WELCOME - KARIBUNI SANA

GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23

“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney


Friday, April 7, 2017

TAFAKARI: TUJIFUNZE KUTOKUHUKUMU KWA HISIA KATIKA KIPINDI HIKI CHA MFUNGO:



Petro aligeuka na kumwona yuke mwanafunzi ambaye Yesu alikuwa akimpenda sana; akumuuliza je na huyu vipi? Je kama mimi nataka kumwacha huyu mpaka nitakaporudi wewe inakuhusu nini? Wewe nifuate mimi Yohana 21:21-22. Tafakari yetu juma hili Yesu anatukumbusha umuhimu wa kuwa na kiasi katika kutaka kujua mambo ya watu wengine; Tunatakiwa kuwa watu wenye hekima na kujali Zaidi mambo yetu, tufanye kile ambacho yatupasa sisi kufanya; 1Wateselonike 4:11 tena mjitahidi kutulia na kutenda shughuli zenu,na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe kama tulivowaagiza.

Tunakumbushwa sana kujitathimini na kuacha kuingilia maisha ya watu wengine; kwa msingi huu kwamba  tukiangalia sana wale ambao wako sana katika maisha ya watu wengine; basi hawana thamani kabisa hata katika maisha yao ya kila siku; wako tayari kunena ya watu wengine na kutoa hukumu ambayo imejaa hisia kulingana na wao wanavyotaka iwe; kwa maneno mengine wanaweza kuwa chanzo cha mafarakano katika maisha ya  watu wengine katika jamii kwa ujumla. 2 Watesolonike 3:11 Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine;

Lakini wale ambao siku zote wao wako katika maisha ya Kimungu  Luka 2:49  Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? hawatakuwa na muda wa kutumia muda wao katika mambo ya watu wengine, daima watakuwa wakitembea katika busara ya Mungu na kutenda mambo yao kwa haki na uadilifu wa pekee. Wakorinto 4:5 basi ninyi msihukumu jambo kabla ya wakati wake; tukumbuke kuwa kila mtu  anatakiwa kuwa tayari kuhangaika na mambo yanayomhusu yeye  mwenyewe; Katika jamii yetu, tukumbuke kuwa kuna watu ambao wao kazi yako kubwa ni kulaumu na kukosoa tu hawawezi kuona kitu au jambo nzuri lolote kutoka kwa wengine; na pengine ukibahatika kuona nini kinaendelea katika maisha yao utashangaa kwa nini wako msitari wa mbele kuhukumu wenzao; pengine maisha yao na hukumu ambazo wanazitoa kwa wengine hazilingani kabisa.

Tafakari yetu leo inaendelea kutukumbusha kuwa  tunapoteza muda wa kufanya mambo yetu mazuri yampendezayo Mungu kwa kujihusisha  na mambo ya watu wengine; lakini utagundua kuwa jinsi kuwahukumu wengine katika mambo ambayo hayana msingi ndivyo tunavyowasaidia wao kufanikiwa Zaidi na kuwa karibu na Mungu na kufanikiwa Zaidi. Tunatakiwa kuanza kusafisha nyumba zetu kabla hujeanza kuona uchafu katika nyumba ya wengine kwa kutumia ulimi wetu.

Na pale tunapogundua  kuwa maisha hayako vizuri yarekebishe na tuyasimamie na sio kutumia muda mwingi katika kuhangaika na maisha ya watu wengine. Kwa nini uwe na uchungu na maisha ya watu wengine? La msingi ni vizuri tukajifunza kutilia mkazo maisha yetu na kuziondoa changamoto zetu za maisha. Ni rahisi kwetu kuona Kibanzi katika jicho la wenzetu na kushindwa kuona boriti katika jicho lako au langu;

Kwa kweli wakati mwingine inatakiwa tuamue kufunga masikio na kuziba macho ili tuweze kusonga mbele; chochote ambacho tutafanya hakitaweza kumridhisha kila mtu na kila mtu atatoa hukumu yake; kama tusipokuwa makini hao ni waharibifu wa safari yako ya maisha; midomo yetu  imejaa masengenyo na majigambo; midomo yetu inapinga uumbaji wa Mungu dhidi ya wenzetu; maneno kama mbaya, hana elimu ya kutosha; hana kazi nzuri; mwone kwanza: je haya maneno yanaashiria nini katika uumbaji wa Mungu; Je Yesu alipokuja kutukumbo sisi kutoka katika misha ya dhambi aliangalia vitu hivyo? Jibu hapana alitukomboa sisi kulingana na njisi tulivyo bila kuangalia ukubwa au uwingi wa dhambi zetu; na jambo njema pamoja na mapungufu yetu sote tumepokea kipimo sawa.

