WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, April 1, 2016

NI WAJIBU WETU KUWAPENDA WAKE ZETU



April 1
Ephesians 5:23-27
Tafakari ya leo tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutujalia kuwa na familia bora na imara kwa kutajalia mke mwema. Bibilia kupitia Mithali 19: 14 Mke mwema hutoka kwa BWANA; Kwa fundisho hili la bibilia inatukumbusha  kuwa Mungu pekee ndiye mwasisi wa ndoa ni; tukumbuke alivyomwambaia Adam na Hawa  zaeni mkaongezeke, mkaijaze nchi na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi. Kwa maelekezo ya Mungu katika uumbaji wake tunakubaliana kuwa mwanaume na mwanamke ni nguzo mbili za msingi wa familia, lakini kwa kuwa wanaume wamepewa sifa maalum kwa amri ya uumbaji, na kwa sababu ya uwezo wao wa mantiki ni imara zaidi ya ule wa wanawake, wao huchukuliwa kama walezi wa familia zao na vichwa vya familia. tukisoma 1 Wakorintho 11:3 Lakini napenda muelewe kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, kama vile mume alivyo kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo. Waefeso 5:23 Kwa maana mume ni kichwa cha mke kama vile Kristo alivyo kichwa cha kanisa, ambalo ni mwili wake, naye mwe nyewe ni Mwokozi wa kanisa. Ikumbukwe huyu ndiye ana uamuzi wa mwisho katika familia akiamua kuukana ukristo, kurudi nyuma inakuwa na athari kubwa sana katika familia. Hivyo hii ndio nguzo ya ndoa ya Kikristo.

Tafakari yetu ya leo msisitizo wetu uko katika wajibu wa wanaume kwa wake zetu; Ni mwanaume ambaye kwa kutumia busara yake, anaweza kuisadia familia yake na kutayarisha mazingira kwa ajili ya furaha yao, na ni yeye ambaye anayeweza kuigeuza nyumba kuwa Pepo na mke wake kuwa kama Malaika. Busara ya mwananume ni tuzo kubwa katika malezi ya familia;Mwanaume ambaye anaisaidia familia yake, lazima atambue kwamba mwanamke pia ni binadamu kama mwanaume. Siri ya ustawi wa familia inategemea na jinsi mtu anavyomtunza mke wake, na hii ni kama ilivyowajibu wa mke kwa mume wake ambao unaeleweka kuwa katika kiwango sawa na Jihadi, pia unatambua kama tendo jema na lenye thamani sana. Lakini mwanaume ajifunze namna ya kumshughulisha mke wake, katika namna ambayo atageuka kuwa na tabia kama Malaika.

Leo tunakumbushwa kuwa mwanaume lazima atafiti kuhusu tabia na matakwa ya mke wake. Lazima apange maisha yake kufuatana na matakwa ya mke wake na mahitaji sahihi. Mwanaume anaweza kwa tabia na msimamo wake kumshawishi mke wake katika njia ile ambayo inampendeza yeye (mke wake), kwake yeye mume na nyumba yake. Kama tunavyokumbushwa kutoka katika waraka wa Waefeso 5:33 Hata hivyo kila mmoja wenu ampende mkewe kama anavyoipenda nafsi yake. Upendo ni nguzo ya Pili na pia ni moja ya tunda la Roho katika ndoa.

Tafakari yetu inawauliza wanaume kama wanajua kuwa mwanamke amejaa wema na ni kiumbe chenye hisia kubwa sana ya upendo na utunzaji wa nyumba? Tunatakiwa tukumbuke kuwa furaha yake hutegemea huruma na upendo wa mume wake. Tukiwapenda wake zetu kwa upendo halisi ndivyo wanavyofurahi zaidi. Kwa hiyo siri ya mwanamume aliyefuzu katika maisha ya furaha ya ndoa ni jinsi anavyo onesha mapenzi kwa mke wake. 1 Wakorintho 13:4-8 Upendo huvumilia, upendo hufadhili; upendo hauna wivu au majivuno. Hili ndilo jukumu letu katika kuwapenda wake zetu na hatuwezi kulikwepa jukumu hili muhimu ili kukamilisha familia iliyo bora. Tukumbuke kuwa tusipokuwa mwema kwa wake zetu, basi anaweza kupoteza mvuto kwenye nyumba zetu, halikadhalika na watoto pia. Na zaidi ya yote kwako wewe mwenyewe. Wakati wote nyumba zetu zitakuwa katika hali machafuko. Mwanamke hubadilika haraka na hatakuwa tayari kufanya juhudi kwa ajili ya mtu asiyempenda.

