WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Tuesday, February 23, 2016

Tafakari ya Heri wenye kuleta Amani





 February  23

Katika Tafakari ya leo tunaendelea kuungana na Mtumishi wa Mungu Dr. Aba Mpesha Ambaye anatukumbusha umuhimu wa kudumisha amani katika maisha yetu ya kila siku;

Tafakari  ya Heri wenye Upole inanikumbusha maneno ya Bwana Yesu kuhusu AMANI. Yesu alisema: Heri wenye kuleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu (Matayo 5:9).

Ukitafakari kwa kina, wito wa Yesu kwa wafuasi wake ni kueneza Amani.  Wote walioitwa na Yesu, walikutana na Amani – Yesu ambaye ni mfalme wa Amani. Kwa hiyo, Yesu ndiyo Amani yao.

Kusema kweli, wafuasi wa Yesu hawakuiitwa kuwa na Amani tu, pia walipaswa kuleta Amani. Wangeitwa kuwa na Amani bila kupata agizo la kuleta Amani, wangekuwa watu wa ubinafsi. Kwa sababu hawakuitwa wawe na ubinafsi, waliagizwa kukana vurugu na malumbano. Vurugu na malumbano havisaidii kutimiza lengo ya Yesu la kuleta Amani. Ufalme wa Yesu ni wa Amani tele. Ndiyo maana wote walio kwenye jumuiya ya Yesu Kristo husalimiana na busu la Amani.

Wanafunzi wa Yesu malisisitiza kudumisha Amani kwa kuchagua kuteseka badala ya kufanya wangine wateseke. Hata Petro alijifunza hilo kutoka kwa Yesu usiku ule Yesu alivyokamatwa, Petro katika kumtetea Yesu, alimkata sikio mtumishi wa kuhani mkuu. Ebu sikiliza Yesu alisemaje. “Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamizwa kwa upanga.” (Matayo26:52).

Ni kweli wafuasi wa Yesu wanapaswa kuhifadhi jamii, wakati dunia inavunja jamii. Wanapaswa kukana kujitutumua binafsi na kukaa kimya wakikumbana na chuki na dhuluma.
Ni kwa njia hii wafuasi wa Yesu ushinda  uovu na wema.

Ebu jiulize, jamii yetu ambayo imelea utamaduni wa vurugu na malumbano, ingekuwaje kama watu wote wangekana vurugu na malumbano, na badala yake wakatekeleza utamaduni wa Amani. Ni kweli tutaitwa watoto wa Mungu na kuirithi nchi tuliyopewa na Mungu, kwa sababu Amani itatawala.

NAAMINI HII NI DUNIA TUNAYOILILIA.  


BASI TUMWOMBE MUNGU ATUPATIE SHAUKU YA KUTAKA KULETA AMANI HAPA DUNIANI, NDIPO TUTAITWA WATOTO WA MUNGU. Hii ni tafakari ya leo toka kwa mtumishi Aba Mpesha.

No comments:

Post a Comment