WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Monday, February 22, 2016

HERI WENYE MOYO MPOLE




February 22
Leo tuungane na Mtumishi wa Mungu Dr. Aba Mpesha ambaye anatuletea tafakari ya leo tukiwa tunatimiza sikuya 12 ya  Kwaresma: Heri wenye Upole maana hao watairithi nchi (Matayo 5:5)
 Nilipofikiria mstari huu, swali lililonijia ni hili: Nani anaweza kukana haki zake zote kwa ajili ya Yesu Kristo? Nilipochunguza na kutafakari vizuri zaidi, niligundua  upole aliouzungumza Yesu katika mstari huu alimaanisha yafuatayo: 
1.  Mtu akidharauliwa ananyamaza.
2.  Mtu akifanyiwa fujo, anastahimili.
3.  Mtu akikataliwa anakubali.
4.   Mtu ambaye hatashtaki ili apate haki yake.
5.   Mtu asiyepiga kelele akinyimwa haki yake.
Ni yule asiyetaka haki kwa ajili yake mwenyewe, bali anataka haki kwa ajili ya wengine – mara nyingi anataka haki kwa ajili ya wanyonge, walala hoi, wajane, maskini, wasiojiweza, watoto, viwete, na watu kama hao.
 Katika tafakari hii nimejiuliza swali hili:
Je watu ninaokutana nao na wakasikia maneno au kuona matando yangu, wanamwone Yesu?
 Nilisita kutoa jibu kwa sababu upande wangu lilkuwa ni la!
 Ndipo nikamlilia Yesu na nikamwomba, Bwana Yesu niumbie UPOLE ili niweze kuirithi nchi.

Hii ndio tafakari yetu ya leo, Amina

No comments:

Post a Comment