WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, January 8, 2016

TUNATAKIWA KUTOA ZAIDI KULIKO KUPOKEA:



January 8


Tafakari ya leo tunaangalia huluka ya binadamu; binadamu tunapenda kupokea zaidi kuliko kutoa. Na pale tunapokuwa tayari kutoa tunajitahidi kutoa kile cha ziada ambacho hatukihitaji kwa wakati husika. Tunajua kuwa utoaji ni kielelzo cha juu kabisa cha neema ya kimungu ndani ya maisha yetu.

Bibilia inatufundisha kuwa kutoka mwanzo kuwa Mungu ndio mmiliki wa kila kitu na maisha yetu yote na vyote ambavyo tunavyo. Sisi ni watumishi tu, hivyo kama yeye alivyomtoaji nasi tunapaswa kufanya hivyo.

Je sisi ni watumishi ambao tunafurahia kupokea tu na sio kutoa?
Je mtumishi bora ni yupi Yule ambaye hutoa kwa moyo wake wote kwa wahitaji au Yule ambaye anatamani tu kupokea?

Kutoa ni moyo wa ushujaa sana kwani ni tendo njema la kuwasaidia wahitaji ambao hawana kimbilio na kimbilio liko kwako kwani Mungu alivyotumba sisi alituumba kwa mfano wake; hivyo nasi tunatakiwa tuwe kama Baba yetu ambaye anatuagiza leo tuwe watu wa kutoa sio wa kupokea zaidi.

Katika Jamii yetu tunao watu ambao ni wahitaji msaada katika Afya zao, katika Elimu zao, na kadhalika na tunapo fikiria mtu ambaye anaweza kusaidia katika hili hapa ndipo wazo la kutoa linapotimia. Mtoaji huleta furaha ndani ya jamii kwani humsaidia yule ambaye ni mwitaji; ukiwa mtoaji ni ukweli kuwa unamweka mwenye shida mbele na unakuwa tayari umefanya kazi ya Utumishi wa Mungu wa kuleta furaha ndani ya jamii ya wenye shida. Ni vyema kama tutaweza kujijengea tabia ya kutoa zaidi kuliko kupokea, Badala ya kuthamani kujiwekea utajiri.

 Katika tafakari ya leo Bibilia kupitia kitabu cha 2 Wakorintho 9:6-7; inatumbusha kuwa apandaye haba atavuna haba; apanda ye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu. Kila mtu na atende kama alivokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu. Pia tumetiwa moyo tuwe watunzaji wema wa kile ambacho Mungu ametupa.

Lakini pamoja umuhimu wa kutoa lakini lazima tuzingatie maelekezo ya Yesu kupitia Luka 16:11 Basi kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe. Pia tumewajibika kuwatafutia risiki wale wa nyumba yetu ndio dhana ya utoaji inapoanzia;

Kitabu cha 1 Timotheo 5:8 atukumbusha: “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.ni kweli kuwa; ni mapenzi ya Mungu tupate vitu vyote vitakavyotufanya  tufurahie maisha yetu duniani. kimaisha, tunapata thawabu kubwa kwa Mungu. Kumsaidia mhitaji kitu, ni kujikopesha mbele ya Mungu  .  tukumbuke kuwa Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa. Kwani Mungu wako atakubariki kama alivyokuahidi.

Kama akiwapo mtu maskini pamoja nawe  usifanye moyo wako kuwa mgumu, wala usimfumbie mkono wako nduguyo maskini”. Mathayo 25:35, 40, 34 Kwa maana nalikuwa na njaa mkanipa chakula, nalikuwa na kiu mkaninywesha, nalikuwa mgeni mkanikaribisha, nalikuwa uchi mkanivika, nalikuwa mgonjwa mkaja kunitazama, nalikuwa kifungoni mkanijia. Yesu akawaambia; Amini nawaambia, kadri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu wahitaji, mlinitendea mimi.


Hivyo, njooni mliobarikiwa na baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu. Mdo 20:35 tunapohitimisha tafakari yetu ya leo tukumbuke kuwa ni kheri kutoa kuliko kupokea. Kwa maana Mungu atakupa kwa wingi Baraka katika maisha yako na uzao wako hapa duniani na atakupa uzima wa milele mbinguni kama tutaendelea kutimiza wajibu wetu wa kutoa zaidi kuliko kupokea. 

Amen

No comments:

Post a Comment