WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, January 29, 2016

TUANGALIE DHANA YA KUVUMILIANA



January 29:

Tafakari ya leo hebu tuangalia dhana ya uvumilivu tukisoma Luka 9;52-56, akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha wasamaria, ili kumtengenezea mahali; lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyoulekeza uso wake kwenda Yerusalemu. Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo walisema Bwana wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni uwaangamize: kama Eliya naye alivyofanya?

Yesu akawageukia akawakanya Akasemahamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo; kwa maana mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa.

Ni ukweli ulio wazi kuwa  kiongozi anatakiwa kuwa, mtulivu, mvumilivu na anayetumia zaidi hekima kuliko mabavu kama Yesu alivyowaambia wnafunzi wake.

kiongozi anatakiwa Kuwa na  msimamo wa uvumilivu ni moja ya kazi ngumu zaidi miongoni mwa viongozi dhidi ya wananchi katika jamii. Ni ukweli ambao haufichiki kuwa  viongozi hawakuzaliwa wakiwa wavumilivu, lakini lazima tujifunze kuwa wavumilivu. Na hii ni kweli hata kwa jamii inatupasa kuvumiliana na kumaliza tofauti zetu kwa busara ya majadiliano.

Katika siasa uvumilivu wa kisiasa unakuza  utamaduni wa utawala bora na ukomavu wa demokrasia; na Kwa demokrasia kufanya kazi vizuri, wananchi lazima kuwa tayari kuvumilia na kuvumiliana.
Dhana ya uvumilivu ni ya msingi sana kwa maendeleo kwani inaruhusu mawazo mapya ndani ya jamii; kupitia dhana hii ya uvumilivu, kiongozi anakuwa  tayari kukubali  na kuheshimu  maoni na mawazo ya watu wengine na haki zao kwa uwazi na uhuru. Katika hali hii,uvumilivu huruhusu kuwepo kwa vyombo huru vya habari kutumika kama chombo muhimu kuwahabarisha wananchi na kuwasilisha madai yao kwa viongozi wao.

Tafakari ya leo unatujenga katika upana wa kuelewa dhan ya demokrasia inahitaji vyombo vya habari ambavyo hugeuka kuwa daraja la mawazo kati ya viongozi na waongozwa. Vyombo huru vya habari husaidia   wananchi kuelewa taratibu ambazo zinaimarisha demokrasia. Bibilia inatumbusha kuwa kuptia Uvumilivu wa viongozi kufuata mambo ya amani na mambo yafaayokwa kuengana; hali hii itasaidia kueneza uwajibikaji kwani wananchi wataweza kukosoa serikali na ujumbe kufikishwa serikalini bila kuogopa kwa kuelewa dhan ya uvumilivu.

Yesu alikuwa mwanaFalsafa  Mkuu wa Uvumilivu  anawa na kuwakumbusha viongozi na wananchi wanatakiwa kuishi kulingana na fikira njema. Mwenye kuifuata falsafa ya uvumilivu hayuko tayari kuamsha fikra mbaya za uvunjajiwa amani bali daima atajitaidi kuziepusha kwa kuendeleza uamuzi  wa uwazi na kwa kutumia njia  ya utulivu wa hekima kupitia uzoefu makini wa kimantiki: Kiongozi mwenye uvumilivu daima hutafakari, na kuziweka fikira mahali pamoja kabla ya kufanya uamauzi.


Ni ukweli ambao haufichiki kuwa sisi kama  wananchi tukiweza kuvumiliana katika maisha yetu ya kawaida, na kuweza kukosoana bila kugombana mara moja  hurudisha imani ya wananchi, upendo na matumaini kati wananchi wao kwa wao au dhidi ya serikali yao; Tukumbukwe kuwa Ingawa watu wengi kufikiria uvumilivu ni upole  na kuto wajibika la hasha uvumilivu ni uwajibikaji ulio jaa busara na subira; Hii ni tafakari yetu ya leo. Amina

No comments:

Post a Comment