WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Sunday, August 14, 2016

UTUMISHI ULIOTUKUKA MBELE YA MUNGU

 AUGUST 14

 ZAWADI AMBAYO KILA MTU ANAHITAJI KATIKA MAISHA;


2 Timothy 3:1–5

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa kila mtu anahitaji zawadi iliyo bora kabisa katika maisha yake; ni kila mtu anahitaji zawadi kubwa ya maisha ambayo ni upendo; ukiwa na upendo kwa kweli familia zetu au jumuia zetu zitakuwaje? Je myumba zetu zitakuwaje? Je ofisi zetu zitakuwaje? Je shule zetu zitakuwaje? Natumaini kama tutakuwa katika maisha ya upendo hakika tutakuwa katika ni kisima cha ajabu chenye upendo mkubwa Galatians 6:10 . Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio  Itakuwa ni rahisi kujiuliza swali hili je leo nani atakuwa mbarikiwa kwani daima akili yetu itakuwa ikiangalia upande mzuri wa maisha yetu na sio upande mbaya: 2 Timothy 3:1–5 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.  Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio  safi,  wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,  wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;   wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.


Tafakari yetu inatuonya kuwa Kunyume cha upendo ni uangamizi kwani kila mtu atakuwa kweney harakati; na akiyatizama maisha yake pekee yake watakuwa wakijisifu katika mafanikio ambayo hayajali maisha ya watu wengine. Daima tunajisahau na kujiona kuwa wafalme katika mafanikio yetu; na kwa msingi huo tunakuwa hatuna muda wa kuonyesha upendo kwa wengine; lakini tukumbuke kuwa kamwe hatujeumbwa kuishi kwa ukabaila na uchoyo; ni wajibu wetu kufanya jambo lolote amablo litaonekana tofauti kwa wengine. Siri ya Mungu kwetu ni hii kamwe hatutakuwa tumeishi maisha ya kumpendeza Mungu kama hutafanya jambo njema kwa wenzetu bila kujihatijika wao kurudisha fadhila. Je umeshaona jinsi marafiki wanavyoishi kwa kuumizana? Ukiwa bizi sana huwezi kuliona hili mpaka pale utakapo tuo ushirikiano na kujifunza kwa watu wengine kwa kuona shida zao; Mathayo 25:40  Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi. Methali 19:17 Amhurumiaye maskini humkopesha Bwana; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.

Tafakaria yetu ina tuuliza kuwa; Je wewe umefanya tofauti gani leo? Kwa mjane? Kwa mototo yatima; kwa mzee au masikini ambaye anahitaji huruma ya Mungu kupitia kwako? Tunapofanya wema kwa wenzetu tunawajengea taswira ya ajabu katika mioyo yao na wanamwona Mungu katika maisha yao kupitia kwetu: je uko tayari kuwa sehemu ya utukufu wa Mungu kwa kuwasaidia wahitaji wa kweli leo? Kama mtoto mmoja alivyomuuliza Mama mmoja ambaye alimnunulia pea tatu za viatu ambavyo alikuwa akivitamani sana kuwa je wewe ni Mke wa Mungu? Katika taswira yake anajua wema unatoka kwa Mung tu? Je wewe uko tayari kufanya wema ili utukufu wa Mungu ungae katika maisha yako? Kutoa kwa moyo ni hadhina pekee unayojijegea mbele ya Mungu. Yatupasa kujifunza kuwa watu wa kutoa na kuwa mwema katika maisha ya watu wengine; Yatupasa kuonyesha maisha yetu mema kila wakati na kila mahali tunapokwenda;

Tafkari yetu leo inaendelea kusisitiza kuwa Upendo lazima uonekane katika maisha yetu kwa vitendo;  kupitia muda wako, uwezo wako wa kifedha hata kwa maneno mazuri ya kuhamasisha kwa kufanaya hivyo tunamkaribisha Mungu katika maisha yetu ya kila siku; wakati mwingine tunakatishwa tamaa pale ambapo unatoa msaada wa wenzetu lakini wahusika wakisha pata msaada yaani wanakuwa hawana muda wa kusema asante, la msingi uelewe kuwa mungu daima anaweka kumbukumbu katika kila jambo njema ambalo tunalifanya hivyo hatunasababu ya kusubiri asante ya kibinadamu waajibu wetu yatupas kushukuru kwani Mungu yeye ndiye atakaye kurudishia wewe mara elfu elfu kwa wema wako. Jicho la mungu ni la ajabu linaona kila kitu tufanyacho. Mbegu iliyo bora hupandwa kwenye udongo mzuri na udongo mzuri hutoka kwa mungu. Sikila shida za watu nawe uwe utabarikiwa kwa msaada wako kwao kwani wao hawana uwezo mwenyezi  Mungu atakubariki kwa upendo wako;

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa pendo la kweli lazima lionyeshwe kwa matendo yetu, tukumbuka kuwa watu wanatuangalia sisi, tukumbuke kuwa kadiri tunavyowasaidia wengine ndivyo hivyo Mungu atakavyo turudishia na kutusaidia kwa kadiri ya mahitaji yetu; Mungu  atakuzidisha mara elfu elfu lakini lazima utambulike  kwa matunda ambayo umeyapanda na yameleta furaha na amani kwa wengine; Mathayo 7:16–20. Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?  Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.  Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.  Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.  Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua. 

Tafakari yetu inasisitiza kuwa  ili kuweza kutekeleza utumishi ulio tukuka lazima atimize wajibu wake wa kujijenmgea msingi ulio bora Mathayo 7: 24-27 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na uyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.  Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa. 

Hii ndio tafakari yetu ya leo Amina


Emmanuel Turuka

No comments:

Post a Comment