WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Tuesday, May 17, 2016

JE UMEWEKA AGANO NA MUNGU

May 21

Ayubu 1:21

Tafakari ya leo tunangalia umuhimu wa kufanya agano na Mungu. Agano ni kitendo cha  kukiri kuwa tayari kutimiza ahadi ambayo umeweka. Bibilia inatukumbusha kuwa agano la Ayubu na Mungu lilikuwa la kutomsaliti pamoja na  mateso na shida zote ambazo alipata. Ayubu alisimama imara na kuitetea imani yake.

Tafakari yetu inatufundisha hata pale mke wake Ayubu alipo mbembeleza Ayubu kumwasi bwana alikataa kufuata ushauri huu  akijua kuwa Bwana aliyetoa ndiye mwenye mamlaka ya kutwaa.

Tujiulize leo mimi na wewe tumemwekea Mungu agano gani? Je wakati wa majibu bado tunaweza tunza agano hilo?  Ni wakati mzuri wa kujitafakari.  Kama ni mama au  baba wa  familia agano la ndoa mnalitekeleza kulingana na kiapo na mafundisho ya  bibilia? Je watoto wanatunzaje agano Lao la  utii na kuwaheshimu wazazi wao?

Tafakari ya leo inanyesha kuwa hili ni somo muhimu sana katika maisha yetu ya  kiroho jambo tunajua kutimiza agano ni  jambo gumu. Tupo kwenye dunia ambayo imejaa majaribu ambayo hutufanya tusahau kutimiza maagano yetu na Mungu. Habari njema hatujechelewa kabisa wakati wa utekelezaji wa agano au maagano ni sasa. Tumwombe Mwenyezi Mungu atufunulie hekima za kuona na kutekeleza maagano yetu naye  Amina.

Emmanuel Turuka

No comments:

Post a Comment