WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Thursday, March 17, 2016

JE SISI TUNAISHI KAMA TAI?



March 17

1 Wathesalonike 5:11


Tafakari ya leo tukiwa bado  tunaendelea na mfungo wa Kwaresima tunatakiwa tuishi kama Tai; Tai ni Ndege ambaye anaweza kuruka juu kuliko ndege wengine wote na kwa kasi ya ajabu sana. Tai ni ndege ambao wanaruka pamoja bila kubaguana kwa upendo mkubwa;  Tai anaona umbali mara saba zaidi ya jinsi anavyoona binadamu. Tai anaouwezo wa kuona chakula kama vile samaki, kisha hulenga shabaa toka mbali na kumpata mlengwa. Tai ni ndege mwenye nguvu kuliko ndege wengine. Tai makazi yake yako juu ya miti mirefu sana kuliko ndege wengine. Je sisi kama wakristo maisha yetu ya Kumtumikia Mungu yanalingana na mwenendo huu wa Tai wa kujiamini?

Tafakari ya leo inaendelea kutufundisha kuwa tukiweza kutumia jicho la Tai katika maisha yetu tuishi kwa kufikiria mambo ya badae tunatakiwa tuwe kama Tai tuwe wa moja katika kumtumikia Mungu kama 1 Wathesalonike 5:11 Basifarajianeni na Kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya. Ni ujumbe mzito amba Tai wanaufanya pamoja katika maisha yao kama ndege. Hapa tunatakiwa kwanza ni kuithamini nafsi yako  na kuisikiliza sauti kubwa itokayo moyoni mwako,ikuongozae juu ya kutenda,hii ni sauti ya Mungu iletayo mafanikio,furaha na kila lililo jema.Sauti hii inakupa nguvu ya kutenda miujiza kila wakati,ndiyo inayofanya nuru ya maisha yako ing'ae. Lazima ujikubali kwa kuwa mimi ni zaidi ya nilivyo.Ukiachilia mbali mazingira ninayoishi na sura yangu,mimi ni wa thamani,kama wengine. Wewe ni wa thamani jinsi ulivyo,na thamani yako ni sawa na binadamu wote.Unao uwezo wa kuwa na kuishi maisha ya furaha na mafanikio. Unastahili, wewe ni Matokeo ya kazi kubwa ya Mungu. Tunatakiwa kuanza kujikubali na kuepuka misukumo ya wale wanaokuzunguka. Anza kutazama uwezo ulio nao,tazama chemchem ya mafanikio iliyopo ndani mwako.Sisi sote ni bora .Sisi wote ni wamoja. Huu ni wakati wa kujifunza kuwa wewe, kujikubali, kukua na kubadilika. Anzakujitambua wewe kisha utatambulika kwa wengine. Kama vile Tai walivyojitambua kuwa wao ni ndege bora na wanaweza kruka juu kabisa kuliko ndege mwingine yeyote.


Tafakari ya leo inataka sisi tuvumbue uwezo ulionao.Tumia uwezo tulionao kupaa  juu ya mipaka unayofikiri ipo katika kuutafuta ufalme wa Mungu. Fanya yale unayoyakusudia maishani na uwe vile unavyotaraji kuwa. Umezaliwa kuwa kiongozi wa maisha yako na kuyatawala mazingira yako ili kuufikia uzima wa milele.Unaweza kupaa juu zaidi na zaidi pasipo kudondoka. Vikwazo vijitokezavyo dhana ya kifikra tu. Hatupaswi kuruhusu kuruhusu fikra za wanaokutuzunguka zitufanye tuwe na mawazo mgando ama yenye mipaka na kutuletea mashaka katika safari yetu ya mbinguni. Huwezi kuruka juu kama tutabaki na fikra kama za kuku na kuendelea kukwaruza na kudonoa tu. Amua sasa kuruka juu ili kumtumikia Mungu.


Tunataadharishwa kuwa lazima tuwe kama Tai kuwa na maono na nguvu ya kuamua, ili waweze kutambua na kufanikiwa katika mawindo yetu na kufanikiwa kupata kila kutitakacho; Wakati huo huo, tai unaweza kuona adui zake kutoka mbali, kama vile nyoka amabao anajaribu kuvamia kiota chake ili aweze kuiba mayai yake au kuua vijana wake. Ingawa tai kujenga viota vyao kwenye miamba ya juu na maeneo, nyoka kuwa na tabia na uwezo wa kupanda kwao. Lakini maono kali ya tai yanaamsaidia kuona maadui kutoka mbali na kiota chake. Tukisoma Warumi 14:17 maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furahakatika roho Mtakatifu.

