WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Thursday, April 14, 2016

WATU WANGU WANAPOTEA KWA KUKOSA MAARIFA



APRIL 14

 Hosea 4:6

Tafakari ya leo tunaangalia jinsi gani tunavoangamia kwa kukosa maarifa. Je ni maarifa gani hayo ambayo yanatusababisha sisi tuangamie Hosea natukumbusha kuwa Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako. Hii ndio elimu na Maarifa ambayo tunakumbushwa kuwa tumeshindwa kushika na kufuatilia. La msingi tunatakiwa kugundua kuwa tumekuwa tukikosa kujua elimu ya Mungu. Kama vile Mungu kupitia Hosea 4:1,2 aliwambia Lisikieni neno la Bwana, enyi wana wa Israeli; kwa maana Bwana ana mateto nao wakaao katika nchi, kwa sababu hapana kweli, wala fadhili, wala kumjua Mungu katika nchi.  Hapana neno ila kuapa kwa uongo, na kuvunja ahadi, na kuua, na kuiba, na kuzini; huruka mpaka, na damu hugusana na damu.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa kuna uhusiano wa karibu sana kati ya matendo yetu ya na matendo ya kiroho; matendo yetu daima yanatutuma na kutufanya uwajibikaji wetu katika maisha ya kiroho yakiwa yanapungua sana; tunaishia kuwa wabinafsi; tunajiangalia sana wenyewe na tunasahau kabisa nafasi yetu ya kumtumikia Mungu na kukosa kabisa maarifa katika utumishi wa Mungu wetu. Bila kujijua watu wengi tunaishi katika giza na kuvunja amri ambazo Mungu alitaka sisi kuzifuata na kuishi kulingana na amri hizo.

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa maarifa ya Mungu ni ukweli, mara nyingi hatusikilizi ukweli wa maagizo au mafundisho ya Mungu kupitia Bwana wetu Yesu kristo au kupitia mitume au wafuasi wake; matokeo yake ndio kiama chetu au maangamizo yetu kwa kukosa maarifa ya kweli ya ufalme wa Mungu; Matthew 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Tafakari yetu ni kweli watu wengi wanajidai kumtumikia Mungu lakini katika uhalisia hawafanyi hivyo; utawezaje kumtumikia mungu kwa maneno na sio matendo? Utawezaje kumtumikia Mungu wakati hufuati amri zake? Huu ndio ukosekano wa maarifa ambayo yanpelekea watu kufanya matendo ambayo yanapingana na maneno yao, kuua , kuiba, kudhulumu yatima na hata kosa la uzinzi. Kwa vile hatuna maarifa yaliyosahii hatuwezi kutatua shida au matatizo yaliyo mbele yetu matoke yae tunaendelea kuangamia bila wenyewe kujijua. Mungu ametupa sisi maarifa ya kuwa wakweli ili tuweze kutimiza amri au sheria nyingine zote bila kushindwa; lakini kwa vile tumekataa maarifa ya kuwa wakweli sasa tutawezaje  kutatua changamoto za kiroho ambazo ziko mbele yetu.  Matahali 3: 19- 23 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya nchi; Kwa akili zake akazifanya mbingu imara;  Kwa maarifa yake vilindi viligawanyika; Na mawingu yadondoza mande.  Mwanangu, yasiondoke haya machoni pako, Shika hekima kamili na busara.  Basi yatakuwa uzima kwa nafsi yako, Na neema shingoni mwako.  Ndipo utakapokwenda katika njia yako salama, Wala mguu wako hautakwaa. Hiiyote tunatakiwa kuwa na maarifa ya kimungu.

Tafakari yetu bado inatukumbusha kuwa  Mithali 24: 3-4 Nyumba hujengwa kwa hekima, Na kwa ufahamu huthibitika, Na kwa maarifa vyumba vyake hujazwa Vitu vyote vya thamani na vya kupendeza. Ukweli ambao ndio msingi wa maarifa ya Kimungu ni chanzo cha mafanikio yote, ukweli utakufany uwe mnyenyekevu, ukweli utakupa busara; lakini moyo wako ukijaa choyo, wivu, majivuno na unafiki ni wazi kuwa hii ni kithibitisho cha maangamizi. Hivyo ni wajibu wetu kujitathimini kuhusu tafakari hii na kumrudia Mungu na kuomba neema ya maarifa yatokanayo na mungu ambayo ni msingi wote wa upendo, amani, uwajibikaji, huruma kwa wajane na wazee, na tukumbuke kuwa Busara na Hekima hutolewa na Mungu na katika Mdomo wake ndipo maarifa na ufahamu hutolewa; Hekima ya Mungu daima inaingia ndani ya Mioyo yetu na kukaa nasi. Hii ndio tafakari yetu ya leo – Amina

Emmanuel Turuka






No comments:

Post a Comment