Tafakari ya leo inatushauri akina baba kutumia mazuri yaliyo jaa sifa na hisia kwa wake zetu tukumbuke kuwa  maneno mazuri na matamu ya kuwasifia wake zetu kamwe hayaondoki kamwe hayaondoki moyoni mwao. Kama mambo yalivyo, mapenzi na huba lazima yawe halisi na kuvutia kwenye moyo wa mwingine, lakini hata kupenda sana kwa mtu haitoshi, kwa kuwa ni muhimu kuonesha huba. Kwa kuonesha hisia zako kwa maneno na vitendo vyako, mapenzi unayoonesha, yatapata jibu zuri kutoka kwa mkeo na nyoyo zenu zitaimarisha muungano wa mapenzi. Uwe wazi na udhihirishe mapenzi yako kwako bila kusita. Wakati yupo au hayupo, msifie. Mwandikie barua unapokuwa safarini na mtaarifu kwamba kutokuwa karibu naye unajihisi mpweke sana. Mara kwa mara mnunulie kitu kama zawadi. Mpigie simu unapokuwa ofisini au shughuli zako na umuulize hali yake. Wake zetu wanafurahi tunapowapa heshima iliyojaa upendo Heshima humfanya mtu ajione unamjali, wanaume wengine atasema anapenda lakini anamwita mwenzie hajasoma, ametoka familia duni, hafanani na hali yangu, kwakweli huku ni kumdhalilisha mwenzio 1 Petro 3: 7 – 9 7Kadhalika ninyi waume, ishini na wake zenu kwa kuwahurumia, mkitambua ya kuwa wao ni dhaifu na hivyo muwape heshima, kwa maana ninyi ni warithi pamoja nao wa neema ya uzima.
Tafakari yetu ni msingi mkubwa sana wa familia bora, jamii bora ni matokeo ya familia bora itokanayo na usimamizi mzuri wa Mume; Marko 10:7 Na kwa sababu hii mume atamwacha baba yake na mama yake na hao wawili, watakuwa mwili mmoja. Hivyo nyumba yenu itakuwa msingi wa maisha bora; ijae msamaha tukumbuke kuwa hapana mtu yeyote hapa duniani ambaye anazo sifa zote na hana makosa. Kwa ufupi, hakuna mtu ambaye hana mapungufu, na hakuna mtu yeyote hapa duniani anayeweza kuchukuliwa kama kiumbe kilichokamilika. Kwa kawaida, wanaume, kabla ya kuoa hudhani kwamba atakaye muoa awe hana dosari yoyote. Hawajali ukweli huu kwamba hakuna kiumbe kifananacho na malaika hapa ulimwenguni. Wanaume hawa, mara waoapo huwaona wake zao waliodhani wakamilifu, si wakamilifu na hivyo huanza kuonesha mapungufu yao. Hudiriki kuona kuwa ndoa zao hazikufuzu na wao wenyewe kuwa na ‘bahati mbaya.’

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa tuishi katika msamaha wa kweli tusamehe na kusahau, kwa kufanya hivyo tutakuwa tunatimiza  maandiko 1 Wakorintho 13:4-8 5 Upendo hauna kiburi na haukosi kuwa na adabu. Upendo hautafuti kujipendeza nafsi; haukasiriki upesi, hauweki orodha ya mabaya. Bali tutajenga nyumba iliyo bora lakini msingi wote wa Nyumba bora Amepewa mwanaume kuusimamia na kuufanikisha. Wanaume tunajukumu kubwa na la msingi mkubwa san asana.

Hii ndio tafakari yetu ya leo – Amina

Emmanuel Turuka







No comments:

Post a Comment