WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Saturday, February 20, 2016

ILI TUWEZE KUTAFAKARI VYEMA TORATI YA MUNGU TUONDOE KIBURI MOYONI MWETU



February 19
Tafakari ya leo tuangalie agizo la Mungu kwa wana wa Israeli wakati wa uongozi wa Nabii Joshua: Mungu alimwagiza Joshua kwa kuwaambia kuwa Joshua 1:8 kitabu hiki cha Torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.
Huu ni ujumbe mzuri katika tafakari yetu ya leo; kwani maagizo haya yanatufundisha kuwa jukumu letu ni kutekeleza maelekezo ya Mungu na kwa kufanya hivyo Mwenyezi Mungu wetu atakuwa yuko juu ya maisha yetu. Tukitafakari na kufuata mwongozo kupitia nukuu hii ni wazi kuwa tutapatiwa chochote tunachohitaji, iwe utajiri, mafanikio katika maisha yetu, ndani ya familia zetu, sehemu zetu za kazi na ndani ya jumuia zetu.
Lakini tunakazi kubwa ya kufanya ili kufikia mafanikio haya ukumu letu kubwa ni kusoma kuelewa na kutafakari neno mungu na kisha kuishi kulingana na neno hilo siku zote za maisha yetu; sio jambo la mara moja. Tafakari ya leo inataka sisi tujenge mazoea ya kulitafakari neno na sheria za mungu siku zote za maisha yetu.
Ni ukweli amabo pengine hatuuelewi kuwa Mungu hajetuahidi sisi kuwa atatupa busara, lakini anajua kama tutasoma na kuelewa yaliyoandikwa na kuagizwa katika kitabu cha torati tutaweza kuishi na kufanya mambo yetu au maamuzi yetu kwa busara kubwa sana.
Tujue kuwa neno lisiondoke kinywani mwetu linatufanya sisi kuwa karibu sana na Yesu. Na agizo hili litakuwa ni chachu ya sisi kujua kuhusu ukweli wa Mungu na miujiza yake kwetu, na ukweli ambao hatuwezi kuujua kuhusu yeye kama hatutakuwa tayari kusoma na kuelewa na kutafakari kitabu hiki.
Je sisi wafuasi wa Kristo tunatimiza wajibu wetu kulingana na kitabu cha Torati? Tu wakweli kwa kiasi gani? Wawajibikaji kwa kiasi gani, tunazingatia sheria za Mungu na za nchi kwa kiasi gani? Je tunakumbuka ahadi ya Mungu kuwa tukitimiza ahadi zake tutapata neema ndani ya maisha yetu; siri kuwa ya mafanikio kulingana na kitabu hiki cha Torati ni UTII: Tukumbuke kuwa utii huleta amani, utii ni ufunguo pekee ambao Mwenyezi Mungu Kupitia Bwana wetu Yesu Kristo ametufungua milango yote ya baraka kwetu. Je tunatumia funguo hii ipasanyo?
Tafakari ya leo inatuonyesha kuwa tunashindwa sana kutimiza maelekezo ya Mungu kuhusu utii na kutufanya tukose baraka nyingi sana. Je wewe na mimi utii wetu kwa Mungu uko kwa kiwango gani? Maagizo ambayo Mungu alimpa Joshua yanatusaidiaje sisi leo? 
Je tunatafakari neno la Mungu Mchana na Usiku? Au maisha yetu ya kila siku yamechukua nafasi ya kwanza ndani ya maisha hivyo hatuna muda kabisa wa  muda wa kutafakari Torati ya Mungu  kwa dhati kabisa? 
Kama tunafanya hivyo bado tunaendekeza kiburi chetu ndani ya mioyo yetu jambo ambalo Mwenyezi Mungu alipendi sisi tufanye. Ondoa kiburi chako na tuanze kutafakari neno la Mungu.

Hii ndio tafakari yetu ya leo; Amina

No comments:

Post a Comment