WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Thursday, June 2, 2016

KWA NINI MAFUNDISHO YA YESU YALIVUTA WATU WENGI

June 2


Tafakari ya leo tunaangalia kwa nini mafundisho ya yesu yaliweza kuvuta watu wengi na amekuwa na wafuasi wengi hata baada ya kupaa kwake na kurudi kwa baba Mbinguni; tunaangalia kuwa injili yote ambayo inaendelea kufundishwa leo ni mafundisho ya Yesu kwa wafuasi na waamini wake; alifahamika kwa wengi kuwa yey alikuwa ni Rabi yaani mwalimu. Tunajua kuwa Yesu alikuwa akifundisha kwa maalaka ambayo hata pale alipokuwa akisisitiza jambo daima alikwenda mbali zaidi ili wafuasi wake waweze kuelewa na kuishi kulingana na mafundisho yake; Injili inaonyesha maisha ya yesu alivyoishi hapa dunia huku akiwa akitimiza kazi ambayo alitumwa kuja kuimamilisha ya wakovu wetu sisiwanadamu. 

Tukiangalia mafundisho ya Bibilia tunaona kuwa kulikuwa na kila aina ya watu ambao walikuwa wakimsikiliza kila wakati alipokuwa akihubiri. Kulikuwa na wataalamu wa sheria, walimu wa masinagogi, na watu wa kawaida. Na tukifuatilia sana mafundisho yake Yesu alikuwa akifundisha katika mtazamo tofauti alipokuwa akiongea na watu wa kawaida na pale alipokuwa akiongea na wataalamu wa sheria vile vile mafundisho yake yalikuwa yakibadilika.

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa sio tu alikuwa mwalimu bora lakini alikuwa pia akiwaandaa wale mitume kumi na wawili ili pindi yeye atakaporudi kwa baba waweze kufanya kazi hii ya ukombozi kwa nguvu ile ile. Mafundisho yake yalikuwa yamejaa zaidi mifano ambayo ilikuwa inawasaidia sana wafuasi wake kulelewa nini alikuwa akifundisha na kuwawezesha kufuata kwa urahisi zaidi; na alikuwa akitumia mifano ambayo ilikuwa rahisi sana kueleweka kwa mtu yeyote Yule; alikuwa akitumia mifano ya kawaida ambayo iko katika maisha ya watu ya kila siku; mifano ya vitu kama mwanga; mlango; zabibu; mchungaji; ni mifano ya kawaida ambayo ilikuwa ikipatikana katika maisha ya jamii husika na ilikuwa ikieleweka kwao kwa haraka na kwa urahisi zaidi;

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa ili tuweze kutimiza wajibu wetu vizuri katika maisha yetu ya kila siku lazima Yesu kupitia mafundisho yake anatukumbusha kuwa tunatakiwa kuwa watu wa furaha daima tukionyesha tabasamu wakati wote wa utumishi wetu  na kuongea katika lugha na misemo ambayo ni rahisi kueleweka kwa kila mtu kulingana na mizingira ambayo wapo; tukisoma Injili ya Mathayo 10:16 Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua. Yesu aliwapa maelekezo mitume wake ya kufanya kazi ngumu lakini wawe na busara ya khali ya Juu na kuwaelimisha kwa mifano ya vitu vitokanavyo na mazingira yao;

Tafakari yetu inaendelea kutoa mafundisho ya Yesu tukisoma Injili ya Marko 4:34 wala pasipo mfano hakusema nao; lakini akawaeleza wanafunzi wake mwenyewe mambo yote kwa faragha. Mafundisho yake kwa mifano daima yaliweza kuwaunganisha wafuasi wake kwa haraka zaidi na katika uelewa mpana. Mfano hadithi ya Mototo mpotevu fundisho ambalo liko kwetu sote kupitia hadithi hii ni kuwa jinsi mungu anavyotupenda hata kama tutakuwa tumemkosea vipi kama tu kwa dhati kabisa tutakiri udhaifu na makosa yetu yeye atatupokea na kutufanyia karamu kubwa. Huu ulikuwa ni mfano wa kawaida katika maisha ya kila siku.

Tafakari yetu leo inatukumbusha pia kuwa Yesu pia alikuwa akifundisha huku akitoa kauli za kutisha ili kuwaleta karibu wafuasi wake wawe na woga wa kuogopa na kutenda mema; tukisoma Mathayo 5: 29-30 Jicho lako la kuume likikukosesha, ling'oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.  Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum. 

Au tukisoma pia Mathayo 7:3-5 Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii? Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?  Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako. Hizi ni baadhi tu ya mifano ambayo ilikuwa inawagusa watu na wanaogopa na kuupokea ujumbe vile ambavyo yesu alitamani uwafikie kwa haraka na kwa ubora wake ili kila mtu aweze kuishi maisha yaliyo bora; hivyo kama nasi tunatamani kuhubiri mafundisho yetu kama Yesu alivyo fanya lazima tuwatishe watu ili washituke na kuamaka;

Tafakari yetu inatuhimiza kuwa Yesu alikuwa akifundisha kwa semi fupi fupi ambazo zilikuwa ni rahisi kwa wafuasi wake kukumbuka na kuweza kuzifuata kama vile alivyokuwa akifundisha tukisoma Injili ya Luka 6: 36-38  Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.  Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.  Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa. Na mfano mwingine ambao ni Mzuri ambao Yesu aliutumia alipokuwa akihubiri ilikuwa sheria ya dhahabu Luka 6:29-31 Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang'anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.  Mpe kila akuombaye, na akunyang'anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.  Na kama mnavyotaka watu wawatendee ninyi, watendeeni vivyo hivyo. Alikuwa daima akifundisha kwa ufupi lakini maneno yake yalijaa hekima na busara na ni rahisi kuyashika na kuafuata.

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa Yesu alikuwa akitumia mbini nyingi ili kuhakikisha kuwa wafuasi wake wanaelewa mafundisho yake na kutekeleza kile ambacho alikuwa anatamani wao wafuate ili waweze kupata wokovu; alifundisha kwa kuuliza maswali kila alipokuwa akifundisha; Mathayo 16:26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?  Mathayo 22: 20-21 Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii, na anwani hii?   Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu. Alikuwa anatumia vile mtindo kurudia rudia akijua kuwa kuna wakati mwingine wafuasi wake wasikie jambo hilo mara kwa mara; ama kuhusu kifo chake na ufufuo wake; 

Marko 8:31 Akaanza kuwafundisha kwamba imempasa Mwana wa Adamu kupatikana na mateso mengi, na kukataliwa na wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na baada ya siku tatu kufufuka. Marko 9:31 Kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake, akawaambia, Mwana wa Adamu yuaenda kutiwa katika mikono ya watu, nao watamwua; hata akiisha kuuawa, baada ya siku tatu atafufuka. Marko 10: 33-34  akisema, Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi, nao watamhukumu afe, watamtia mikononi mwa Mataifa,  nao watamdhihaki, na kumtemea mate, na kumpiga mijeledi, na kumwua; na baada ya siku tatu atafufuka. 

Hii ndio tafakari ya leo – Amina

Emmanuel Turuka

 

 

 




No comments:

Post a Comment