WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Wednesday, February 17, 2016

WAJIBU WETU NI NINI KWA MUNGU KATIKA MIJUMUIKO YETU?


February 17,

Tafakari ya leo hebu tuangalie dhana ya  mijumuiko wa wakati wa kumwabudu Mungu. Kanisa linawajumuisha wapendwa katika kutimiza wajibu mmoja mkubwa kwa kumwabudu, kumsifu na kumshukuru Mungu; hata yale makanisa ya kwanza kabisa katika mijumuiko yake yalikuwa na lengo moja kubwa kumsifu Mungu, kwa sala na nyimbo na neno la shukrani.

Tafakari yetu ya leo inatumbusha kuwa makanisa ua mijumuiko yetu ya imani iwe na lengo la kutenda haki ya kumsifu Mungu, kumshangilia Mungu na kwa Baraka zake kupitia mikusanyiko yetu tumepewa uwezo wa kuwaombea wenye shida mbalimbali, za magonjwa, vipato na maisha mema yenye kibali cha Mungu. Tuanajua katika makanisa yetu tuna washiriki ambao wanauwezo wa kifedha kuliko uwezo wa kanisa. Kamwe tusiwageuze hao kuwa miungu watu wetu, kaw kuwasifu wao zaidi kukiko Mungu kwa vile wao tunawaona.

Tukisoma kitabu cha 2 Wakorinto 4:15  kwa maana mambo yote ni kwa ajili yenu, ilineema hiyo ikiongezwa sana kwa hao walio wengi shukrani izidishwe, na Mungu atukuzwe . Kuishi kwa imani. Tukumbuke kuwa Mungu ndiye atupaye sisi mkate wetu wa kila siku, ni yeye pekee awezaye kutupa sisi mbegu  na mazao yetu yakaongezeka mara dufu.

Hii inatakiwa kuwa ni sehemu ya maisha yetu sisi wakristo kwa kuendelea kumpa sifa na mtukufu Mungu wetu kila siku; kama 2 wakorinto 9: 11 inavyotuambia mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. Hivyo hili linatakiwa kuwa ni jukumu letu la kila siku. Tukumbuke kuwa sio tu tunapata wokovu toka kwake bali tunapata kila kitu toka kwake. Kama sio Mungu unapata wapi jeuri ya afya njema?

Paulo katika kitabu cha Waefeso 5:3 anasisitiza kuwa  lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wotewa kutamani, kama iwastahilivyo wakatakatifu. Wala aibu wala maneno ya upuuzi wala ubishi; hayo hayampendezi bali afadhali kushukuru. Hivyo Tafakari ya leo unasisitiza katika kushukuru, kushukuru kushukuru. Tunapofungua midomu yetu tujiepushe na maneno yote mabaya, machafu ambayo hayampendezi Mungu au jirani yako. Bali tufunguapo midomo yetu imiminike kwa maneno ya shukrani. Tuombe kujazwa na Roho wa bwana kwani yeye ndiye kioo cha shukrani atatupa maneno mazuri ya shukrani.

Sala na kushukuru iwe ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku, tunatakiwa tuanze sana kujijengea utamaduni wa kushukuru na kutoa shukrani kwa kila kitu na kwa wakati wowote; tukianza  kujenga utamaduni wa aina hii hata maisha ndani ya Jumuia zetu yatabadilika na tutabarikiwa sana, kwani katika Kristo unakaa utimilifu wote wa mungu kwa jinsi ya kimwili.

Paulo alipokuwa akiongea na Wakolosai 3: 15, 17 aliwaambia Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani. Na kila mfanyalo kwa neno au kwa tendo, fanyeniyote katika jina la bwana yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa tuendelea kusali bila kuchoka ikiwa ni sehemu ya muhimu ya maisha yetu katika kusifu na kushukuru kwa Mungu wetu. Sala ni kitu ambacho kinatakiwa kuwa cha furaha daiam na unafurahia kufanya hivyo, lakini kama wewe wakati unapomshukuru Mungu kwa sala  unakuwa huna furaha ujuwe kuwa bado unatawaliwa na kumilikiwa na mambo ya ulimwengu huu. Hivyo ukijikuta katika wakati huu inatakiwa umwombe roho Mtakatifu akubadilishe na atakupa furaha ya kweli wakati unasali.


Tafakari ye leo wakati tunaendelea na kipindi hiki cha toba tunatakiwa kufurahi kila wakati, tusali kila wakati, na tumtolea Mungu shukrani kila wakati.  Mungu anatupenda san asana na anataka sote tushiriki naye katika karamu ya mwisho tukiimba na kusifu pamoja naye hii ndio tafakari yetu ya leo.

No comments:

Post a Comment