WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Sunday, August 21, 2016

YESU NJOO KAA KWANGU LEO


August  19

2 Timotheo 1:7-8

Tafakari yetu leo inamwita Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mwokozi wetu aweze kuja kukaa nasi; Maisha yetu kama binadamu tunapambana na matatizo na mahitaji mengi ambayo mengine hujisababishia sisi wenyewe na Mengine Husababisha na watu wetu wengine: katika mazingira ya aina yeyote ile hatutakiwi kupoteza imani; kama Mtume Paulo anavyotukumbusha kuwa pamoja na mateso ,kufungwa na kujua kuwa maisha yake yataishia kuuawa bali hakupoteza iamani yake aliendelea kumwamini Mungu kupitia kwa bwana wetU Yesu Kristo ambaya alikuwa anakaa ndani ya Moyo wake; Hivyo ni jukumu letu nasi leo kumkaribisha Yesu katika mwili wetu aweze kuisha nasi katika maisha yetu; tunajua kuwa ugumu wa maisha uko mbele yetu; msongamano wa mawazo uko mbele yetu; haya yote yanavyotokea lazima tuwe tayari kuyakabili, lakini unapomkaribisha Yesu ndani ya maisha yetu changamoto hizi ni rahisi kuzikabili kwani neno lake linatoa faraja kubwa na kufukuza mbali shida zote;

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa ushindi mkubwa wa msiaha yetu ni kuwa kwani yeye anafahamu hata idadi  ya nywele Mathayo 10:20 lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Sisi hatuna uwezo wa kujua idadi yake lakini yeye anajua; hivyo tunataka zawasi gani zaidi katika maisha yetu kama sio uwepo wake katika maisha yetu? Yesu ni jibu la maswali yetu yote; je nani angeweza kufanya kama Yesu ambaye aliuacha utukufu wake wote na kukubali kuja duniani na kupata mateso, kudharauliwa, kupigwa, kutukanwa na kasha kusulubiwa msalabani kwa ajili yangu mimi? Kwa nini sasa nisimkaribishe Yeye katika maisha yangu? 2 Timotheo 7-8 Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi. Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, wala usinionee haya mimi mfungwa wake, bali uvumilie mabaya pamoja nami kwa ajili ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu; 

Tafakari yetu leo inaendelea kutukumbusha kuwa; inatukumbusha mfano wa Yule mama ambaye alikuwa akisumbuliwa na tatizo la kutoka damu kwa miaka mingi na alikuwa akitafuta tiba kwa kipindi hicho chote; Lakini aliposikia habari za Yesu na ukuu wake alijisemea moyoni mwake namkaribisha Yesu katika maisha yangu, lakini kwa uwezo ambao anao pamoja na kumkaribisha katika maisha yangu nitaligusa tu pindo la vazi lake nami nitapona. Pamoja na umati mkubwa wa watu alifanya kila jitihada za kujipenyeza, kusukuma na watu ambo pia walitaka kumwona na kumsikiliza Yesu lakini walikuwa hawaka tayari kumkaribisha Yesu katika maisha yao ili aweze kuwaponya na matatizo yao; lakini yeye alifanikiwa kumgusa pindo lake kwa imani moja tu kuwa ugonjwa wangu utapona kwa tendo langu na ilikuwa hivyo; hivyo tunamwitaji yesu kwa kuwa Yesu ni jibu katika matatizo yetu:

Hii ndio tafakari yetu ya leo- Amina

Emmanuel Turuka



No comments:

Post a Comment