WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Sunday, February 21, 2016

KESHO YETU IKO MIKONONI MWA NANI?

February 21



Kuna wimbo mmoja wa zamani ambao una maneno haya namjua anayeishikilia kesho na anayeshikilia mikono yangu. Tunatakiwa tujiulize swali moja kama hatuna mamlaka na kesho kwanini bado tunaendelea kupanga kuhusu maisha yetu ya kesho? Mungu ndiye anayeendesha maisha yetu na hatima yetu ya kesho na anajua kesho yetu itakuwaje la msingi sifa na utukufu uwe juu yake

Hata viongozi wa siasa pamoja na jitiada zao za kuongoza nchi bado hawana mamlaka na nguvu ya kuiona au kuishi kesho; mipango yetu yote inaishia leo, hivyo kesho yetu ni kwa kudra ya Mwenyezi Mungu. Hivyo hakuna kiongozi yeyote zaidi ya Mungu ambaye ndiye anayeijua hatima yetu ya kesho.

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa sisi ni wanadamu tunaoishi leo huo ndio ukweli mtupu tupende kuamini au kuwa na kiburi cha kutoamini hivyo.

Mwenyezi mungu anajetoa ahadi kwetu kuhusu kesho; kama mwenjili Mathayo 6:34 anavyosema basi msisumbukie kesho kwa kuwa kesho itaisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake. Au tukisoma kitabu cha Yakobo 4: 13-16 haya basi ninyi msemao leo au kesho tutaingia katika mji Fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida: walakini hamjui yatayo kuwa kesho. Uzima wenu ni ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo kasha kutoweka. Baada ya kusema Bwana akipenda tutakuwa hai na kufanya hivi na hivi. Lakini sasa mwajisifu katika majivuno yenu; kujisisfu kotekwa namna hii ni kubaya.

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa tunatakiwa kumtamamini mungu zaidi katika kila jambo tulifanyalo kwani katika mikono yake ndipo neema yote ya maisha yetu imo. Hivyo ni Mungu tu ambaye anajua na anamiliki kesho yetu; ndio maana hatujui hata mbingu inafanana vipi, kwani kesho yetu imejaa utukufu wa ajabu na amani ya kweli sio kama leo yetu ambayo tunaishi iliyojaa kila aina ya tabu na uozo.

Lakini kesho yetu ili iweze kuwa katika mikono yetu lazima tujijengea tabia ya kuwa na imani dhabiti. Kwani kwa imani tunakuwa na hakika ya mambo ambayo hayaonekani lakini yanatarajiwa nasi. Na kuwa na imani ni kinyume cha kuwa na woga. Je tunawoga kuhusu kesho? Tujikumbushe kuwa kuwa ukiwa mwoga katika maamuzi yako na katika maisha yako ni wazi kuwa huna imani na Mungu hutegemea sana dunia hii.

Tafakari yetu ya leo inatukumbusha kuwa kama hujui kesho yako wewe mwamini Mungu yeye ndio mwenye haki miliki ya kesho. Tuondoe wasiwasi  na kujihakijishia kuwa Mungu atandenda yote kwa ajili yetu; ni muhimi kwetu kutekeleza majukumu yetu nay eye atafany sehemu yake;

Tukumbuke kuwa tunatakiwa kumwamini na kufuata maelekezo ya Mungu ili tuweze fanikiwa ili kuweza kuifikia kesho , na njia pekee ni kwa maombi sala ni salaha pekee ambayo itatufungulia njia ili tuweze ifikia kesho yetu. Tukisoma 1 Wathesalonike 5: 17-18 ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika kristo yesu.

Tafakari yetu ya leo inatukumbusha maneno yaliyoandikwa na Mwenjili Mathayo 6: 33 -34 Basi utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. Basi msisumbuke kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
Hivyo wapendwa hatuna sababu ya kuhofu kuhusu kesho kama tumejikabidhi wenyewe katika mikono ya Mungu. Hatuna sababu ya kuhofu kwani tunajua kuwa Mungu ndio tegemeo letu na yeye peke yake ndio mwenye hati miliki ya  kesho yetu. Amen



No comments:

Post a Comment