WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Thursday, February 25, 2016

NENO AMINA LINATUKUMBUSHA NINI?





February 25

Katika tafakari ya leo tunajikumbusha ukuu wa neno Amina: Neno AMINA linalotumika sana katika maswala ya imani,  ni neno lenye maana nzito kwani ni neno ambalo limetumiwa sana katika bibilia na katika sala na ibada zetu za kila siku.

Neno Amina linaashiria  umoja wetu  katika kuamini kile ambacho kimesemwa au kuombwa kwa Mwenyezi Mungu: Neno Amina linatuunganisha sote katika sala au maombi na kukubalina katika umoja wetu mbele ya Mwenyezi Mungu.

Kwa ufupi ni neno linaloashiria “na iwe hivyo”; “tunakubaliana katika hili tunaloliomba”;  “tunaamini katika uhakika au kuwa na uhakika wa kile tunachokiomba au kukisifu”.

Tunasema neno Amina wakati wote wa ibada zetu za kila siku, katika sala zetu; Katika mijadala yetu; kwa ujumla Neno Amina linahitimisha sala na maombi yetu ikiwa ni  kielelezo cha makubaliano yetu na MUNGU.

Tukisoma kutoka katika kitabu cha kumbukumbu la Torati 27:16 inasomeaka hivi na alaaniwe amdharauye baba yake au mama yake. Na watu wote waseme, Amina. Hii inamaanisha kuwa wote wanakubaliana na laana hii kwa umoja wao.

Tafakari ya leo inatuonyesha kuwa Amina inamaanisha kuwa tunakubaliana na Baraka zote, ikiwa ni katika kuzipokea; Zaburi ya 72: 19 inasema kuwa jina lake tukufu na lihimidiwe milele; Dunia yote na ijae utukufu wake. Amina, Amina

Tafakari ya leo inatuonyesha jinsi Yesu alivyosema neno Amina katika mafundisho na mahubiri yake kuliko mwalimu mwingine yeyote katika Bibilia. Katika John 3:3 Yesu akajibu Amina amina nakuambia Mtu asipozaliwa mara ya pili hawezi kuuona ufalme wa Mungu. Katika majibu na mafundisho ya Yesu alikuwa anatuonyesha kuwa yale aliyokuwa akiyafundisha na yawe hivyo. Hapa tunajifunza kuwa neno amina linaonyesha uthibitisho katika kukabiliana Na yale ambayo yamesemwa au kufundishwa.

Somo muhimu leo ni kuwa "Amina ," tunasema , wakati wowote na tunamthibitishia Mungu kuwa  toka imara na tuamini kuwa kile tunachokiomba tunaomba tupate Baraka kutoka kwa Mungu.

Neno Amina tukilisema kwa dhati  Mungu atatimiza ahadi ya maombi yetu na kupata  neema na baraka tuziombazo tukumbuke kuwa ahadi zote za Mungu tunazipata tukiamini na kushukuru kwa kutumia neno lenye nguvu Amina. Kila kitu ambacho Mungu ameamwahidi  mwanadamu, atatimiza. Tukumbuke kuwa Yesu wakati anasulubuwa tukisoma Luka 23: 43 akamwambia Amina nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
 
Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa neno AMINA lina nguvu sana, kwani tunalitumia mwishoni mwa sala zetu, tukiwa na maana kubwa ya asante kwa Mungu kwa kupokea maombi yetu. Hivyo Amina inatufungulia kila ahadi ya baraka, amani , utoaji , faraja , msamaha, uzima, na utakatifu  tukiendelea kutambua kuwa yeye ni mwenye utukufu na nguvu, milele na milele. Amina. 





No comments:

Post a Comment