WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Thursday, February 25, 2016

ZABURI YA 23: BWANA NDIYE MCHUNGAJI WANGU



February 24

Tafakari ya leo hebu pamoja tutafakari Zaburi ya 23 ambayo inasema: Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. 
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. 
3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. 
5 Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika. 
6 
Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele

Zaburi hii ya 23 inatuomyesha uhusiano ambao uko kati ya Mungu na sisi waja wake; tunatambua kuwa kondoo hana sauti na mahitaji yake; lakini mchungaji ndiye anayefanya maamuzi ya mahitaji yake na natakiwa ayajue na awatekelezee; ndio maana Mwenyezi  Mungu anajua mahitaji yetu kabla hata sisi hatujemwomba.  Mwenyezi Mungu ametujalia sisi malisho mazuri na salama kupitia Bwana wetu yesu Kristo kwa kifo chake ametusafishia njia ya malisho mazuri, wajibu wetu sisi ni kufuata maelekezo yake. Ndio maana hataki sisi kama kondoo  wake tunywe maji katika chanzo ambacho sio salama, kama maji yanayotembea kwa kasi kwani sio salama bali ametutuyarishia tunye maji katika kisima  kilicho tulia na salama.

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa sisi hatuna uwezo wa kumshinda shetani bila msaada wa Mungu. Tukizingatia tabia yetu ya udhaifu ambayo tunayo toka kuumbwa kwa dunia. Tabia hii ndiyo inayotupelekea sisi kuanguka katika dhambi mara kwa mara; Hatutakiwi kumwachia nafasi shetani hata kidogo na pale tunapoanguka katika dhambi tunatakiwa kuomba msamaa kwa Mungu wetu; Na kuomba ulinzi mzuri kutoka kwa Mchungaji Mwema ambaye alikufa Msalabani   kwa ajili ya wokovu wetu Amina.


No comments:

Post a Comment