WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, March 10, 2017

TAFAKARI: TUNAIPOKEAJE ZAWADI KUTOKA KWA MUNGU?


·        KWA MOYO WA SHUKRANI NA UNYENYEKEVU?
·        KWA MOYO WA MALALAMIKO?


Katika kipindi hiki cha Kwaresma tafakari yetu ya wiki hii inatuuliza swali moja je sisi ni watu wa kushukuru au ni watu ambao tumejaa malalamiko tunavyoyakabili maisha yetu ya kila siku?

Tujikumbushe kuwa Mungu wetu ni Mungu aliyejaa huruma na ni Mungu ambaye ni mtoaji; lakini sisi kama wana wake je tunatambua ukuu wa mungu katika maisha yetu? Je zawadi zote ambazo Mwenyezi Mungu anatujalia sisi tunazipokeaje, tunazipokea kwa moyo uliojaa shukrani au tunazipokea kwa kuturidhika na kwa malalamiko? Tatizo letu tunasahau haraka sana zawadi ambazo Mungu anatujalia katika maisha yetu, na daima tunaishia kuwa watu ambao tunakuwa wa kulalamika zaidi na sio kushukuru na kuomba bila kuchoka.

Lakini tunabahati kubwa pamoja na malalmiko yetu Mwenyezi Mungu bado anaendelea kutupenda na kutujalia sisi mahitaji yetu. Tukumbuke jinsi wana wa Israeli walivyokuwa wakilalamika lakini kila siku mpya Mwenyezi Mungu aliendelea kuwalinda na kuwapa mahitaji ambayo walikuwa wakihitaji kwa siku hiyo.

Katika kipindi hiki cha Kwaresima tuendelee kufunga na kusali tukiomba msamaha kwa kosa hili kubwa la kulalamika hata pale tunapotendewa mema. Tunatakiwa kupokea kila zawadi tunayojaliwa katika mikono ya shukrani. Tukumbuke kuwa mbele ya Mungu malalamishi sio kitu cha kujivunia. Unyenyekevu, moyo wa shukrani ndio vitu vya kujivunia mbele ya wenzetu na Mungu.

Tukumbuke kuwa wakati mwingine Mungu anatupa sisi zawadi ambazo hatustahili kabisa. Je kuna zawadi gani kuwa zaidi ya Kumtoa mwanaye aje ulimwenguni ateseke na kufa kifo cha aibu kwa ajili ya dhambi zetu ili sisi nasi tufurahie utukufu wa Mungu Mbinguni. Kwa kuja kwake sisi tumekombolewa.

Tunavyo kumbuka mateso ya Yesu, tujikumbushe kuwa mateso yake yamekuwa ufunguo ambao umetufungulia sisi uzima wa milele. Yesu ameweza kutusaidia sisi kukata kiu ya kufurahia maisha maisha yetu ya baadae; kwani tukiweza kuishi ndani yake kwa matendo kamwe hatuwezi kuogopa kifo; kwani uchungu na ugumu wa Kifo Yesu ameshauondoa.

Kwaresima hii itukumbusha kuwa Yesu ndio mkate kweli wa uzima ambao unasafisha kabisa njaa, wajibu wetu ni kuendelea kuishi kulingana na mafundisho yake. Na kubwa ambalo tunakumbushwa leo tuache kulalamika bali tupokee zawadi zote tunazopewa kwa upendo na kwa moyo wa shukrani ili neema ya mungu ibaki juu yetu.

Ili kuweza kuijiimarisha katika zawadi hii Yesu anataka sisi leo kuendelea kujifunza umuhimu wa zawadi zote ambazo tunazipata leo kupitia watumishi wake ambao wamepewa uwezo wa uwakilishi wa Kristo katika maisha yetu. Wao ni binadamu kama sisi bali ni chombo kilichobarikiwa katika kutekeleza mafundisho ya kutuelimisha sisi umuhimu wa kupokea zawadi zetu kwa moyo mkunjufu uliojaa upendo na shukrani na sio kujijengea tabia  ya kulalamika  na kuona kuwa Mungu anatuchukia;

Tukiweza kupokea zawadi hii ndipo tunapotambua ukuu wa neema ya mungu juu yetu; Mungu anatujenga sisi katika imani kubwa kama tutaweza kuacha kabisa malalamiko, tutakuwa tumekomaa katika imani. Katika tafakari yetu ya wiki hii tumpe asante mungu kwa upendo wetu kwetu kwa kutujalia sisi ridhiki yetu ya kila siku na tunamshukuru kwa kutujalia sisi pia mkate wa uzima jambo la msingi ambalo ndilo linalotawala tafakari yetu je sisi tunapokeaje hii zawadi kubwa ya ukombozi wa maisha yetu?



Emmanuel Turuka

No comments:

Post a Comment