WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Sunday, January 3, 2016

Bwana Tufundishe jinsi ya kusali:

JANUARY 3



Hili lilikuwa ombi la wafuasi wa yesu, pamoja kuwa na yesu siku zote wafuasi wa Yesu walijifunza na walimwona yesu akitumia muda mwingi akiwa akiongea na Mwenyezi Mungu kwa sala. Na alikuwa akitumia muda huo akiwa katika faraga na sehemu ya utulivu; hali hii ilikuwa ni ngeni kwa wanafunzi ndipo nao walitamani kufanana na Yesu hivyo waliomba nao wafundishwe jinsi ya kusali.

Tunafahamu kuwa sala ni njia pekee ambayo inafungua njia ya mawasiliano na Mungu. Sala ni njia pekee ambayo inatuunganisha na mungu. Sala ni njia pekee ambayo inaonyesha ukuu wa mungu katika maisha yetu; sala ni nia pekee ambayo inaonyesha shukrani yetu, unyenyekevu wetu, na kuomba msamaha kwa mungu;

lakini tukumbuke kuwa maombi pia yanaunganisha mioyo yetu na akili zetu ambazo zinaleta utulivu kwani mwili wako ndio hakelu la bwana, hili ni kanisa ndani yako; tukisoma kitabu cha James 4: sala hutupatanisha na Mungu; sala huleta upatanishi miongoni mwetu, huwezi kuwa mpatanishi kama hujui jinsi ya kuomba; upatanishi msingi wake mkubwa ni unyenyekevu na unyenyekevu hutoka na uwezo wetu wa kuongea na Mungu; ndio maana wapatanishi wanaitwa wana wa Mungu; tukisoma Matayo 5:9 anafafanua zaidi.

yesu alipokuwa akihubiri kuhusu upatanishi alikuwa akiliongelea hili katika maana pana sana. Hakuwa anaongelea tu kuwa kuna mtu mmoja ambaye anawajibu wa kuleta upatanishi pale ambapo tunafikiri kuwa kuna khali ya kutokuwa na amani; Yesu alikuwa anatuagiza sisi sote kuwa jukumu la luleta upatanishi ni letu sote.lakini upatanishi wa kweli utapatikana kama tunajua jinsi ya kusali; jinsi ya kuongea na Mungu kama Yesu alivyokuwa.

je tunajua kuwa amani huleta haki na furaha ya maisha? Na amani ya kwelihupatikana kwa sala ambayo hutufanya sisi kuwa wanyenyekevu.

Kwa hiyo tukiendelea na tafakari yetu katika mwaka huu tukumbuke kuwa sisi nasi leo tunatakiwa kuendelea kuomba kufundishwa jinsi ya kusali kama wafuasi wa Yesu walivyo omba kufundisha na Yesu aliwafundisha.

No comments:

Post a Comment