WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Wednesday, April 6, 2016

FAIDA YA UVUMILIVU KATIKA MAISHA YETU YA KIROHO NA KATIKA JUMUIA ZETU


APRIL 6

Wafilipi 2:4-8

Kwa haraka haraka tu Uvumilivu ni uwezo wa, au ni mazoezi ya, kutambua na kuheshimu imani au matendo ya wengine; uvumilivu uko katika kila nyanya ya maisha yetu, kuanzia maisha yetu ya kila siku; TATIZO katika maisha ya kawaida sana, swala la uvumilivu halizungumzwi sana, tunachokiona sana ni mazungumzo ya kulipa kisasi;Nafikiri itakuwa jambo njema kama tutaendelea kufundisha na kuhubiri uvumilivu katika nyanya zote. Pengine fujo hizi ambazo taifa linaendelea kujionea zikizidi kujitokeza zingeweza kukoma au kupungua

Hii inatokana na kukosekana mambo makubwa matatu ambayo ni ufahamu au maarifa, hekima na  hasa uvumilivu. Kiongozi asiye mvumilivu anaweza kujikuta anatumia mabavu kutawala ili watu wajue kuwa yupo, ana nguvu na ana mamlaka. Na hii falfasa ambayo huangukia kwa wananchi vile vile pale ambapo wanakuwa hawana uvumilivu; Bibilia inatuonyesha mfano mzuri wa bwana wetu yesu ambaye pamoja na ukuu wake alijishua na kuvumilia yote na kuwatumikia wote bila makuu: wafilipi 2:4-8 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;  bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;  tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. 

Tafakari yetu leo inatufundisha kuwa ni ukweli ulio wazi kuwa  kiongozi anatakiwa kuwa, mtulivu, mvumilivu na anayetumia zaidi hekima kuliko mabavu, kiongozi anatakiwa Kuwa na  msimamo wa uvumilivu ni moja ya kazi ngumu zaidi miongoni mwa viongozi dhidi ya wananchi katika jamii. Ni ukweli ambao haufichiki kuwa viongozi hawakuzaliwa wakiwa wavumilivu, lakini lazima tujifunze kuwa wavumilivu. Na hii ni kweli hata kwa jamii inatupasa kuvumiliana na kumaliza tofauti zetu kwa busara ya majadiliano.

Tafakari yeru tunaangalia hata katika siasa uvumilivu wa kisiasa unakuza  utamaduni wa utawala bora na ukomavu wa demokrasia; na Kwa demokrasia kufanya kazi vizuri, wananchi lazima kuwa tayari kuvumilia na kuvumiliana. Tukumbuke kuwa dhana ya uvumilivu ni ya msingi sana kwa maendeleo kwani inaruhusu mawazo mapya ndani ya jamii; kupitia dhana hii ya uvumilivu, kiongozi anakuwa  tayari kukubali  na kuheshimu  maoni na mawazo ya watu wengine na haki zao kwa uwazi na uhuru. Katika hali hii,uvumilivu huruhusu kuwepo kwa vyombo  huru vya habari kutumika kama chombo muhimu kuwahabarisha wananchi na kuwasilisha madai yao kwa viongozi wao.

Tukumbuke kuwa demokrasia inahitaji vyombo vya habari ambavyo hugeuka kuwa daraja la mawazo kati ya viongozi na waongozwa. Vyombo huru vya habari husaidia   wananchi kuelewa taratibu ambazo zinaimarisha demokrasia.uvumilivu wa viongozi huru utasaidia kueneza demokrasia  na uwajibikaji kwani wananchi wataweza kukosoa serikali na ujumbe kufikishwa serikalini bila kuogopa.

Tafakari yetu leo inatuonyesha ukweli kuwa Falsafa ya Uvumilivu hufunza na kuwakumbusha viongozi na wananchi wake kuwa wanatakiwa kuishi kulingana na fikira njema. Mwenye kuifuata falsafa ya uvumilivu hayuko tayari kuamsha fikra mbaya za uvunjajiwa amani bali daima atajitaidi kuziepusha kwa kuendeleza uamuzi  wa uwazi na kwa kutumia njia  ya utulivu wa hekima kupitia uzoefu makini wa kimantiki: Kiongozi mwenye uvumilivu daima hutafakari, na kuziweka fikira mahali pamoja kabla ya kufanya uamauzi.Msingi wa kimaadili wa falsafa ya uvumilivu  kama mtaalam mmoja alivyo wahi kusema kuwa kwa ufupi tunaweza kusema kuwa uvumilivu umesheheni nini?

Tafakari yetu inalenga kurunzi kwa sisi wananchi wa Tanzania bado tuna kila sababu ya kuendelea kuenzi na kuthamini uvumilivu miongoni mwetu; uvumilivu kati ya wananchi wa dini tofauti, kusikilizana na kushauriana kwa faida ya taifa letu; tukiweza kuutumia uvumilivu katika kiwango cha juu tutafanikiwa kuondoa chuki ambayo inaanza kueneakatika taifa letu; Ni kweli kama tutaweza kuwaweka wenzetu mbele katika maisha yetu ya kila siku na kuwa tayari kushirikiana nao tutakuwa tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutekeleza injili hii ya uvumilivu.

Hii ndio tafakari yetu ya Leo; Amina

Emmanuel Turuka



No comments:

Post a Comment