Tafakari ya leo dhana kubwa kama tulivyofundishwa katika injili mara kwa mara yatupasa kushukuru kwa kila jambo. Hii ndio tafakari yetu ya leo;
WELCOME - KARIBUNI SANA
GOD’S PROMISES ARE NEW EVERY MORNING” LAMENTATION 3;23
“All our dreams can come true – if we have the courage to pursue them.” - Walt Disney
Saturday, May 7, 2016
Friday, May 6, 2016
ASANTE SANA MAMA
May 6
Tafakari ya leo tunapokaribia kusherekea siku ya kuwakumbuka mama zetu ambao wametufikisha hapa tulipo tuna kila sababu ya kumshukuru sana Mungu.Upendo wa mama ni wa ajabu ambao haulinganishwi na kitu chochote kile; hata ukimkasirisha vipi atakasirika na baada ya Muda tu atasamehe na kusahau na kurudisha upendo wake wote kwako. Je kwa nini tusiseme asante sana Mama na sina chochote cha kukulipa zaidi ya kukuombea tu kwa mungu ili neema zake ambazo hazina mipaka zizidi kutawala maisha yako amina.
Thursday, May 5, 2016
NAKUTEGEMEA MUNGU WANGU
MAY 5
Tafakari yetu leo inalenga na kusisitiza kuwa pamoja na uelewa wetu ambao ni kazi ya mikono ya Mungu wetu bado tegemeo letu liko juu yake; yeye pekee yake anaweza kusimamisha Jua na kila kitu kwa neno lake tu; Hivyo tusijifanye kuwa sisi hatumtegemei mungu.
Wednesday, May 4, 2016
WAACHENI WATOTO WADOGO WAJE KWANGU
May 4
Mathayo 18: 3-4
Tafkari yetu leo tunaangalia jinsi Yesu alivyotuagiza kuwa tukiwa
kama motto mdogo ni rahisi sana kuingia katika ufalme wa Mungu; Je Kwa nini
yesu anataka sisi tuwe na fikra na akili za motto mdogo katika kuridhi ufalme
wa mbinguni? Watoto wadogo mara zote ni wategemezi wa wazazi wao kwa kila kitu;
ni wasikivu, na pale wanapokosea wataumia watalia lakini mwishoni
hujinyenyekeza na kuomba msamaha, hawana kiburi, hawafikirii madaraka , wala
mali na kila kitu mbele yao wanachokipata wanashukuru na kufurahia; hupenda
kujifunza na hata wakikosolewa hucheka na kujaribu tena;
Tafakari yetu leo wazo kubwa ni ugumu wa sisi kama watu wazima
ambao tayari tumeshakuwa na akili zetu zimeshakuwa na tunakuwa na ugumu wa
kujinyenyekeza mbele ya mungu tukitambua kuwa sisi tunaweza kujitegemea sisi
wenyewe na hatuhitaji msada wa Mungu; Yesu hapa anatukumbusha kuwa ili ukuu war
oho unahitaji unyenyekevu ambao watoto wanao na sisi watu wazima tunapingana
nao; tukumbuke kuwa unyenyekevu ni hatua ya kiroho ya kukua na sio hatua ya kujidumaza; Yesu
anatufundisha kuwa lazima tubadilike kama tunataka kuingia katika ufalme wa
mbinguni; Lazima tutubu makosa yetu kwa moyo na kuweka kusudio la kuacha
kutenda dhambi au kuendelea kutenda dhambi. Lazima tabia zetu kuhusu dhambi
ziwe za kupinga dhambi.
Tafakari yetu tukisoma 1 Wakoritho 14: 20 inatukumbusha
kuwa Ndugu zangu, msiwe watoto katika
akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu
mkawe watu wazima. Akili ya
watotohawafikirii mabaya; ma hawafikirii kutendewa mabaya humpenda kila mtu,
humwamini kila mtu, humfurahia kila mtu wamwonaye; hivyo sisi kama wakristo
tunatakiwa kubadilika kuwa wema, kuishi katika maadili mema, kutenda mema, na
tukifanya hivyo thawabu yetu itakuwa kubwa mbele ya Mungu; ndio hata tukisoma
kutoka Injili ya Yohana 3:3-5 Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin,
nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu. Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee?
Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa? Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa
maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. Kwa kuzaliwa kwa mara nyingine ni kuwa tayari
kubadilika na kuuvaa unyenyekevu ambao ni msaada mkubwa katika matendo yetu
katika kukamilisha safari yetu ya Mbinguni;
Tafakari yetu inatukumbusha kuwa Mtoto hana hadhi yeyote ndani ya
familia au jamii; kwa vile huonekana kuwa ni tegemezi basin a hana nafasi ya
kufanya maamuzi yeyote; Hili ni tatizo kubwa kwetu kwani tunapenda kuheshimiwa,
kunyenyekewa, hata wakati mwingine kuabudiwa; tunatakiwa tuwe watu ambao sio
kitu katika ulimwengu huu bali tukijua kuwa Mungu ndio tegemeo letu na ngao na
kinga yetu; Kama vile watoto wanavyowategemea wazazi wao kwa kila kitu nasi ni
wakati wetu wa kumtegemea Mungu kwa kila kitu.
Hii ndio tafakari yetu ya leo Amina
Emmanuel Turuka
Tuesday, May 3, 2016
JE WEWE NI MKE WA LUTU?

May 3
Mwanzo 19:26
Tafakari ya leo tunatafakari maisha yetu hapa dunia kwa kuangalia
zaidi lengo letu kubwa na hatima ya maisha yetu tunaielekeza wapi? Yesu kupitia
injili ya Luka 17: 28-29 Na
kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa,
walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga; lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na
kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote. Bwana wetu Yesu Kristo alituonya kuwa Mke wa Lutu
alikuwa Baridi, hajali, hana utii sio tu kwa mumeo hata kwa Mungu ndio sababu
hukumu ya mungu alishuka juu yake; Kama uilivyokuwa kwa Adam na Hawa ndivyo
ilivyokuwa na Mke wa Lutu; Aliambiwa asigeuke nyuma na akageuka nguzo ya Chumvi
kwa kupenda kuishi katika ulimwengu wa dunia na sio ulimwengu wa Kimungu.
Tafakari yetu inatukumbusha kuwa tulio wengi leo hii ni kama Mke
wa Lutu, hatusikii sauti ya Mungu na maelekezo yake, na kama tunaisikia basi
hatuko tayari kufuata haya maelekezo yake na tunaishia kuwa Nguzo ya chumvi
ambazo zinatemebea na hazina huhai wa kimungu. Mathayo 24:12 inatukumbusha
kuwa na kwa sababu ya kuongezeka
maasi, upendo wa wengi utapoa; Kama ilivyokuwa kwa mke wa Lutu kuwa
pamoja na kuishi na mume ambaye alikuwa akimwogopa na kufanya kazi na Mungu kwa
imani kubwa na Mungu Kuwapa zawadi ya Kuishi zaidi pale alipoamua kuwasha moto
wa kibiriti na kuiingamiza Sodoma, Mke wake alishindwa kutembea katika Mwendo
huu wa imani na kumwogopa Mungu.
Tafakari yetu inatukumbusha kuwa wakati huu
Sodoma ilikuwa imejaa uchafu wa kila aina; hivyo mke wa Lutu sio tu alihamia
Sodoma bali Sodoma ilihamia ndani ya Nafsi yake; alikuwa mwanamke ambaye
alipenda na kuabudu anasa ambazo zilikuwa zikifanyika Sodoma; Ndio maana
hakuweza kusikia sauti ya Mungu ambayo ilikuwa ikimwokoa katika maangamizi
alijawa na kiburi cha anasa na hivyo alishindwa kutekeleza agizo la Mungu.
Hivyo tatizo kubwa ni nini hapa? Mke wa Lutu aliupenda zaidi ulimwengu kuliko
kumpenda zaidi Mungu;
Kama ilivyo kwa mke wa Lutu hata sisi leo
tumesongwa sana na anasa za dunia hata ile damu ya yesu ambayo imetukomboa
hatuipi thamani kwani matendo yetu hayafanani na thamani ya Damu hiyo. Hata
hatufanyi majukumu yetu vile inavyotakiwa; hatuna nafasi ya kuwalea watoto wetu
katika maadili ya kimungu; muda wetu mwingi tunapotezea katika maisha ya anasa
za dunia hii; sauti ya Mungu daima inatuambia kuwa “Jiponye nafsi yako
usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani,
usije ukapotea”. Lakini hatusikii sauti hiyo na tunaendelea na maisha yetu ya
anasa za duniii hii.