Sisi kama watoto wa Mungu ni lazima kuzingatia malipo mambo mazuri ya amani, furaha, na haki. Tukumbuke kuwa lazima tujiandae kwa nguvu zote tukijua kuwa shetani na wafuasi wake wana uwezo wa kushambulia kiota chetu, ambayo ni Familia yetu, fedha, mahusiano, afya, ustawi wa kiroho, Wakati ulimwengu mapepo ya enzi, mamlaka, na wakuu wa giza hili ambao ni kujaribu kuiba, kuua na kuharibu maisha yetu tele ya Mungu ndani ya familia zetu, wapendwa, na jamii yetu, tunaona ni kutoka mbali na mtizamo na maono nguvu ya Mungu na kuanza kupinga hilo kwa kushambulia yake. adui ambaye anajaribu kuja katika kuwa na hofu na kukimbia mbali 1 Peter 5:8 Muwe na Kiasi na kukesha kwa kuwa mshitaki wenu ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka zunguka, akitafuta mtu ammeze. Hivyo tunatakiwa tuwe na nguvu za kushindana na adui kama Tai afanyavyo. Tunatakiwa kuendelea kuomba bila kuchoka; ili kwa neema ya Mungu tuendele kupata faraja kubwa sana.


Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa ushindi wetu uko juu ya Mwili na damu ya Bwana wetu Yesu Kristo; Yohana 6: 55-57 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli , na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye Mimi wataishi kwa sababu yangu. Maana yake ni  nini? Sisi , waumini , ni mmoja ambaye kula nyama safi ya maneno ya Yesu kutoka mbinguni kupitia mafundisho Roho Mtakatifu , ambayo daima kutufanya kuishi maisha yake hapa duniani kifalme kama vile tulivyopasa tuishi mbinguni; 1 Kor 2:13 Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho,tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni.


Tafakari ya leo inatufundisha kuwa Tai ni ndege wanaopenda sana  kuwa tayari wakati wa  dhoruba.Tunafahamu kuwa ndege wengine wote hujaribu kuto ruka wakati wa dhoruba na kujificha kwenye viota vyao au mapango yao kwa ukali  wa upepo, Lakini tai hupenda  kuruka  wakati huo kwa kutumia upepo wa dhoruba ili waweze kuruka juu zaidi kwa muda mfupi. Tai ni wanjanja kwani wanjua kwa kutumia upendo wa dhoruba wataruka juu dhaidi bila kutumia nguvu yao watakuwa wanaelea tu na kusukumwa na upepo huo. Katika maisha yetu ya kila siku tunakutana na dhoruba nyingi katika maisha yetu kama shida mbalimbali, majonzi, na majaribu malimbali; tukisoma Yohana 16:33 Haya nimewaambieni mpate kuwa naamani ndani yenu. Ulimwengu mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu. Au Kitabu cha Yakobo1:12 Heri mtu astahimiliye maajaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa atalipokea taji la uzima. Bwana alivyowaahidi wampendao. Lakini tukumbuke kuwa tunatakiwa kuhesabu furaha tupu tukiangukia katika majaribu mbalimbali, mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa chochote.

James 1: 2-4. Tukumbuke jini Mungu alivyomjaribu Ibrahimu kabla ya yeye kuaminiwa kwake kama rafiki yake mpendwa kwa milele

Tulio wengi tukijaribiwa kidogo tu; tunalalamika sana na kukata tamaa baadhi yetu tunakuwa kama Waisraeli walivyokuwa wakimlalamikia Mungu alipowatoa katika nchi ya Mateso Misri; tukumbuke kuwa Mungu anahitaji kutu pima kwa sababu sisi sio viumbe kamili bali tunahitaji kusafishwa kupitia majaribu mbalimbali, na mateso ili tupate kuwa wakamilifu; na mara baada yamajaribu, Mungu hutuimarisha sisi kwa milele yeto; 1 Petro 5: 10 Na mungu wa neema yote aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milelekatika kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yey mwenyewe atawatengeneza na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.

Je sisi ni kama tai ambao daima kujenga viota vyao katika mahali pa juu ambapo adui hawezi kufikia kwa urahisi? Mungu siku zote ana nguvu za kutuinua sisi juu lakini yatupasa kuwa Wanyenyekevu, masikini wa roho,tuwe wapole na tuwe rehema ya Mungu; Tukumbuke kuwa kama tai anavyowapenda watoto wake: Mungu alitupenda sisi zaidi, kwani ni upendo gani mkubwa wa kumtuma Mwana wake wa pekee kuja dunia kuishi nasi na kasha kufa katika kifo cha aibu msalabani ili nasi tuweze kingia katika ufalme wa mbinguni;



Tunafunga Tafakari yetu ya leo kuwa kwa kutilia mkazo jambo kuwa kama ilivyo kwa tai katika anga inawakilisha siri ya Mkristo ambaye amejifunza na kuwa tayari kumpigania Mungu katika khali yeyote ile katika ulimwengu wa roho, tunafahamu kuwa tupo kwenye changamoto nyingi kama upepo wa mashaka na dhoruba za maisha bali tunatakiwa kutegemea zaidi msaada wa Mungu. Hivyo tukiweza kumtegemea Mungu yeye atatufanya sisi tuweze kupaa juu zaidi na kuelee katika dhoruma yeyote ile bila shaka lolote.

Tunatakiwa kuwa kama Tai ili tuweze kuweza kufurahia maisha utakatifu, ni moja ya siri kubwa ya imani. Tunatakiwa kutenda kama Yesu na kuishi maisha ya mkristo kwa uadilifu mkuu na  ili tuweze kushinda maisha ya ufalme wa mbinguni.  Tunatakiwa tuwe, si jogoo wala kuku .

Hii ndio tafakari yetu ya leo



Emmanuel Turuka

No comments:

Post a Comment