha ya baadae bila mipango hiyo kupokea maelekezo ya Mungu ndani ya Nyoyo zetu. Agizo ambalo tunapata leo hatutakiw kugeuka nyuma na kuyarudia maisha yaliyojaa dhambi. Tumepata Baraka ya kukombolewa na damu ya Yesu jukumu letu sasa ni kusonga mbele na kamwe kuto geuka Nyuma.

Hii ndio tafakari yetu ya leo;

Emmanuel Turuka


 

No comments:

Post a Comment