WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Monday, January 7, 2019

SIKU 6: AKISI YA IMANI

JANUARY 6.         2019

FUNZO  KUTOKA KWA ABRAMU

Lengo la Mungu ni kutuongoza sisi katika mwelekeo mzuri katika maisha Yetu na ametujalia Sisi zawadi ya Imani kama dira ya kufuata:

Jambo la msingi ambalo lazima tulikumbuke ni kuwa dira yetu sio njia iliyonyoka:

Tukumbuke kuwa kadiri tunavyo songa mbele katika njia hiyo ndivyo tunavyo kutana na vikwazo ambavyo vinapima imani yetu mbele ya Mungu:

Mara nyingi katika vikwazo hivi tunaanza kukata tamaa  na kuacha kumwamini Mungu na kuanza kutegemea akili zetu wenyewe:
Tuna amua kubadilisha mwelekeo na kupuuza mwongozo wa Mungu kupitia imani na kukaribisha mashaka na woga kuchukua nafasi ya zaidi ya Imani:
 
Abramu ni mfano wa mtu ambaye imani yake ilikumbwa na hofu pamoja na Mungu kumpa maelekezo na ahadi nzito na Nzuri kama tunavyo soma katika:

Mwanzo 12:1-3 BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;

3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.

Ni kweli kabisa katika Imani na utii Abramu aliweza kuacha makazi yake na kwenda nchi ya ahadi kanani kama alivyokuwa amehaidiwa na Mungu’

BWANA akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu BWANA aliyemtokea.

Mungu alitaka Abramu aweke masikani kanani: kutokana na matatizo Abramu aliona Kanani sio mahala pazuri pa kuishi akatunga na uwongo pia ili aweze kupikelewa Misri hii ilikuwa Safari yake binafsi kwa sababu Kanani kulikuwa na njaa:

Ni kweli kabisa kama Abramu angeweza kutimiza maelekezo ya Mungu katika Safari yake yote na kufanya makazi kama Mungu alivyomwagiza na kumwabudu yeye Mungu angemlinda na kumpatia mahitaji yake:

Alichokiona Abramu ilikuwa ni ukame na njaa Imani yake ilijaa mashaka: Mungu kwake ilikuwa sio kipimo tena kwa wakati huu:

Leo sote tunakumbushwa kuwa kubadilika kwa mazingira: hali ya kiuchumi isiwe  sababu ya msingi kuacha kumwamini Mungu:

Leo tusiwe kama Abramu tuhakikishe kuwa tukipata mwongozo wa Mungu tuutekeleze mpaka Mwisho bila kutafuta sababu na wala mazingira yasiwe na nafasi ya kubadilisha Imani kuwa mashaka au woga: mazingira na akili zetu zisiwe sababu ya kupoteza imani yetu kwa Mungu: Bali viwe vitu vya kutujenga Sisi:

Abramu alifikiri kuwa kwa kwenda Misri  ilikuwa ni jibu sahihi la kukwepa njaa: Alisahau kuwa alikuwa amepoteza Imani mbele ya Mungu:

Mara nyingi tunasahau kuwa Mungu wetu yeye ni mlinzi wetu na mpaji wa Riziki zetu za kila siku:

Mara nyingi tunajiona kuwa sisi ndio wenye mamlaka zaidi ya Mungu:

Abramu alitakiwa kubaki katika Mungu na kubaki kanani pamoja na mashaka yake yote yaliyo mpata: Wajibu wake ulitakiwa kuendelea kumtumaini Mungu na kuiweka Imani yake juu ya Mungu:

Mungu alikuwa na mpango mzuri na Abramu : hata Leo sisi tunaendelea kusahau kuwa Mungu ni kila kitu kwetu  na ana mpango mzuri Kwetu ni wajibu wetu kuendelea kumwamini:

Mpango ambao utashindwa mbele ya Mungu: Tukumbuke kuwa Mungu hayuko karibu na wenye kiburi bali hufanya Kazi na wanyenyekevu wenye Imani ya kweli :

Hilo ndilo somo letu la leo kuhusu Imani: Imani yako imeendelea kukua katika mashaka ??

Amina 🙏🏿🙏🏿🙏🏿Amina 👏👏👏Amina

No comments:

Post a Comment