WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Sunday, April 17, 2016

MAOMBI MAZITO AMBAYO YESU ALIFANYA JUU YETU KWA BABA


APRIL 17

zaburi ya 37: 4

Tafakari ya leo tuangalie na tuzingatie maombi mazito ambayo Yesu alituombea kwa Mungu ili nasi tuweze kuwa na uzima wa milele; utumishi wake hapa dunia ulikuwa kwa ajili ya ukombozi wetu japo hatutaka kukombolewa naye; Alipingwa kila kona hasa na wale ambao walijiona kuwa wao wanafahamu zaidi kuhusu sheria na kanunu kulingana na mafundisha ya mapokeo; pamaja na kukataliwa bado alitupenda na hata kutusamehe kwa mara nyingine alipokuwa anakufa msalabani;

Kwa pamoja tuitafakari hii sala ya Yesu kutoka katika kitabu cha Yohana 17-1-26 Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; 
kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele. 
Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. 
Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye. 
Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako. 
Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika. 
Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako. 
Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. 
Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako; 
10 na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao. 
11 Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. 
12 Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie. 
13 Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao. 
14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu. 
15 Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu. 
16 Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu. 
17 Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli. 
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni. 
19 Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli. 
20 Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao. 
21 Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. 
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. 
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi. 
24 Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu. 
25 Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma. 
26 Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.

Hivyo Tafakari tukisoma pia Waebrania 12:2 inatukumbusha kuwa tunatakiwa kumtaza Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. kwa hiyo ni wajibu wetu ili kuweza kupata na kufurahia haja za mioyo yetu. Hii ni Tafakari ya leo Amina

Emmanuel Turuka


No comments:

Post a Comment