WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, February 12, 2016

TOSHEKENI NA MISHAHARA YENU:



February 12

Tafakari ya leo tufungue mioyo yetu na tusikie "Sauti ya mtu imesikika jangwani: `Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.  Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.  Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."`

"Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?  Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu”.

Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?  Akawajibu, Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo. Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini?  Naye akawaambia, Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa. 

Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?  Naye akawajibu, Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."

Tafakari ya leo natamani kulizungumzia neno hili  Toshekeni na mishahara yenu:

Neno  hili ni zito japo lilizungumzwa kipindi kirefu nyuma lakini tunaendelea kulishuhudia leo tunapowaangalia watendaji wetu katika serikali zetu; Neno hili linatufundisha uadilifu, uwajibikaji kulingana na maadali  na kanuni za kazi ambazo zinatulazimu sisi kama watendaji wa Taifa kuweka mbele matakwa ya Taifa na sio masihahi binafsi;

Najiuliza tena  Neno hili linamaana gani kwa taifa letu? 
Kama nchi na wananchi wake tunahitajii uhuru wa kiuchumi ambao unatokana na viongozi wetu waridhike na mishahara yao; kinyume chake kama hawataridhika na mishahara yoa na kuweka mbele masilahi yao vitendo vya  rushwa na ufisadi ambao unarudisha maendeleo ya Taifa nyuma sana vitadhidi kuendelea.

Tafakari itukumbushe sisi  Kama Taifa na kama Raia na watendaji ambao tumekula kiapo cha utii na maadili bora ya uwajibikaji kwa Taifa letu kuwapa wananchi wanyonge zawadi kubwa ya  uhuru  wa kiuchumi  ni ili kila mmoja wetu aweze kuyafurahia  zawadi pekee rasilimali  ambayo Mungu amelijalia Taifa hakuna atayepingana name kuwa  nchi yetu imefurikakwa  asali na maziwa tazo ni wachache tu ambao wanafaidi kwa kutoridhika na mishahara yao. 

kwa kipindi kirefu tumeona kuwa nchi yetu  Tanzania iliyokuwa ikifurika neema  ya rasilimali sasa imegeuka; kwa wengine imekuwa ni nchi inayofurika machungu; matendo yaleyale ya kifisadi, ya ukandamizaji, ya unyanyasaji ambao  Farao aliwatendea wana wa Israeli huko misri miaka hiyo; lakini kwa kuangalia falsafa hiyo ya matendo ya Farao ndio tunaona Namna watendaji wetu walikokabidhiwa dhamana ndani ya Taifa letu  ambao sio waadilifu wananyatenda sasa yanaenda kinyume na uhuru tuliopewa kama zawadi kuto kwa Mungu ambao kila mmoja anastahili kufurahia na kufaidi asali na maziwa yanayofurika katika nchi hii. Na sio kwa kikundi kidogo cha watu.

Yohane Mbatizaji a usitadhi kabisa anayafafanua makundi yaliyokusanyika uwiano sahihi wa toba. Kulingana na Yohane matajiri wanaotakiwa kuangalia haki ya maskini, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."(Lk 3,11), kwa watoza ushuru waepuke rushwa na matendo ya kifisadi "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."(Lk 3,13) na kwa maaskari wazingatie haki "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo.
Toshekeni na mishahara yenu."(Lk 3,14).

Leo hii ndani ya Taifa vitendo hivi vimeshamiri tena kwa kiasi kikubwa katika jamii yetu, na pengine kila mmoja ameshiriki kwa namna moja au nyingine katika uovu huu, moja kwa moja au kwa kutokuwajibika ipasavyo katika eneo lake la kazi na hivyo kusababisha mianya katika kukua kwa matendo haya maovu. Tafakari ya leo inatuasa  sisi kama Taifa inatupasa tubadilike na kuhakikisha haki na upendo vinashamiri katika jamii yetu.

Kama tutafanikiwa kuishi kwa ujumbe huu wa Yohani Mbatizaji kuwa tutosheke ni mishahara yetu mimi naamini kuwa tukiweka mbele maslahi ya nchi, nchi itasonga mbele. TUKUMBUKE KAULI YA YOHANA MBATIZAJI KWA WALE ASKARI kuhusu dhuluma:
TOSHEKENI NA MISHAHARA YENU, watu wana madaraka makubwa mishahara mikubwa na masurufu manono lakini bado wanaiibia nchi.

Je watendaji wetu wako tayari kutoa hesabu za utendaji wao siku watakapotakiwa na Mwenyezi Mungu tukiamini kuwa kazi zote hutoka kwa Mungu “Sisi tunajielewa kuwa ni watenda kazi wa saa ya kumi-na-moja katika shamba la Bwana la siku za mwisho, na kwamba ingawa mishahara yetu haijulikani  mapema, lakini hatuna mashaka kwa sababu Bwana wetu ni mkarimu”.

Tafakari hii  inatufundisha kitu kingine kipya kuwa tunatakiwa kujihadhari na tabia ya kupenda fedha, na yatupasa toshekeni na vipato tulivyo navyo kwa sababu Mungu mwenyewe alisema,

Tukisoma Ebr 13:5,6 Kwa vyovyote sitakupungukia kabisa, wala sitakutelekeza na kukuacha bila msaada. Kamwe, kamwe, sitakuacha hata kwa kiwango kidogo, kukuacha bila msaada, au kukuacha, au kukuangusha, au kulegeza mkono wangu kwako. Hakika sitafanya hivyo! Kwahiyo tunafarijika na kutiwa moyo, na kwa uhakika na ujasiri twathubutu kusema, ‘Bwana ndiye anisaidiaye.

Kwa kutosheka na mishahara yetu na kwa kuamini kuwa sisi ni wachache ambao tumechaguliwa na Mwenyezi Mungu kuwa saidia wengine ili waweze kupata ridhiki zao; au kufurahia asali na maziwa kwa vipaji vyetu kwa kutimiza wajibu wetu tutakuwa tunatekeleza ujumbe huu wa Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hivi vitu vingine vyote mtapewa kwa maelefu.

Tukitenda kila kitu kwa haki kamwe hatutakosa chochote tunachohitaji unachohitaji ambacho kitakuwa ziada. Mwenyezi Mungu atakupa namna yauta kila uchokihitaji zaidi.

Imani yangu ni kama ile ya Paulo kama tutatosheka na mishahara yetu,na kuwajali wanyonge katika Kupata Riziki
zao, Na Mungu wangu atawajazeni na kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu. Hivyo tunawaomba  watendaji wetu kutosheka na mishahra yao na hivyo kutawapa muda wa kulisaidia Taifa na kuacha kuhangaika na  shughuli binafsi ambazo ziko nje ya maadili ya utumishi wao kwa msingi bora wa kimungu.


"Mungu hatakosa kuwajaza wale wote wanaoifanya kazi yake sawasawa na mapenzi yake" hii ndio tafakari yetu ya leo -amina

No comments:

Post a Comment