WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Wednesday, March 1, 2017

SIKU 40 NI KIPINDI CHA KUTENDA MEMA (KWARESMA/LENT)





Kwaresma ni kipindi ambacho tunakumbuka maisha ya Mwokozi wetu Yesu kristo na kazi yake ya ukombozi wa maisha yetu katika safari ya maisha yetu baada ya maisha ya hapa duniani. Kwa maneno mengine Kwaresma ni kipindi maalum ambacho wakristo
Wanatakiwa wayaelekeze maisha yao zaidi katika sala, kufunga na kuwasaidia wale ambao wanahitaji masaada. Ni kipindi zaidi cha kutafakari na kufanya toba na kumrudia Mungu.

Kipindi cha Kwaresma  kinajumuisha siku arobaini za toba na shukurani kwa Mungu. Tukisoma katika maandiko matakatifu tunaweza kuona jinsi  watumishi wa Mungu manabii ambao Mungu aliwapa majukumu mazito baada ya kufunga na kusali kwa siku 40; Walitakiwa kutubu kabla ya maombi au ahadi ambazo Mwenyezi Mungu aliwaandaa kuzipokea kwa faida ya watu wao.  Musa alifunga siku 40 kabla ya kupokea amri kumi za Mungu “Naye alikuwa huko pamoja na Bwana siku arobaini na masiku yake; hakula chakula, wala hakunywa maji. Naye akaandika katika hizo mbao hayo maneno ya maagano, hizo amri kumi.” (Kutoka 34:28). Nabii Eliya alifunga siku 40 kabla ya kuonana na Mungu kwenye mlima Orebu: “Akainuka, akala akanywa, akaenda katika nguvu za chakula hicho siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu mlima wa Mungu.(I Wafalme 19:8)

Kipindi cha kwaresma siku 40 kwa mfuasi mtiifu wa kristo lazima atapambana na mitihani mingi; kwa vile shetani naye anakuwa kazini kupinga mema ambayo unataka kufanya lazima utakutana chaweza taabu, wasiwasi, uzuzu, woga, kukosa msimamo au mwelekeo.

Tukumbuke maisha ya Yesu kabla ajeanza utume wake Katika Agano jipya, Yesu alifunga siku 40 (jangwani) akipambana na majaribu kabla ya kuanza kazi yake. Alijaribiwa na shetani mara tatu; lakini aliyashinda majaribu ya shetani;

Tukumbuke kuwa Kufunga ni jambo linalomsaidia mtu kutafakari kuhusu mambo ya kiroho na kumkumbusha kwamba kuna mambo muhimu maishani kuliko mali na chakula. Funga inatusaidia sana sisi kujenga uhusiano mzuri pamoja na Mungu. Na kubwa zaidi funga inatusaidia sana sisi tuaminio  katika kutimiza ahadi ya kumshukuru Mungu na kuonyesha kwamba mtu amejitoa kwake. Ninafunga kwa sababu ninampenda Mungu.

Yesu alitoa taadhari ambayo sisi tunapotekeleza Kwaresima hii ya mwaka 2017 tujiepushe kujiona kuwa sisi ni bora zaidi; mimi ni mwadilifu zaidi kuliko mwenzangu; Tuondoe dhana ya kuhukumu; hii ni sawa na kujisifia mwenyewe wakati hujui mwenzako pia amefanya nini ambacho kimempendeza Mungu. Tumkumbuke Yule farisayo mwenye kiburi aliyejiona kuwa bora kuliko wengine kwa sababu alifunga kwa ukawaida, unaonyesha wazi kwamba Mungu anakataa mtazamo kama huo. Yesu anatukumbusha kuwa tendo la kufunga ni tendo jema lakini ni tendo linalohusisha nafsi yako na Mungu na hupaswi kuwaambia wengine kwamba umefunga.

Wote wakitambua hali yao ya dhambi mbele ya Mwenyezi Mungu hutumia wakati huo katika kutubu, kuungama na kukiri makosa yao mbele ya Mwenyezi Mungu. Toba hiyo hufanyika kwa njia mbalimbali. Licha ya kufanya hiyo toba, pia wanashauriwa kusali zaidi wakati huo wa toba. Tunavyofahamu sala ni mahusiano ya karibu sana ya binadamu na Muumba wake. Hapo hutoa sala za kushukuru, sala za kuabudu, sala za kumsifu Mwenyezi Mungu, sala za kumtukuza, sala za kuomba msamaha kwa dhambi mbalimbali tulizomkosea Mwenyezi Mungu na pia zile ambazo tumewakosea binadamu wenzetu.

Maisha yetu sisi kama binadamu maisha yetu yamejaa matendo maovu; hivyo kipindi cha kwaresima ni wakati mzuri wa  kujipatanisha na Mungu kwani kwa kutenda dhambi sisi tunajifarakanisha na Muumbawetu, na hivyo tuhitaji upatanisho. Siyo hayo tu, pia huyo binadamu huwa amejitenga na binadamu wenzake anayeishi na kushirikiana naye. Kwa hiyo jambo la tatu analopaswa kulifanya mtu yule mwenye kufanya toba ni kufanya matendo mema, yaani kutoa sadaka kwa ajili ya maskini na wale ambao ni wanyonge katika jamii yetu.

Ni matumaini yetu kuwa Mfungo huu wa Kwaresima utakuwa ni wenye manufaa kabisa kwa Waumini wenyewe binafsi, lakini pia kwa ndugu na marafiki wote. Tukumbuke kuwa hasira ya Mungu itatulizwa tu ikiwa waumini tunafunga na kujinyima mambo mbalimbali. Tukiwa na imani tunasadiki kuwa kwa mfungo huo wa waumini wakristo utasaidia kabisa kwa kutuletea neema.

Jambo jingine ambalo Waumini Wakristo wanapaswa kulizingatia ni kwamba imewapasawa kutoa sadaka zao kwa moyo wa ukarimu. Wakati huu wa Mfungo ni wakati hasa wa kutenda matendo mema na kuacha uchoyo na ubinafsi. Waumini wanapaswa kuwa wema zaidi, na kuwa wakarimu zaidi. Hivyo ndivyo inavyowapasa wale wote ambao wameamua kufunga na kumrudia Mwenyezi Mungu.

Tukumbuke kuwa Kweresma inatupasa itubadilishe kuwa waumini bora kabisa sisi tu kwa siku 40 bali kwa amsiah yetu yote mpaka tunakufa mfungo, utusaidie kutubadilisha kabisa kutoka ndani ya mioyo yao. Tunaweza kusema kuwa lengo la Mfungo ni kumbadilisha binadamu, ni kufanya mageuzi ya ndani. Kwa maneno mengine tunaweza kusema kuwa Mfungo mtukufu ni kipindi cha kubadilika kutoka ndani na kuwa binadamu aliye mwema na mkarimu zaidi. tunanatakiwa kuonyesha upendo wao kwa maskini.Basi tunaomba kwa njia hii ya Mfungo mtukufu waumini wazidi kujipatanisha na Muumba wao, na pia wajenge mahusiano mema na ndugu zao wanaoishi nao. Kwaresima ni mabadiliko, Kwaresima ni mageuzi, Kwaresima ni kuwa na upendo zaidi wenye ukarimu zaidi. Kwaresima ni kuahidi kuacha mabaya na kuzingatia mema na hivyo Kwaresima ni kuwa watu wapya waliojaa huruma na upendo kwa Mungu na jirani.
  
Nawatakieni kwaresma njema ya mwaka 2017

Emmanuel Turuka

Kalamazoo Michigan

No comments:

Post a Comment