WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Sunday, January 6, 2019

SIKU 4; AKISI YA IMANI

JANUARY 4

JE TUNAISHI KATIKA MASHAKA

Ni Jambo ambalo halikwepeki kabisa kuhusu masha katika imani na katika maisha Yetu ya ya kila SIKu kama nilivyoeleza kidogo katika maelezo yaliyotangulia: kwa upande mwingine mashaka huchochea imani:

Tukisoma kitabu cha Mhubiri: Maombolezo: Habakuki na Zaburi tunaoma mashaka ambayo watumishi wa Mungu walikuwa wakiyapitia:

Lakini hata nasi katika maisha yetu ya kila siku tunaishi katika mashaka makubwa: Maswali kama:

je nimefanya uchaguzi sahihi?
Je Jambo hili nimelifanya ipasavyo?
Je nguo hii naihitaji au niirusdishe dukani?

Tuna mashaka kuhusu jambo ambalo liko mbele yetu mashaka yaliyojaa woga;

Tuna mashaka kuhusu watu wengine juu ya maisha yetu suspicion.

Tuna mashaka juu ya maisha Yetu ya kutojiamini na kujitoa thamani wenyewe:

Tuna mashaka juu ya kila kitu  katika maisha Yetu (skepticism).

Tuna mashaka juu ya Mungu Bado akili yetu haijeweza kuacha kudadisi kuhusu ukuu na uweza wa Mungu.
(uncertainty).

Yaani maisha Yetu ni mashaka mashaka tu:

Yesu alimwambia Tomaso mwenye imani haba: Yesu alijua kuwa Tomaso anaimani na anaamini lakini imani yake ilijengwa katika mashaka: Imani yake ilijengwa katika kuona kwanza:

Ndio maana wengi wetu Imani yetu imejengwa katika msingi wa Tomaso: ni imani ambayo imezungukwa na mashaka: na ni kweli kuwa mashaka sio kinyume cha imani; ila kutoamini ni kunyume cha imani. Mashaka ni kutokuwa na uhakika: kupata ugumu katika maamuzi:

Waebu 11:6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.
Ni kweli mashaka ni sehemu ya kuifikia imani; hii yote inatokana na ukweli kuwa binadamu tunakosa ushupavu wa kumwamini Mungu na maagizo yote yanayo husiana na Imani: katika maisha yetu ni rahisi kabisa na kuwa na uhakika wa 2+2=4: je jibu hili linaweza badilisha maisha au kusudi lako la maisha? Tuendelee kutembea pamoja katika Safari hii ya Imani:

Emmanuel Turuka
Kalamazoo MI
49009

No comments:

Post a Comment