WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Sunday, February 14, 2016

ZABURI 133:1: TUWE WAMOJA

February 14 



Tafakari ya leo tunaagalia Tazama! Jinsi ilivyo vyema na jinsi inavyopendeza  Ndugu kukaa pamoja kwa umoja:

Je katika maisha yetu tunafurahia faraja ya kukaa pamoja kama ndugu: iwe ni ndugu wa kuzaliwa au ni ndugu tuliounganishwa na imani kuwa sisi ni wamoja na tumezaliwa ili tuweze saidiana;

Je kwa mwelekeo wa jamii yetu ambayo imetawaliwa na maasi, mauaji, ubakaji, rushwa, na mengine mengi je bado tunanafasi ya kuishi kulingana na Zaburi hii;

Je ni katika wakati gani tunaunganishwa zaidi katika katika umoja huu? Tukumbuke kuwa watu wote upendo mambo mazuri , bila kujali hayo mambo mazuri wanayapataje; ni vyema tukayapata haya mambo mzazuri kama bibilia inavyotufundisha kupitia njia za Mungu kwa kadiri ya mafundisho yake.

Tafakari katika zaburi ya leo ni kuwa inatuhamasisha sisi kujenga umoja na upendo, tunajua kuwa sisi kama binadamu sio viumbe tulio kamilika lakini tusitumie udhaifu wetu katika kuvunja mafundisho na amri za Mungu ili tujipatie maisha mazuri kwa njia ambazo sio sahihi na kuvunja umoja, kuharibu amani ndani ya jamii yetu na kuleta mafarakano kupitia matendo yetu yasiyo faa.

Tukumbuke kuwa umoja wetu uliojengwa juu ya Kristo yesu ni bora kuliko kitu kingine chochote kile. Tukumbuke kuwa Mungu ni Kisima cha Umoja wetu na upendo wetu. Tukitaka kuwa na furaha ya ajabu lazima twende kwake.

Tafakari ya leo kutoka katika hii zaburi inatukumbusha mambo matatu, mosi ni jambo njema wapendwa wanapoishi kwa kupendana na kuwa na kauli moja katika maamuzi, jinsi ya kunagalia mambo katika kutekeleza majukumu ya jumia yao na pale wanapokuwa wote wakifikiri katika mlengo mmoja wenye kheri na ukweli kwa manufaa yao na jamii inayowazunguka.

Pili wanapokuwa pamoja katika upendo wa kweli na sio wa kinafiki japo kiakili kila mtu anaouwezo wa kufikiri toufauti lakini wakakubalia katika upendo maamuzi yao. Ni jambo ambalo tunatakiwa kulitekeleza kila siku katika maisha yetu na hii itatusaidia kuwa na Jamii inayo mpenda na Kumwogopa Mungu kwa kukuaji wake.
Tatu ni Baraka ya pekee kwetu tukiwa wamoja, tukisali, katika kazi zetu, katika mijumuiko ya furaha au tabu kama Mtume Paul 2 Wakorinto 6:1 anavyotukumbusha Nasi tukitenda kazi Pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure. Tunapofanya kazi pamoja hatufanyi peke yetu tunafanya pamoja na Mungu; hivyo ni rahisi katika umoja wetu kupinga dhambi.

Mungu anapenda umoja wetu, ni jambo linamfurahisha sana hasa umoja wenye amani, upendo na ukweli: Mungu huchukia umoja unaoleta mafarakano, matabaka katika jamii. Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa Umoja ni zao jema kwetu hutuletea furaha ya kweli na ustawi wa jamii zetu.

Kwa hiyo Umoja ni kitu kizuri kwa sababu kinatutakatifusha sisi na tunaitwa watu wa Mungu. Umoja ni kitu kizuri kwa sababu kinatuuisha sisi kwani inatupa nafasi ya kutenda mambo yetu kama watu wa Mungu. Umoja ni kitu kizuri kwa sababu ni mapenzi ya Mungu sisi kuwa wamoja


Hii ndi tafakari yetu ya leo Jamii yetu tukiweza kuishi kwa umoja na upendano na ukweli hatutahangaika na matendo yote mabaya yanayokwenda kinyume na mapenzi ya Mungu. Amina

No comments:

Post a Comment