WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Thursday, January 7, 2016

BIBLIA INATUFUNDISHA NINI KUHUSU UMUHIMU WA UWAJIBIKAJI



January 7


Tafakari ya leo inahusu swala nzima la umuhimu wa uwajibikaji na maagizo ya bibilia yanavyosisitiza umuhimu kwa viongozi wote wa dini na siasa na serikali kuwajibika kwa Taifa husika. Tunajua kuwa viongozi  wa dini wanao wajibu wa kuhakikisha kuwa wanawa hudumia waumini wao ipasanyo katika kutimiza kazi ya mungu kwa umakini, upole na unyenyekevu, na lazima matendo yao yawe na mfano wa uwajibikaji wenye Tija kwa taifa.

Ni ukweli kuwa uwajibikaji unahusu uadilifu, uaminifu, unyenyekevu, kutenda haki, kujali wananchi wanyonge ambao hawana kimbilio isipokuwa kwa kiongozi mwabijikaji na awezaye kusimamia haki kwa wote; Tufahamu kuwa leo hii wananchi wanawahitaji viongozi ambao ni wawajibikaji, waadilifu, wakweli, na wanao mwogopa Mungu katika matendo yao. Ndio maana sikuhizi wananchi wanao uwezo mkubwa wa kuwawajibisha viongozi wao ambao utendaji wao sio mzuri; wanaojali zaidi masilahi binafsi, na sio ya Taifa; ili kuwapa wananchi wao maendeleo wanayoyatamani kwa naona waweze kujiona kama ni sehemu ya jamii ambayo inafurahia matunda ya taifa lao.  

Bibilia inatukumbusha kuwa viongozi lazima wawe waadilifu na wanajali uwajibikaji wa taifa uadilifu huleta upendo kwa taifa na mshikamano  kama tunavyosoma kutoka katika kitabu cha 1 wakorinto 13. Wazo kubwa hapa ni upendo ambao unasaidia kufanya kazi kwa uadilifu; upendo ni kila kitu haufurahii udhalimu bali hufurahia dhana ya pamoja.

Tukizingatia kuwa wananchi wanawachagua viongozi kwa vile wamewaamini na kuwapa dhamana na sio bure wanawataka sasa waweze kuwajibika; kiongozi ambaye hawajibiki hujenga chuki, hasari, visasi  kati yake na wananchi ambao wameamua kuwachagua. Matayo 6; 22 anatukumbusha kuwa uwajibikaji ni taa ya ni jicho; basi jicho lako likiwa safi mwili wako wote utakuwa na nuru, hii ndio dhana ya uwajibikaji. Marko anafafanua vizuri sana 10:45 kwa maana mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa bali kutumika na kutoa nafsi yake iwe faida ya wengi.

Kiongozi mzuri atafurahi pamoja na wananchi wake na atalia pamoja na wananchi wake; kwani ukitaka kuwa kiongozi lazima uwe mtumishi wa wote. Tunawaombea viongozi wetu wawe na moyo safi wa kuwajibika na kuwafundisha wakubali kukosolewa na wale ambao wanashindwa kuwajibika tuweke mfumo wa kuwawajibisha. Tukumbuke kuwa hakuna kiongozi ambaye anasifiwa akiwa ni mtu wa kuendekeza ubinafsi, bali ukiwa mwajibikaji mtoaji kwa wananchi katika maendeleo yao huwa unasifiwa sana na unapata baraka za kimungu.

Kiongozi mwajibikaji huwa anaangalia kwanza masilahi ya watu wake; Yesu katika kitabu cha Matayo 11.28- 30 alielezea nini maana ya uwajibikaji kuwa unakuwa ni kimbilio la wanyonge aliposema njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na kuelemewa na mizigo nami nitawawapumzisha.

Viongozi ambao sio wawajibikaji hutumia nguvu zaidi katika kuhakikisha kuwa jamii inapoteza haki zao za msingi nguvu zao za kipesa pamoja na wafuasi wao wachahce na hivyo  kuwatesa wanyonge kwa kuwanyima haki zao za msingi kama, matibabu, haki ya kupata huduma bora za usafiri na maji salama, haki ya elimu bora na malazi salama.

Kiongozi mwajibikaji na mwogopa mungu ataweza yasimamia vyema shida za jamii yake na analinganishwa na maneno haya mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo nanyi mtapata raha nafsini mwenu nitawatua mizigo yenu. Tunahitaji viongozi wa kama Yesu katika jamii zetu watakuwa wapole hawana kiburi na wanamwogopa mungu.

Kitabu cha Wafilipi 2.3 4 kinatukumbusha kuwa tusitende neno lolote kwa kushindana wala majivuno bali kwa unyenyekeve, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.


Hii ndio dhana ya uwajibikaji ambayo bibilia inataka sisi tutekeleze kama viongozi. Tunatakiwa tutimize kusudi la mungu ambalo ni njema mbele ya watu tunaowaongoza. Tukumbuke kuwa pale tunapowatendea haki waja wa Mwenyezi Mungu Yeye aliyeanziasha hii kazi nzuri Moyoni mwetu hatatuacha peke yetu atakuwa nasi na ataendelea kutupa nguvu ya ajabu katika kutimiza wajibu wetu kwa Taifa lake. 

Hii ni tafakari ya leo ambayo tukiitekeleza ipasavyo itatatufunulia nuru ya kweli katikautendaji na uwajibikaji wetu - amina 

No comments:

Post a Comment