WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Wednesday, March 29, 2017

TAFAKARI: WOGA KATIKA MATENDO YETU UWE SILAHA YA USHINDI




Tafakari yetu ya juma hili tunaangalia dhana ya woga katika maisha yetu; woga ni kielelezo kuwa kuna kitu kimesimama katika njia mbayo tunastahili kupita; lakini pengine kwa mantiti ya ukweli kabisa hakuna kitu cha namna hii; woga huleta wasiwasi na kutufanya kushindwa kufanikiwa malengo yetu; woga hutupotezea kabisa uwezo wetu wa kufikiri na kufanya maamuzi sahihi wa kufikia malengo ambayo ndio lengo la mafanikio yetu;

Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa vizuizi kama woga visiwe kikwazo katika maisha yetu hasa ya kiroho tunakumbushwa hata tukijikwaa kwenye ukuta  ni lazima tukubali kuwa kujikwaa sio mwisho wa safari. Woga ambao husabibisha akili zetu kudumaa lazima upate ufumbuzi ndani ya akili zetu. Akili zetu lazima zijue kuwa kushindwa kunakutokana na woga hatupaswi kutoa  nafasi kwani bibilia inatukumbusha kuwa neema yake inatosha katika shida zetu. Woga utupe sisi ujasili wa kupata ushindi; kushindwa kunakosababishwa na woga kuwe sehemu ya ushindi; Yesu alipokuwa akitembea juu ya maji wafuasi wake walishituka na kujawa na woga wakifikiri kuwa wameona ni jini; walipomtambua kuwa alilikuwa Yesu Petro akamwambia Yesu bwana nami naomba nitembee juu ya maji Yesu alimwita akamwambia njoo, alianza vizuri lakini kwa vile alileta silaha ya woga akaanza kuzama.

Je woga wetu hutoka wapi? Woga katika maisha yetu huletwa na watu wengine, pengine tunatamani kumpendezesha kila mtu, au kuishi kwa matarajio ya maisha ya watu wengine na kwa macho yao  hivyo kwa kuishi katika maisha ya namna hiyo huweza kutupa sisi wakati mgumu sana; lazima kutakuwa na vizingiti vingi sana lakini bado hatutakiwa kukubali kuwa vikwazo vituzuea katika maisha yetu. Tunatakiwa kuwa tayari kuruka vihunzi, na daima macho yetu yawe yanangalia mpira ili tuweze kushinda na sio kuwa watu ambao tumejaa woga. Tukiwa na mawazo ya kushindwa sio sehemu ya ushindi; kushindwa ambako kunatokana na woga ni ishara ya kutuambia sisi kuwa hatuko sawa;

Najua kabisa hatuwezi kuepuka woga lakini woga usitawale maisha yetu, hata Yesu alitawaliwa na woga alipokuwa katika bustani kabla ya safari ya mateso yake lakini kwa ujasiri mkubwa aliushinda woga na kuweza kubeba kikombe cha mateso kwa ujasiri mkubwa hatimaye kuleta ukombozi kwetu sote kwa damu yake pale msalabani.

Tukiendekeza woga basi tumeshajiwekea sisi wenyewe dalili kubwa ya kushindwa;woga unatakiwa utufundishe sisi na kutuletea mageuzi na kutufanya kuwa watu bora zaidi. Tunaposoma kuhusu maisha ya jehanamu tunajawa na woga; basi Woga huu unatakiwa utusaidie sisi tuyafuate maelekezo ya mungu katika kuishi maisha bora ambayo yanampendeza Mungu wetu. Hivyo woga utujengee sisi ushindi kama Yesu alivyofanya na leo tumekombolewa kupitia damu yake takatifu sisi sana kwa ukombozi huu jukumu letu  ni kufanya matendo mema ambayo yanampendeza Mungu.


 Ni jambo nzuri ambalo sisi binadamu tumewekewa Mwenyezi Mungu alijua uzaifu wetu kuwa kwa kushindwa kwetu ambako kunatokana na woga awetu tumewekewa namna ya kuweza kuomba msamaha. Ndio maana  ya kipindi hiki cha toba, kipindi hiki ni alama tu ambayo tunatakiwa kuishi kwa namna hii katika maisha yetu yote. Natukiweza kuishi katika namna hii tutakuwa tumefanikiwa sana sana. Kristo ametuonyesha mfano kuwa yeye aliweza kusimama kidete katika kutuonyesha mfano maisha yale ambayo Mwenyezi Mungu anataka sisi tuishi; tumepewa nafasi ya pili ya kujirekebisha na kuishi bila kutanguliza woga mbele bali kutanguliza ushujaa wa kumpigania Yesu; tunatakiwa tutambue udhaifu wetu na kupata nguvu za kuukabili udhaifu huo; tubadilishe tabia zetu; 

Tafakari yetu inatukumbusha kuwa pamoja na kukabiliwa   maisha wakati mwingine yanakuwa magumu sana; kupitia kipindi hiki cha mfungo na kumrudia Mungu tumepata nafasi nyingine nzuri sana na ya ajabu sana; Mungu anaendelea kutujalia sisi siri kubwa ya ushindi wa maisha yetu na mbinu za kumshinda shetani; lazima tukubali kuendelea kujifunza na kuwa tayari kubadilika; maisha ya ushindi ni magumu na kuwa mwoga haitasaidia kushinda vikwazo ambavyo vinachelewesha ukamilifu wa safari yetu hapa duniani bali lazima tusimame imara na kuamini kuwa bila nguvu za kristo ndani yetu sisi wenyewe hatuwezi kuipigana vita hii kwa ushindi mkubwa; woga wetu utaendelea kuwako bali tukimpokea Kristo woga hauna na nafasi hata kidogo. Maisha yatendelea kuwa mazuri kwa wale wanaomwamini kristo na wako tayari kufa pamoja naye. Woga wako ukimtegemea kristo hauna nafasi kabisa na utakuwa huru; tufunge na Kristo na tufe naye msalabani kwa kuishi maisha yale ambayo kristo aliishi na kuwa alama ya ukombozi wetu ;

Huu ndio ujumbe wetu wa wiki hii ya kwaresma.

Amina            Amina            Amina

Emmanuel Turuka
2017



No comments:

Post a Comment