WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Monday, April 18, 2016

WEMA NA UZURI WA MUNGU


April 18


Zaburi  27:4.  

Tafakari ya leo tuangalie je ni kitu gani sisi kama binadamu tunakihitaji zaidi kutoka na uzuri wake. Kitu kimoja mimi, wewe na dunia tunahitaji ni kuishi ndani ya Mungu. Kuishi katika uwepo wa mungu katika siku zote zote na kuona uzuri wa mungu kila siku za maisha yetu; kugusa uzuri wa Mungu, kunusa uzuri wa Mungu, kuonya uzuri wa Mungu. Katika ulimwengu wa leo tuko mbio sana na vitu ambavyo mwisho wa siku havina faida kubwa kwetu. Ulimwengu wetu haujetawaliwa na uzuri wa Mungu kwani vita na mapigano ndio vinaendelea kuchuakua uzito na kupoteza uzuri wa Mungu; kwa kweli katika ulimwengu wa leo tunahitaji uzuri wa Mungu ambao ni amani na upendo.

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa kama tunavyohitaji chakula kwa ajili ya miili yetu, hivyo hivyo tunahitaji uzuri wa Mungu katika kurutubisha roho zetu; Mungu daima anatupa sisi uzuri wake ili kuimarisha roho zetu, lakini ni wajibu wetu sisi wenyewe kupokea na kutunza uzuru huo; kwani tukipokea uzuri huu ndio unaoleta nguvu, Baraka na mafanikio ndani yetu. Kupokea ua kuto pokea ni kitu kimoja. Lakini kufurahia na kushukuru ni kitu kingine; hatuwezi kuelezea uzuri wa Mungu sisi wote kwa namna moja ila kila mtu ataelezea kwa namna tofauti kulingana na jinsi alivyogusa, alivyonusa na alivyo onya; kama Zaburi ya 27:4 inavyosema Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake. 

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa Mungu ni ukamilifu wa vyote na mmiliki wa vitu vyote vizuri na sio vibaya . vitu vibaya ni matokeo ya kazi ya mikono yetu sisi binadamu na sio mikono ya Mungu. Vitu vyote vizuri, iwe tabia, utendaji wa kazi, maadili mema, uwajibikaji malezi ya vijana yenye maadili mema, ndoa zilizo bora ni kazi ya matunda ya uzuri wa Mungu.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa Mungu hayuko ili awe sehemu ya kichwa chako kama hiyo ingekuwa hivyo basi kulikuwa hakuna sababu ya yeye kukujua wewe; kwa sababu wewe pia ungemjua Mungu zaidi na mipango yake yote; Mungu ni mkubwa zidi yetu na ufahamu wetu, yeye ndiye mwanzo na mwisho, mjengaji na mbomoaji wa jambo lolote line ambalo analiona linakwenda kinyume na taratibu zetu; mungu lazima awe hivyo ili tuweze kuona na kufurahia uzuri wake; jukumu letu ni kuendelea kujifunza kuhusu Mungu na kuendelea kumpenda kwa akili zetu zote ambazo ni zao la wema wake kwetu.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa wema na uzuri wa Mungu ni zao la Limungu. Sio kila kitu tukifanyacho hapa dunia ni kizuri na kinaakisi wema wa mungu bali lazima kipate kionyo cha kimungu; maadili ya kimungu; tukizingatia kuwa Mungu yeye mwenyewe ni mkamilifu katika nyanya zote; la msingi tumepewa nafasi pamoja na mapungufu yetu ambayo yanaharibu wema na uzuri wa mungu katika maisha yetu; yatupasa bado kumpelekea Mungu Masanduku yetu ya ubaya wetu ili tuombe msamaha kwa ni yeye kwa wema na uziri wake bado amejawa na huruma na atatusamehe ili yuweze furahia uzuri wake; mungu daima anataka kutufanya sisi kuwa sehemu ya uzuri wake kwa kutusafisha na kutusamehe dhambi zetu.

Hii ndio tafkari yetu ya leo Amina


Emmanuel Turuka

No comments:

Post a Comment