Tafakari yetu leo inaendelea kutukumbusha kuwa tuache dhambi ya
kiburi ambayo ndio msingi wa dhambi nyingine zote; Tuwe wanyenyekevu tusikie
sauti ya bwana na kutekeleza maagizo yake; tukumbuke kuwa utii ni sadaka ya juu
sana, Yesu alituagiza kama tunampenda tutazishika amri zake; kutotii ni dhambi
mbaya sana; Mungu anafurahishwa na utii wetu kwake na amri, mafundisho yake
kwetu sisi kupitia Mwokozi wetu yesu kristo. Tunakumbushwa kuwa tusiwe kama Mke
wa Lutu aliyeangalia nyuma kwa kufikiri kuwa dunia hii ndio zaidi kwetu kuliko
Mungu. Tunatakiwa kuacha dhambi ya kiburi na kutekeleza utii kwa Mungu katika
kuishi maisha yetu kama yeye anavyotaka sisi tuishi;
Tafakari yetu inatutadharisha na matendo yetu
ya kuangalia Nyuma; Tumeagizwa tuangalie mbele ili tuweze kufuzu kuingia katika
nyumba ya Mungu; lakini kwa kuangalia nyuma kama mke wa Lutu tunakuwa
tumejiondoa wenyewe katika kushiriki utukufu wa Mungu; tukisoma Luka 9: 61-62
Mtu mwingine pia akamwambia, Bwana, nitakufuata; lakini, nipe ruhusa kwanza
nikawaage watu wa nyumbani mwangu. Yesu akamwambia, Mtu
aliyetia mkono wake kulima, kisha akaangalia nyuma, hafai kwa ufalme wa Mungu.
Hatutakiwi kabisa kuangalia nyuma tunapoutafuta ufalme wa Mungu; Kuangalia
nyuma hapa maana yake ni nini? Tunayaangalia maisha yale ya zamani, ya ulevi,
uzinzi, uwongo, wizi, chuki, na kadhalika; tukumbuke kuwa hakuna maisha ya
baadae bila mipango hiyo kupokea maelekezo ya Mungu ndani ya Nyoyo zetu. Agizo
ambalo tunapata leo hatutakiw kugeuka nyuma na kuyarudia maisha yaliyojaa
dhambi. Tumepata Baraka ya kukombolewa na damu ya Yesu jukumu letu sasa ni
kusonga mbele na kamwe kuto geuka Nyuma.
Hii ndio tafakari yetu ya leo;
Emmanuel Turuka
TAZAMA ILIVYO NJEMA NDUGU WAKIKAA KATIKA UPENDO
May 2
1Peter 3:8
Tafakari ya leo inatukumbusha kuhusu umuhimu wa wa kuishi pamoja
kwa upendo na maelewano; kama waraka wa 1 Petro 3:8 unavosema Neno la mwisho ni hili; mwe na nia moja, wenye
kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu; kama Waraka wa Waefeso 4: 2-8 unavyoyukumbusha kuwa
sote lazima tuishi kwa upendo na kuwa wamoja tukizingatia kuishi katika unyenyekevu
wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; na kujitahidi
kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika
tumaini moja la wito wenu. Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na
katika yote na ndani ya yote. Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo
cha kipawa chake Kristo. Hivyo
husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa.
Tafakari yetu vile vile inasisitiza kuwa bibilia
inatukumbusha kuwa tunatakiwa kuishi kwa kupendana pamoja kama waraka wa Warumi
12: 15- 18 Furahini pamoja nao wafurahio;
lieni pamoja nao waliao. Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie
yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa
kujivunia akili. Msimlipe
mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote. Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu
wote. Tukumbuke kuwa pale penye
amani na upendo furaha ya bwana utawala na watu wanakua katika neema ya Mungu
na maarafa ya mungu; umoja wa kweli huzaliwa miongoni mwetu. Lakini pale ambapo
pana chuki amani hutoweka neema ya Mungu na maarifa yake hutoweka pia; woga
hutawala, uwazi hupotea shetani natawala na kuleta maangamizo ambayo mwisho
wake humwangamiza mwanadamu na kumfanya kujenga kiburi na majivuno.
Tafakari ya leo neno la msingi katika kuishi
kwa upendo na wezetu linatawalia na neno heshima; tukiweza kuwaheshimu wezetu
na kuwapa haki wanayostahili upendo utatawala maisha yetu, na hakuna kiburi
wala chuki kitapata nafasi katika maisha yetu; mwenyezi Mungu anatamani sana
sisi tuwe tofauti katika dhana nzima ya kuishi pamoja kwa kupendana; Mungu
anataka sisi tuwe chanzo cha Baraka kwa wenzetu; tuwe watu ambao hatutamani
wenzetu wapate shida au tabu; na pale wanapofanikiwa tusiwe watu wa kwanza
kuwaonea wivu na kuwachukia. Bali tushangilie pamoja katika mafanikio yao na
tulie pamoja na kuwapa nguvu katika shida zao.