Tukisoma Injili ya Mathayo 7:5 Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.  inatukumbusha kuwa sisi tuko makini sana katika kuhakiki maisha ya watu wengine na mapito yake; swali la kujiuliza je sisi tunafanikiwa vipi na kupata kibali cha kuwahukumu wengine? Au nasi tumekuwa katika kundi la wanafiki kwa kupenda tu kuhukumu? Tunatakiwa kuwa kioo cha matendo yetu na busara yetu kuwa mfano kwa wengine? Tusome sana neno la mungu;

Tukisoma kitabu cha Zakaria 4:10 Maana ni nani aliyeidharau siku ya mambo madogo? Kwa kuwa watafurahi, nao wataiona timazi katika mkono wa Zerubabeli; naam, hizi saba ndizo macho ya Bwana; yapiga mbio huko na huko duniani mwote.  katika maisha vitu vinakuwa taratibu havilipuki tu kutoka kusikojulikana. Kila mafanikio yanahitaji uwajibikaji na uvumilivu. 

je unaona raha gani kuongelea  mambo mabaya juu myu mwingine? kwa nini usiongelee mazuri au pale alipokosea usimrekebishe kwa upole na kwa busara iliyojaa unyenyekevu? itakuwa ni jambo la kufurahia kwa wakati huu wa mfungo na toba ni kujifunza kutenda kila jambo kwa haki kama Yesu alivyotutendea na uthibitisho wa hili ni kitendo cha kukubali kufa msalabani kwa wokovu wetu;

ushauri wangu kama unatenda jambo njema na unahukumiwa ni wakati wa kushukuru sana kwani  unafanya jambo nzuri ambalo linawaumiza na wanataka kukurudisha nyuma; kumbuka ukiwaruhusu na kuwapa nafasi ya kukukatisha tamaa ujue kuwa  nawe mwisho wako utakuwa umefika. Kama Yesu angesikiliza kelele zote za walimu wa sheria na wayahudi ambao walikuwa wanampinga; sisi tusingeweza kupata wokovu wetu huu ambao tunaufurahia leo. La msingi ukikabiliwa na mtihani wa aina hii simama kidete na ujipanga vizuri kwani ushindi wako unakaribia. Methali 18:21 mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; na wao waupendao watakula matunda yake.

Inasikitisha sana leo kuona jamii na jumuia zetu zinatawaliwa na nguvu ya masengenyo; wivu na undumila kuwili . hivyo kwa kweli kama tunapenda kufurahia maisha mazuri lazima tujiepushe sana kuutumia ulimi wetu katika kusema mambo mabaya juu ya wenzetu. Metali 6:17 mambo ambayo yanamchukiza sana bwana Macho ya kiburi, ulimu wa uongo na mikono imwagayo damu isiyo na hatia.

Tukumbuke kuwa tunapokuwa tuko midumo juu tayari kuwahukumu na kuwalaumu na kuwahukumu wenzetu, Mungu kamwe hana muda wa kutusikiliza yeye wakati huu anafanya kama hatusikii na utuandalia adhabu,  mfano wa Yesu na kundi la watu waliompelekea mwanamke alifumaniawa katika tendo la unzinzi. Pamoja na kufafanua sheria zote kuhusiana na kosa hilo Yesu alikaa kimya kama vile hawasikii, aliponyanyuka aliwauliza swali kama kuna mmoja wenu asiye na dhambi awe wa kwanza kumrushia  mama huyu; Yohana 8:7. Fundisho hapa ni moja tu hukumu kama wewe hujetenda dhambi yeyote ile; tujenge upendo wa kweli kati yetu upendo ambao huubagui; hii ndio tafakari yetu ya wiki hii.

Amina                   Amina            AMINA

Emmanuel Turuka

2017


No comments:

Post a Comment