WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Wednesday, January 16, 2019

SIKU 16: AKISI YA IMANI

JANUARY16.                        2019

BUSARA NI MUHIMU KATIKA KUTEKELEZA IMANI (1)

Somo letu leo ebu tuangalie namna gani busara huimarisha Imani: sio tu Imani ya mapito ya Dunia bali Imani juu ya uwezo wa Mungu;

mtaalamu mmoja Albert Einstein. wakati mmoja alipokuwa akiendele na mihadhara yake alikuwa akitoa katika vyuo vikuu mbalimbali  kuhusu somo la theory yake ya relativity;

Einstein  pamoja na akili na busara zake hakuwa na leseni ya kuweza kuendesha gari hivyo alikuwa na dereva ambaye alikuwa akimzungusha wakati wote wa mihadhara katika vyuo mbalimbali;

Aliamini uwezo wa dereva wake na hakuwa na mashaka kabisa na uwezo wa dereva wake alimwamini kwa matendo yake: Imani ni Matendo:

Siku moja walipokuwa wakielekea katika moja ya mhadhara; dereva wake alimwambia kuwa unajua umekuwa nami kwa muda mrefu katika hii mihadhara  unajua kuwa mimi nimesikiliza midhara yako kwa muda mrefu:
Alimwambia Dr Einstein kuwa mimi ninaweza nikatoa mhadhara leo:

Dereva Alikuwa na Imani na kujiamini kuwa anao uwezo wa kufundisha:  Alitaka kuonyesha kwa vitendo: Imani bila Matendo inakuwa imekufa:

Dereva alijenga imani katika Jambo ambalo hajawahi fanya: lakini aliamini atafanikiwa: Einstein alicheka na kukubali kwa mashaka: Hakuwa na Imani kuwa anaweza kufanya Kazi katika ubora unaotakiwa: Hekima yake ikamsukuma akubali lakini imani yake ilikuwa haba:

Hatimaye alisema ngoja tujaribu kwani watu wa chuo hicho hawajewahi niona mimi hivyo hawatanifahamu nimefanana vipi;

Hivyo walikubaliana  dereva alivaa kama Dr. Einstein na Dr. Einstein akavaa nguo za dereva na kofia yake;
Walipofika alitambulishwa kuwa ni Dr. Einstein;

kila kitu kilikwenda vizuri sana kama walivyokuwa wamepanga; Dereva aliweza kutoa mhadhara vizuri sana kuhusu somo la relativity na Einstein  alikuwa amekaa nyuma akisikiliza; na kufurahia umahili wa dereva wake; lakini wakati akiendelea kutoa mhadhara mratibu wa mhadhara alisema kuwa bado walikuwa na dakika 15 zaidi hivyo ni muda ambao unatosha kumwuliza Dr Einstein swali; miongoni mwa watu ambao alikuwa amehudhuria alikuwa Profesa wa hesabu ambaye alimuuliza dr Einstein swali gumu kuhusu formula na lugha ambazo dereva hakuweza elewa kabisa;

Kitu kizuri dereva alikuwa mwepesi wa kufikiri na akamjibu profesa wa hesabu kuwa  suluhu la tatizo ambalo alikuwa ameuliza lilikuwa rahisi sana na alishangaa kwa nini ameuliza umeuliza swali kama hili; kwani kila mtu anaweza kujibu hili swali; hivyo nitamwambia dereva wangu aje hapa na kujibu swali hili; Busara na Imani vinapo fanya Kazi pamoja:

Kwa kuthibitisha hili ngoja sasa nimwite dereva wangu aweze kuja kujibu hili swali; kwa upande mmoja Dr Einstein alikuwa na akili lakini dereva wake alikuwa na mtu mwenye busara/hekima na Imani;

Tunachojifunza hapa kuwa daima tumekuwa hodari sana wa kuweza kuamini na kutenda kwa mambo ya kidunia: Tunatumia busara na Imani vizuri sana katika mambo siyo ya Kimungu

Wakati umefika sasa iwe ni Busara/Hekima na Imani viwe juu ya Mungu: tunapotamani kuimarisha busara na Imani Yetu iwe juu ya Mungu Baba : Mwana na Roho Mtakatifu:

Ni kweli kuwa wewe na mimi tunatamani kuwa na hekima; Tunafahamu kuwa kila siku tunakabiliwa na maamuzi ambayo yanahitaji uwezo wa ufikiri kwa haraka uliojaa busara na Imani:

Daima tunaomba hekima; tukumkuke kuwa sote tumejaliwa maarifa ;  maarifa ni uwezo unaotusaidia sisi kuweza kukusanya taarifa ili kuweza kufikia utatuzi wa shida ambayo iko mbele yetu; Bali tuombe hekima ya kimungu ili tuweze tekekeza Imani katika njia ya Kimungu:
Methali 18:15 Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.

Ni ukweli kuwa hekima ni neema kutoka kwa Mungu; ni uwezo ambao unapata ili  Kuyaishi  maisha katika jicho la ukweli na kuitekeleza Imani katika vitendo:

Tuhitimishe somo letu tukiwaza zaidi kutafuta busara/hekima na Imani kwa kutenda vile Mungu anavyotaka Sisi tutende:

🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿👏👏👏👏👏

Emmanuel Turuka
Kalamazoo MI 49009
2019

No comments:

Post a Comment