Tafakari yetu leo inatukumbusha kuwa ili tuweze
kufanikiwa lazima tukubali na kujikataa wenyewe; tusiwe watu ambao tunajijali
wenyewe na kuona vitu bora vyote ni vyako na wengine hawastahili; bali
tunahitaji kuwa wenyenyekevu na kuweka matakwa ya wengine mbele zaidi katika
kuleta maisha ya upendo wa kweli miongoni mwenu na kufanikisha amri ya upendo
wa kuishi pamoja. Ni jambo gumu ambalo linasumbua katika utekelezaji wake. Maisha
yetu yamejaa choyo, umimi, wivu na unafiki; ni neema tu itakayo tusaidia
kutekeleza dhana ya kuishi kwa pamoja kama ndugu kama tutaweza kusoma na
kuelewa nyakati za Mungu na maarifa yake, katika kutekeleza upendo wa kweli .
Hii ndio tafakari yetu ya leo; Amina
Emmanuel Turuka
Sunday, May 1, 2016
TUMSHUKURU BWANA KWANI NI MWEMA
mAY 1
ZABURI YA 107
Tafakari ya leo tunakila sababu ya kumshukuru Mungu kwa upendo wake na kwa Kutujalia kuweza kuanza Mwezi Mpya wa May tukiwa na tunaendelea kufunikwa na damu ya Mkombozi wetu, na kuendelea kuneemeka na baraka na neema zake katika maisha yetu ya kila siku. Mzaburi ametuonyesha njia zote ambazo Mungu anatusaidia kama alivyowasaidia wana wa Israeli kutoka katika mikono ya Farao na kuwalisha na kuwannemesha wakati wote wa safari kwenda katika makazi mapaya. Je wewe na mimi tunaendelea kumshukuru Mungu kila siku?
1 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 Na waseme hivi waliokombolewa na Bwana, Wale aliowakomboa na mkono wa mtesi.
3 Akawakusanya kutoka nchi zote, Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini.
4 Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa.
5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.
6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa.
8 Na wamshukuru Bwana, kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
9 Maana hushibisha nafsi yenye shauku, Na nafsi yenye njaa huijaza mema.
10 Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma,
11 Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, Wakalidharau shauri lake Aliye juu.
12 Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa wala hakuna msaidizi.
13 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
14 Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akayavunja mafungo yao.
15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
16 Maana ameivunja milango ya shaba, Ameyakata mapingo ya chuma.
17 Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao, Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa.
18 Nafsi zao zachukia kila namna ya chakula, Wameyakaribia malango ya mauti.
19 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.
21 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
22 Na wamtolee dhabihu za kushukuru, Na kuyasimulia matendo yake kwa kuimba.
23 Washukao baharini katika merikebu, Wafanyao kazi yao katika maji mengi,
24 Hao huziona kazi za Bwana, Na maajabu yake vilindini.
25 Maana husema, akavumisha upepo wa dhoruba, Ukayainua juu mawimbi yake.
26 Wapanda mbinguni, watelemka vilindini, Nafsi yao yayeyuka kwa hali mbaya.
27 Wayumba-yumba, wapepesuka kama mlevi, Akili zao zote zawapotea.
28 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
29 Huituliza dhoruba, ikawa shwari, Mawimbi yake yakanyamaza.
30 Ndipo walipofurahi kwa kuwa yametulia Naye huwaleta mpaka bandari waliyoitamani.
31 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
32 Na wamtukuze katika kusanyiko la watu, Na wamhimidi katika baraza ya wazee.
33 Amegeuza mito ikawa jangwa, Na chemchemi za maji zikawa nchi ya kiu.
34 Nchi ya matunda mengi ikawa uwanda wa chumvi, Kwa sababu ya ubaya wao walioikaa.
35 Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji, Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.
36 Maana amewakalisha huko wenye njaa, Nao wametengeneza mji wa kukaa.
37 Wakapanda mbegu katika mashamba, Na kutia mizabibu iliyotoa matunda yake.
38 Naye huwabariki wakaongezeka sana, Wala hayapunguzi makundi yao.
39 Kisha wakapungua na kudhilika, Kwa kuonewa na mabaya na huzuni.
40 Akawamwagia wakuu dharau, Na kuwazungusha katika nyika isiyo na njia.
41 Akamweka mhitaji juu mbali na mateso, Akamfanyia jamaa kama kundi la kondoo.
42 Wanyofu wa moyo wataona na kufurahi, Na uovu wa kila namna utajifumba kinywa.
43 Aliye na hekima na ayaangalie hayo; Na wazitafakari fadhili za Bwana.
Hii ndio tafakari yetu ya leo; Amina
Emmanuel Turuka
Subscribe to:
Posts (Atom)

